Skip to main content

‘’WAADHIBIWE WAZAZI WATAKAOWAKIMBIZA WATOTO WAO MAHAKAMANI’ : WADAU PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WADAU wa haki jinai kisiwani Pemba, wamesema ili kupunguza matendo ya ukatili na udhalilishaji, lazima kuwe na kifungu cha sheria, kinachowaadhibu wazazi na walezi, watakaobainika kuwatorosha watoto wao.

Walisema, wazazi na walezi kwa sasa, wamekuwa wakiwatorosha watoto wao, iwe wa kike au kiume, mara baada ya kujitokeza kwa matendo hayo.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, juu ya uwepo wa wimbi kubwa la kufutwa kwa kesi za udhalilishaji, walisema kwa sasa, kumeibuka mtindo wa baadhi ya wazazi kuwatorosha watoto wao.

Walisema, hayo hujitokeza kwa wazazi wa upande wa mtoto wa kike, na hasa ikiwa tayari wameshachukua rushwa au wameshaandaa mipango ya kuwafungisha ndoa.

Mmoja kati ya wanaharakati hao, Dina Juma kutoka Jumuiya ya PEGAO, alisema wapo wazazi wamekuwa hawapendi kuendelea na kesi za watoto wao mahakamani, hivyo njia nyepesi ili kuiua kesi hiyo ni kumtorosha mtoto wake.

‘’Maana wanajua kuwa, mtoto aliyedhalilishwa huwa ni shahidi nambari moja, hivyo ikiwa ataitwa mahakamani vikao vinne hajaenda, chatano mara kesi inaweza kuondolewa, na kisha kuwafungisha ndoa,’’alieleza.

Nae mwanaharakati Tatu Abdalla Msellem, alisema wazazi wa upande wa mtoto wa kike, hufanya hivyo baada ya kughilibiwa na upande wa mtuhumiwa, na wengine hufanikiwa.

‘’Kwa mtindo wa sasa, wa wazazi hasa wa watoto wa kike wa miaka 15 hadi 17 kuwakimbiza watoto wao kwa tamaa ya fedha ama ndoa, matendo hayo hayataondoka,’’alieleza.

Nae Afisa Mawasiliano wa TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Gaspery Charles, alisema kama hakikuwepo kifungu kizito cha kuwaadhibu wazazi wenye tabia hiyo, matendo hayo hayatopungua.

‘’Ifike wakati sasa kuwepo na kifungu cha sheria, ambacho kinataja adhabu kwa wazazi, watakaochangia kesi za watoto wao kufutwa au kuondolewa mahakamani,’’alishauri.

Nae mwanaharakati Hafidh Abdi Said, alisema hata wazazi wa vijana wa kiume, wamekuwa wakiwakimbiza, baada ya kuona wametenda makosa mbali mbali.

‘’Hii tabia inaweza kuondoka, ikiwa sasa sheria itaweka wazi, kuwa, wazazi au walezi waliochangia kukimbizwa kwa kijana (mtuhumiwa), ikiwa watawekwa ndani hadi kijana wao arudi,’’alishauri.

Aliyekuwa Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini Pemba, Tedie Mchomvu, alisema alifanikiwa kumpata mshitakiwa Khamis Juma Chumu ‘soda’ (76) mkaazi wa Mtoni wilaya ya Chake chake, aliyembaka mtoto wa miaka 13, baada ya kukimbia na kisha kushikiliwa kwa watoto wake.

 

Alisema mpango huo, unaweza kusaidia kwa wale wazazi na walezi, wenye tabia ya kuwaficha ama kuwakimbiza watoto wao, iwe wa kike ama kiume, ili wasiendelee na kesi mble ya vyombo vya sheria.

 

Wakili wa kujitegemea Pemba Zahran Mohamed Yussuf, alisema haoni mantiki kwa vyombo vya ulinzi na usalama, kuwashikiliwa watu wengine kwa kosa mtu mmoja.

 


‘’Kwa vile Jeshi la Polisi linajiendesha kwa mujibu wa sheria, lazima liwashikilie wale ambao wanawatuhumu, lakini sio ndugu na jamaa wa mshtakiwa, huko ni kukiuka haki za binadamu,’’alieleza.

 

Mratibu wa Dawati la Jinsia la wanawake na watoto wilaya ya Wete Hassan Khamis anasema, njia ya kupunguza kwa wibi la kesi hizo, ni sheria kuongezewa meno.

Mkuu wa Idara ya Ustawi wa Jamii Pemba Omar Mohamed yeye anasema, wamekuwa wakikosa ushirikiano kwa watoto hao, wanapofikishwa mahakamani, aidha ni kuwa wanatishwa na wale wanaowabaka au kuwalinda wapenzi wao.

Aidha wadau hao, walisema kesi nyingi ambazo huishia kufutwa ni zile ambazo, watoto wa kike wana umri katia ya miaka 15 hadi 17, jambo ambalo linarejesha nyuma jitihada za kupunguza matendo hayo.

Hakimu wa mahakama maalum ya kupinga udhalilishaji wilaya ya Wete Ali Abdulrahman Ali, alisema wamekuwa wakiumisha kichwa hasa kesi za watoto wenye umeri katia ya miaka 15 hadi 17.

“Hatuwezi kumtia hatiani mtuhumiwa kwa ushahidi wa daktari pekee kwa sababu, cheti cha daktari kinaonesha mtoto kutendewa kitendo (ubakaji) na sio kujulikana mtuhumiwa”, anafafanua.



Salma Hamad Omar mwenye umri wa miaka 19 mkazi wa Mzambarau Takao anaeleza, watoto wenye umri huo hukataa kutoa ushahidi kwa sababu, hao wanaume ni wachumba zao, hivyo wanaona shida kusema wamebakwa.

Mtoto mwe umri wa miaka 17 Maryam Faki Ali mkaazi wa shehia ya Minungwini anaeleza, watoto wenye umri huo hawapendi kutoa ushahidi kwa sababu huwa kuna makubaliano baina yake na mwanaume.

Takwimu za jeshi la Polisi wilaya Wete za mwaka 2020 zinaonyesha kesi 85 za udhalilishaji ziliripotiwa, huku kesi 30 zikiwa ni kesi za ubakaji zinazohusisha watoto kati ya mika 15 hadi 17.

Kati ya hizo kesi, kesi nne (4) tu ambazo zilitolewa hukumu, huku 17 zikfutwa katika kituo cha Polisi, kesi saba (7) zilifutwa mahakamani na kesi mbili (2) zikiwa katika upelelezi.



Wakati mwaka 2021, kesi zilizoripotiwa zilikuwa 44, ambapo kesi 28 zikiwa za watoto wenye umri wa miaka 15 hadi 17, ambapo ni kesi nne (4) tu zilizotolewa hukumu kama ilikvyokuwa kwa mwaka 2020, huku kesi 12 zikifutwa Polisi na saba (7) mahakamani na kesi tano (5) upelelezi wake bado unaendelea.

                                                       MWISHO. 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch