Skip to main content

KIJALUBA iSAVE ZANZIBAR, MRADI JUMUISHI UNAOKUJA NA MBINU ZA KISASA KUKUZA PATO

 

               



NA HAJI NASSSOR, PEMBA@@@@

KIJALUBA iSAVE Zanzibar, ni mradi jumuishi, unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi.

Kupitia mradi huu, watu hao wenye ulemavu wa aina mbali mbali, utawajengea uwezo kuhusu maisha yao wenyewe na jamii zao, kwa ujumla.

Maana, lengo kuu hasa la mradi huu wa Kijaluba iSAVE Zanzibar, unaangazia zaidi, kukuza uwezo wa watu hao, kwa kujenga mitazamo chanya, juu ya ushiriki wao, na kujiingiza katika shughuli za kujipatia kipato.

Kipato hicho, hasa kwa aina ya maradi huo ulivyo, ni kupitia katika vikundi vyao vya kuweka na kukopa ‘saccos’ ambapo kwa baadhi ya maeneo, huitwa vikoba.

MBINU ZA UTEKELEZAJI WA MRADI HUO

Kwa mujibu wa Msaidizi Afisa Mradi wa kijaluba Mohamed Salim Khamis, anaefanyia kazi zake Pemba, anasema kwanza ni kuwawezesha watu hao kupata kipato.

‘’Lakini jengine ni kuwezeshwa, ili wawe na ushiriki kamili katika miradi na maendeleo ya jamii kwa ujumla, kutokana na mazingira yao,’’anasema.

Mbinu nyingine aliyoitaja, ambayo mradi utakwenda kushughulika, ili kuhakikisha kundi la watu wenye ulemavu wanakuza pato lao, ni kuangalia vikwazo vinavyowakatisha tamaa.

‘’Kwa mfano, kama jamii wanamitazamo kuwa, watu wenye ulemavu hawawezi, tutoa elimu, au kama tutagunuda wanatengwa, tutaelezea haki zao kwa jamii yao,’’ anaeleza.

Watu hao wenye ulemavu kupitia mradi huo wa miaka miwili, wataanzishiwa vikundi vya kuweka na kukopa (iSAVE groups) na kuviunganisha na taasisi za kifedha.

Kumbe, hapa baada ya kupewa mbinu za kisasa kwenye vikundi vyao vya kuweka na kukopa, kisha wataunganishwa na tasisi za kifedha kama benki, ili sasa waweza kuomba mikopo.


Hapa Msaidizi Afisa Mradi huo wa kijaluba Mohamed Salim Khamis, anafafanua kuwa, pamoja na yote hayo, kundi hilo litajengewa uwezo kwenye eneo la ujasiriamali.

Walishasema wahenga kuwa, mgagaa na upwa wala hali ugali mkavu, hapa msemo huu utasadifu, kwa kundi la watu wenye ulemavu, maana wanagaa gaa kwenye ufukwe wa Kijaluba.

‘’Baada ya kuanzishiwa vikundi hivyo, na kuwiva kiujasiriamali hapo watakuwa tayari sasa kuombewa mikopo kwenye tasisi za kifedha kama PBZ, CRDB, NMB na Idara ya Uwezeshaji,’’anafafanua.

Anasema, walengwa wakuu wa mradi, ni watu wenye ulemavu wakiwemo watoto, wanawake, wanaume pamoja na vijana, ambapo watajumuisha angalua asilimia 60.

Akimaanisha kuwa, kwa mfano kila watu 10 wataokanufaika na mradi huu jumuishi, basi sita wawe watu wenye ulemavu na wanne wale wasiokuwa na ulemavu.

‘’Kwa hiyo, wanajamii wa wilaya ya Chake chake kwa Pemba na wilaya ya Kusini kwa Unguja, ndio ambao watafikiwa na mradi huu, ambapo shehia za wilaya hiyo ni eneo la majaribio,’’anafafanua.

WATEKELEZAJI MRADI

Hapa Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, Fat-hya Mussa Said, anasema, mradi unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya shirikisho la Jumuiya za watu wenye ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ pamoja na TAMWA-Zanzibar.

Akaeleza kuwa, kazi yao kubwa katika mradi huu, ni kuhakikisha kila kitakachofanywa ndani ya mradi, basi jamii nyingine inapata taarifa kwa kule TAMWA, kuwatumia waandishi wa habari.

‘’TAMWA tunaguswa na haki za watu wenye ulemavu, na ndio maana tukawa washirika wa utekelezaji wa mradi huu, ambao unafadhiliwa na Chama cha watu wenye ulemavu cha Norway ‘NAD’, anafafanua.

Mratibu huyo, anaona kama jamii ya wilaya ya Chake chake itajali kwa kiasi kikubwa haki za watu wenye ulemavu, mradi huo utatekelezwa vyema.

Kumbe anasema, kila mmoja akizijali kwa vitendo haki za ndugu yake mwenye ulemavu, maana hakuna sheria, kanuni wala sera iliyoandikwa pahala popote, kuwabagua. 





‘’Leo wapo makatibu wakuu watu wenye ulemavu, wapo wakurugenzi, wenyeviti wa taasisi mbali mbali, ni ishara kuwa wanauwezo mkubwa,’’anasema.

Hili liliongezewa nguvu na Msaidizi Afisa Mradi huo Mohamed Salim Khamis, akisema kama jamii haiwakubali watu wenye ulemavu, mradi huo unaweza kuwa mgumu.

‘’Naamini kwa vile watu wa wilaya ya Chake chake wanajali mno haki za watu wenye ulemavu, hata utekelezaji wa mradi huu wa Kijaluba, unaweza kuwalaini sana,’’anafafanua.

HATUA ILIYOFIKIWA

Tayari waalimu wasimamizi wa vikundi vya kuweka na kukopa wameshapewa mbinu za kwenda kuihamasisha jamii, na hasa kundi la watu wenye ulemavu, kuanzisha vikundi vya kuweka na kukopa.

Mwalimu wa mafunzo hayo Bakar Haji Bakar kutoka TAMWA-Pemba, aliwaeleza wasimamizi hao ngazi ya shehia, wahakikishe, hata kwenye uongozi wa vikundi kipaumbele ni watu wenye ulemavu.

‘’Kwa mfano wale viongozi sita wa mwanzo, katika kila kikundi, watu wanne, wawe ni watu wenye ulemavu, maana pia mradl huu unalenga kutoa fursa za uongozi kwao,’’anasema.

Kumbe mradi huu utakapotia nanga Disemba 2024, kutoka pale ulipoanza Novemba 2022, watu wenye ulemavu kwa wilaya ya Chake chake, wewe wameshaiva kiuongozi.

Kupitia mradi huu wa majaribio, utaona kuna wananchi 1876, wakiwemo wanawake 1,122 na wanaume 750, kutoka wilaya za Chake chake Pemba na Kuisni Unguja, watanufaika.

Chakuzingatia tu ni kuwa, kila watu 60, kati ya 100, watakuwa ni wenye ulemavu mchanganyiko, tena waliomo kwenye shehia za wilaya ya Chake chake kwa Pemba na au wilaya ya kusini Unguja.

Watu hao, watawezeshwa kupitia vikundi maalum vitakavyoanzishwa katika kila shehia ya wilayani humo, ambapo kila kikundi, kitakuwa na wastani wa wanachama kati ya 25 na wasiozidi 30.



Afisa Utawala kutoka Shirikisho la jumuiya za watu wenye ulemavu Zanzibar ‘SHIJUWAZA’ kisiwani Pemba Aisha Abdalla Juma, yeye amefurahishwa, na ujio wa mradi huo.

Anaona sasa, utakwenda kuwaamsha watu wenye ulemavu, juu nafasi yao katika jamii, katika kujikwamua na umaskini unaowakabili.

‘’Omba omba sio agizo kwa watu wenye ulemavu, bali wanafanya hivyo kwa kutokujua, na ujio wa mradi huu tunategemea sasa kundi hili la wenzetu wenye ulemavu, watajiweza kiuchumi,’’anasema.

Kubwa, aliigeukia jamii ya wilaya ya Chake chake, kutoa kila aina ya ushirikiano, hasa katika kuhamasishana juu ya kushirikiana nao, katika kuanzisha vikundi hivyo.

Upande mwengine Mwezeshaji wa vikundi vya watu wenye ulemavu ‘CRP’ Fatma Abrahman Ali wa shehia ya Ole wilaya ya Chake chake, anaesimamia vikundi tisa, vyenye wanachama wastani wa 25 hadi 30 kwa kila kimoja.

Katika vikundi hivyo, kwa mfano chenye wanachama 30, ni lazima 20 wewe watu wenye ulemavu, kwani ndio hasa malengo ya mradi husika.

‘’Kwa saa tumemaliza mafunzo sisi waalimu wasimamizi, kisha tutakwenda kwa jamii, kuihamasisha namna ya uundaji wa vikundi vya kuweka akiba, ili sasa wapate kujikomboa,’’alifafanua.

Mwalimu wa vikundi hivyo kutoka ‘SHIJUWAZA’ Fatma Abdalla Issa, anasema kutokana na mafunzo waliokwishapatiwa, sasa wako tayari kwenda shehiani.

WALENGWA WA MRADI

Hidaya Mjaka Ali wa shehia ya Vitongoji wilaya ya Chake chake, mwenye ulemavu wa viungo, anasema wanausubiri kwa hamu mradi huo.

Nassra Issa Omar wa shehia ya Wawi, mwenye ulemavu wa uoni, anasema kama mradi huo utawafikia kwa vitendo, anaamini wimbi la watu wenye ulemavu, kuzitegemea familia zao, litapungua.

Khamis Mohamed Nassor wa Gombani, alisema jipya analoliona kwenye mradi huo, ni kujumuishwa wao na wetu wenye ulemavu, kuanzia uundwaji wa vikundi na uongozi.

‘’Ni kweli wenzetu wenye ulemavu walikuwa wakiachwa nyuma kwa muda mrefu, lakini sasa ujio wa mradi huu nao watapa mwanga wa kujitegemea,’’anasema.  

Mradi wa Kijaluba, ni jumuishi unaolenga kuwawezesha watu wenye ulemavu kiuchumi, kwa kule kuwajengea uwezo kuhusu maisha yao na jamii zao.

Mradi huo unatarajiwa, kukuza uwezo wa kundi hilo, samba mba na kujenga mitazamo chanja, juu ya ushiriki wao, kujiingiza katika shughuli za kujipatia kipato.

Aidha mradi huo ulioanza mwaka 2022, ukitarajiwa kumalizika mwaka 2024, utakwenda kushughulikia vikwazo vinavyowarudisha nyuma, watu wenye ulemavu.



Kwa sasa mradi huu, anatekeleza wilaya ya Kusini Unguja na Chake chake kwa Pemba, kama eneo la majaribio, ambapo walengwa wakuu ni watu wenye ulemavu wakiwemo vijana, watoto kwa asilimia 60 na 40 na watu wengine.

MIKATABA NA SHERIA YA WATU WENYE ULEMAVU

Kwa mfano kifungu cha 28 (1), (b) cha sheria ya watu wenye ulemavu Zanzibar, nambari 8 ya mwaka 2022, kinabainisha haki ya kufanyakazi na ajira kwa watu hao.

Nacho kifungu cha 31, kikasisitiza kuwa ni kosa kuwabagua, kuwadhalilisha, watu wenye ulemavu kwa sababu ya hali zao.

Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu, Ibara ya 27, unafafanua kuwa, nchi zilizoridhia mkataba, zinalazimishwa kutambua haki za kujipatia nafasi za kumudu maisha yao.

Ibara ikasisitiza nchi hizo Tanzania ikiwemo, kukuza upatikanaji haki ya kufanyakazi, ikijumuisha wale waliopata ulemavu wakiwa kazini, pamoja na kukataza ubaguzi.

                               Mwisho      


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch