Skip to main content

WATU WENYE ULEMAVU VIKUNGUNI WALILIA UKOSEFU WA DAWA ZAO



 NA ZUHURA JUMA, PEMBA @@@@

WATU wenye ulemavu katika kijiji cha Vikinguni shehia ya    Ng'ambwa Wilaya ya Chake Chake Pemba wameiomba  Serikali kuwawekea dawa zao katika vituo vya afya, ili kuwasaidia katika kupunguza makali ya magonjwa yanayowasumbua. 

Walisema kuwa, watu wenye ulemavu hasa wa akili pamoja na wenye kifafa wanahitaji watumie dawa kila siku ili kuimarisha afya zao, ingawa wakati mwengine hawatumii kutokana na kuzikosa dawa hizo ukilinganisha wengi wao hali zao ni duni kimaisha.

Wakizungumza na Zanzibarleo kijijini kwao walisema, dawa hizo ni tatizo katika kituo cha afya cha Vikinguni hali ambayo inawafanya wakanunue, jambo ambalo wakati mwengine wanashindwa kutokana na kukosa fedha.

"Kila siku watu hawa wanahitajia wameze dawa ili afya zao ziweze kuimarika lakini wakati mwengine tunashindwa kuwapa kwani mpaka tununue na hatuna uwezo", waliesema watu wenye ulemavu.

Nassir Suleiman Hamad alisema kuwa, wamekuwa wakipata usumbufu wakati wanapoanguka watu wenye kifafa na wenye ulemavu wa akili na wanapokwenda hospitali hukosa dawa.

"Kila siku tunapokwenda katika kituo cha afya na wagonjwa wetu hao tunaambiwa dawa hakuna, kwa hiyo tunasumbuka sana kwa sababu hatuna uwezo wa kupata dawa kwa kila siku", alieleza baba hiyo.

Kwa upande wake Maryam Ahmed Hemed alisema kuwa, kuna haja kwa Serikali kuwawekea dawa kwenye vituo vya afya ili kuondokana na usumbufu wanaoupata.




"Wakati mwengine tunakwenda hospitali kubwa kuomba dawa na ukiangalia pia ni usumbufu kwa sababu hatuna hata nauli ya kufikia huko, tunaomba tusaidiwe tunateseka", alisema.

Nae Fatma Hamad Khamis alisema kuwa, watu wenye ulemavu wa akili na wa viungo wengi wanaambatana na ugonjwa wa kifafa, hivyo kila siku wanatakiwa kumeza dawa, ingawa wakati mwengine wanashindwa kutokana na kukosa pesa ya kununulia dawa hizo.

"Wasipomeza dawa ni kama yale maradhi tunayapalilia, hivyo tunaomba tuonewe huruma kwa kupatiwa hizi dawa, ili zitusaidie", alieleza mwananchi huyo.

Afisa Mdhamini Wizara ya Afya Pemba Khamis Bilal Ali alisema, Wizara ya Afya ina mfumo wake wa kutoa matibabu katika hospitali na vituo vya Afya ngazi kwa ngazi, hivyo watu wenye ulemavu wa akili kliniki na daktari wao yupo katika hospitali ya Wilaya Vitongoji.

"Hivyo pale Vitongoji kwenye mfumo wa kuomba dawa, ikiwa tunazo tunawapatia kwa sababu wao ngazi yao wanaruhusika kutoa dawa hizo na matibabu yake", alifafanua.

Alisema kuwa, Serikali inaangalia makundi yote ingawa inatoa huduma kulingana na uwezo wa sehemu husika katika hospitali na vituo vya Afya kama ilivyo kwa vituo vya kujifungulia kwa mama wajawazito, kwamba huwezi kujifungulia kituo ambacho hakitolewi huduma hiyo, hivyo hivyo kwa watu wenye ulemavu.

Mdahamini huyo alieleza, kwa hivyo na wao matibabu yao ili yawe rahisi kwa kesi hizo, wanashauriwa wafike katika hospitali za Wilaya iliyopo vitongoji au Chake Chake kwa ajili ya kupata huduma hizo katika hali ya ubora.
                       MWISHO.


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch