Skip to main content

SHERIA YA ELIMU ZANZIBAR YATIMIZA MIAKA 41, WADAU WATAKA ICHUNGULIWE UPYA

 




 HABIBA ZARALI, PEMBA

LICHA ya sheria ya elimu Zanzibar nambari 6 ya mwaka 1982 kufanyiwa marekebisho ya mwaka 1993, ili kuimarisha upatikanaji wa elimu bora, lakini bado inaliliwa.

Sheria hiyo ambayo inaonekana kukosa mashiko ya kuwadhibiti wazazi na walezi kikamilifu wasioshughulikia watoto wasiokwenda skuli, au wanaokatisha masomo kwa kuwaozesha waume.

Baadhi ya vifungu hivyo ni kile cha 20 (1) na 22 cha sheria ya elimu Zanzibar, kwa kumuozesha mtoto ambae bado mwanafunzi.

Ambapo hapo mzazi atakuwa ni mkosa na akitiwa hatiani adhabu zake kwa kosa la kwanza anatakiwa kulipa faini isiyopunguwa shilingi 1,500 na isiyozidi 3,000.

Kosa la pili katika sheria hiyo ni faini isiyopunguwa 3,000 na isiyozidi 5,500 ambapo kosa la tatu atalipa faini isiyopunguwa 5,500 na isiyozidi 10,000 au kifungo kisichozidi miezi sita au vyote viwili.

Pamoja na sheria hii kuwa haimkatazi mwanafunzi kuoa au kuolewa kabla ya kukamilisha elimu ya lazima, lakini kifungu cha 20 (3) kinaeleza kuwa hakuna mwanafunzi anaesoma elimu ya lazima kuoa au kuolewa, kabla ya kukamilisha elimu hiyo.

Sheria ikafafanua kuwa, na ikitokezea imefungwa ndoa wakati ikiwa bado ni mwanafunzi, mwanafunzi huyo lazima afukuzwe masomoni.

WADAU/WANAHARAKATI WA ELIMU WANASEMAJE?

Wanaharakati na wadau mbali mbali wa elimu, wametoa kilio chao juu ya sheria hiyo ya elimu, huku wakisema ni vizuri sheria hiyo kurekebishwa.

Mwenyekiti wa Bodi skuli ya sekondari ya Mohamed Juma Pindua Hamdu Hassan Mohamed, anasema sheria hiyo imeshapitwa na wakati na inahitaji kurekebishwa.

Anasema sheria hiyo inaonekana kuwapa kiburi wazazi kwa kuwakatisha masomo watoto wao, na kuwaozesha mapema, jambo ambalo ni kuwakosesha haki yao ya msingi.

“Sheria hii kwa wakati ule basi ilikuwa inafaa, maana nakumbuka nilikuwa napokea mshahara 680 na ulikuwa ukitosha, lakini leo hii haina thamani kutokana na wakati uliopo,”anaeleza.

Mwanaharakati wa kupambana na vitendo vya udhalilishaji Tatu Abdalla Mselem anasema kutokana na faini kuwa ndogo, inamfanya mzazi kutoona thamani ya kumuachia mtoto wake kuendelea na elimu na badala yake kumuozesha mapema.

Anasema  katika kifungu cha sheria hiyo ambacho hakimkatazi mwanafunzi kuoa au kuolewa kabla ya kukamilisha  elimu ya lazima, wazazi hutumia fursa hiyo na  kuwaozesha watoto mapema, kabla ya kumaliza skuli.

“Kitendo cha kuwaozesha watoto mapema ni kuwadhalilisha, kwani wanakosa haki zao za msingi za kupata elimu,”anaeleza.



Mwanaharakati Sifuni Ali Haji anasema kuwa faini hiyo ya mzazi anayotozwa ni ndogo mno, na ndio maana ndoa kwa wanafunzi, zimekuwa zikiongezeka.

Anasema faini ya shilingi 1,500 ni ndogo hivyo kunahitajika kukaliwa kitako na kuangaliwa upya kwa kina ili kuweza kuifanyiwa marekebisho kulingana na wakati uliopo.

“Sheria hii ipitiwe na ifanyiwe marekebisho katika vifungu vyote, ambavyo haviendani na wakati tulionao,’’ anashauri.

WAALIMU

Msaidizi mwalimu Mkuu skuli ya sekondari Uweleni Khamis Mohamed Ussi, anasema kutokana na adhabu kuwa ndogo, imepelekea wazazi na walezi kukosa woga na kuwaozesha watoto wao wakiwa bado wako masomoni.

Anasema ingekuwa sheria ni kali na madhubuti yenye kwenda na wakati, na hatuwa zikachukuliwa dhidi ya wazazi wanaowaozesha watoto wao, wimbi hilo lingepungua.

 “Hivi sasa wapo baadhi ya wazazi hufanya ujanja wa kufanya harusi sehemu nyengine kwa kuficha wasijulikane kwa lengo la kujificha,’’anasema.

Mwalimu mkuu skuli ya Mahuduthi Siti Sleyyum anasema marekebisho ya sheria hiyo yanahitajika kwani wazazi wanaichukulia nafasi hiyo na wanajiamini kwa kuwa haina ukali wowote.

“Sheria hiyo inamkanganyiko, kwani haikutamka wazi hasa pale ilipoeleza kuwa, haimkatazi mwanafunzi kuowa au kuolewa kabla ya kukamilisha elimu ya lazima,’’anaeleza.

Anasema ni vyema sheria hiyo ingetamka wazi na kwenda moja kwa moja tu kuwa mwanafunzi asiolewe badala ya ilivyozunguka zunguka.

Mwalimu Siti Mohamed wa skuli ya Mtambile anasema wazazi ni lazima wapewe elimu, juu ya athari ya ndoa za mapema, ili kuhakikisha watoto wao wanapata elimu ambayo ndio itakayoweza kuwasaidia katika maisha yao.

Anasema mbali na kuwepo kwa mapungufu hayo ya sheria lakini wanafunzi na wao wanapaswa kujielewa, ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea.

Mratibu wa Chama chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar Ofisi ya Pemba Fat-hiya Mussa Said, anasema kutokana na faini kuwa ndogo, ndio maana wazazi huwakatisha watoto wao.

Aliitaka serikali kupitia wizara ya elimu kuifanyia marekebisho ya haraka sheria hiyo ili adhabu kali iweze kutolewa kwa wazazi watakaowaozesha watoto wao ambao bado hawajamaliza masomo.

KIONGOZI WA DINI

Mmoja kati ya viongozi wa dini ya kiislamu Wilaya ya Chake chake ambae hakutaka jina lake litajwe anasema  inaweza kuwa ni  vigumu kwa wananchi kuona kuwa ni kosa  kumuozesha mtoto ambae bado hajamaliza masomo kwa vile haiendani na  imani  zao.

“Ingawa dini ya kiislamu haijamkataza mtu kutafuta elimu, lakini wazanzibari ambao wengi wao wanafuata imani ya dini hiyo, wanaamini mtoto ni yule ambae hajabaleghe na sio vyenginevyo,’’alisema.

WIZARA YA ELIMU

Ofisa Mdhamini wizara ya Elimu na mafunzo ya Amali Pemba Mohamed Nassor Salim, anasema sheria hiyo imepitwa na wakati, na bado ina vifungu vinahitaji marekebisho.



Akizungumzia kuhusiana na kesi za ndoa za utotoni anasema zinafanywa kwa usiri mkubwa bila ya kuripotiwa na huzigunduwa pale mwanafunzi wakiwa wameshaolewa.

Hata hivyo anasema licha ya changamoto hiyo, lakini wizara kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wamekuwa wakitoa elimu kwa jamii madhara ya ndoa  za utotoni.

Mwanasheria wa Serikali Ali Amour Makame anasema wakati ilipotungwa sheria hiyo kiwango cha adhabu kilichowekwa kilikua kikubwa, ingawa kwa sasa ni ndogo.

Lengo la sheria hiyo ni kumlinda mtoto kumaliza elimu ya msingi na sio vyenginevyo, ingawa wapo baadhi ya wazazi hufuata sheria ya dini ya mtoto anapokuwa baleghe tu na kumuozesha.

WAZAZI/WAELZI

Mmoja kati ya wazazi Amina Khamis wa Mkoani, ameitaka jamii kushirikiana kwa pamoja, katika kutokomeza ndoa hizo, ili watoto waweze kupata elimu  ambayo itaweza kuwasaidia katika  maisha yao.

Ali Sharif wa Chake chake, anasema ni vyema wazazi wapewe elimu juu ya athari ya ndoa za utotoni, ili kuhakikisha watoto wao wanapata elimu ambayo ndio itakayoweza kuwasaidia hapo baadae.

Anasema mbali na kuwepo kwa mapungufu hayo ya sheria lakini ni jukumu la wanafunzi kujielewa ili kuweza kufikia malengo waliyojiwekea.

WANAFUNZI

 Mwanafunzi Aisha Ali wa skuli ya sekondari Uweleni, anasema baadhi ya wazazi na walezi huwalazimisha kufunga ndoa watoto, ambao bado wanahitaji kupata elimu hasa ya lazima.

Anasema wazazi wamekuwa wakifanya hivyo, bila ya kujali athari anazoweza kuzipata mtoto anayeolewa akiwa mwanafunzi.

 Wapo badhi ya wazazi wamekuwa wakiwaozesha watoto kwa kisingizio cha tamaa za kupata kipato kupitia mahari wanayopewa.



Mwanafunzi Abdul Juma wa skuli ya Kengeja, anasema wamekuwa wakifanya hivyo bila YA kujali athari anazoweza kuzipata mtoto anayeolewa akiwa mwanafunzi.

    mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch