Skip to main content

RC MATTAR: UWAPE TUNGENI MASHAIRI KUPINGA UDHALILISHAJI, DAWA ZA KULEVYA

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MKUU wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massuod, amewataka washairi na watunzi wa Umoja wa Washairi wa Pemba ‘UWAPE’ kutunga mashairi, yenye kuihamasisha jamii, kupiga vita vitendo vya udhalilishaji, dawa za kulevya na majanga mengine.

Alisema, jamii imezongwa na majanga na kukuawa kila siku, hivyo washairi wanayonafasi ya kukemea, kushauri, kuekeza njia ya kupunguza matendo hayo, na chanzo chake kupitia mashairi yao.



Mkuu huyo Mkoa, ameyasema hayo Machi 19, 2023 ukumbi wa Umoja ni nguvu Mkoani, kwenye hutuba yake iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Chake chake, Rashid Abdalla Ali.

Mkuu huyo wa Mkoa alisema, njia ya mashairi ni nzuri na nyepesi katika kufikisha ujumbe husika kwa jamii, hivyo ni wakati wa washairi wa ‘UWAPE’ kuliono hilo haraka..

‘’Kwa sasa, kila mmoja ni shahidi kuwa, jamii yetu inakumbana na majanga, mbali mbali hata migogoro ya ardhi, dawa za kulevya, udhalilishaji na mivutano ya kifamilia, hivyo washairi waangalie kuisadia jamii,’’alieleza.






Katika eneo jingine, Mkuu huyo wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, alisema wazo la kuanzisha UWAPE, ni mzuri, maana itasaidia hata vijana kujiajiri.

Aidha aliwataka watunzi wa mashairi kutoka umoja huo, kutumia mashairi yao, katika kuikuza na kuiendeleza lugha ya kiswahili sanifu.

Alisema, duniani kote wanaamini kuwa, ukitaka lugha sanifu ya kiswahili na lahaja zake, ni Zanzibar hivyo kupitia UWAPE, iwe jukwaa muhimu na adhimu katika eneo hilo.

Hata hivyo aliwapongeza viongozi wa UWAPE, kwa kubuni umoja huo, ambao kwa njia moja ama nyingine, inazidi kuitangaaza kugha ya kiswahili nje na ndani.

Aidha aliipongeza bodi ya redio Jamii Mkoani, kwa kusimamia hadi kufanikisha kuanzishwa kwa umoja huo, ambao alitaka kuona unasambaa hadi mkoa wa kaskazini Pemba.

‘’UWAPE usambaae hadi wilaya za Wete na Micheweni, hii itasaidia kwanza kutangaazika vizuri, lakini itaibua vipaji vyengine tofauti,’’alieleza.

Katibu Tawala wilaya ya Mkoa Miza Hassan Faki, aliipongeza redio Jamii Mkoani, kwa kuibuka washindi wa taifa, kwa matumizi bora ya lugha ya kiswani kwa mwaka huu.


Alieleza kuwa, ushindi walioupata wakati wa kongamano la Idhaa za za lugha ya kiswahi, Machi 18, mwaka huu ni ishara njema kwa wafanyakazi wa redio hiyo.

Akizungumzia wanachama wa UWAPE, amewakumbusha kuwa  kabla ya kuchapisha mashairi yao, kujenga utamaduni wa kuhaririana, ili kuepusha matumizi mabaya ya lugha husika.

Hata hivyo, ameukumbusha uongozi wa ‘UWAPE’ kutunga mashairi yanayojenga umoja na mshikamano miongoni mwa wananchi nchini.     

Akisoma risala, Mwenyekiti wa UWAPE Khalid Said Mohamed, alisema, moja ya changamoto inayowakabili kwa sasa ni ukosefu wa ofisi na studio ya kurikodia kazi zao.





Alieleza kuwa, jengine ni kukosa nyenzo za fedha za kuisambaaza ‘UWAPE’ mkoa wa kaskazini Pemba pamoja na jamii kukosa mwamko wa kuyapokea mashairi yao.

Hata hivyo, alisema wazo la kuanzishwa kwa ‘UWAPE’ ni kuwepo kwa kipindi cha tungo na mashairi, kwenye redio Jamii Mkoani, ambapo watunzi walikuwa hawajuani.

‘’Kisha kwa mara ya kwanza, tulikutana watunzi na washairi wote Septemba 24, 2022 redio Jamii Mkoani, na kuibua wazo la kuanzisha umoja, uitwao UWAPE,’alieleza.

Mapema Mkuu huyo wa mkoa wa kusini Pemba, Mattar Zahor Massoud, alikizindua kitabu cha mashairi, CD na chanali ya youtube pamoja na kumkabidhi zawadi mtunzi bora wa mashairi kutoka UWAPE.

UWAPE ambayo imepata usajili mwaka huu, inao wanachama 25, kati ya hao wanawake 10 na wanaume 15, ambapo lengo lao kuu ni kutoa elimu kwa njia ya mashairi, kipato, kukikuza kiswahili pamoja na jamii kupenda mashairi.  

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch