Skip to main content

SAADA KIJANA ALIYEHAMASIKA KUUSAKA UONGOZI, ASEMA CHANGAMOTO, BEZO KWA WENZAKE ZINAMPA KASI ZAIDI

 

          



NA MARYAM SALUM, PEMBA@@@@

“AMA kweli subira ni kitu cha kheir, mwenye kusubiri hakosi”

Kejeli, maneno mabaya, machafu, matusi ya nguoni yote sikujali… nahakikisha nafikia lengo langu”,.

Hayo maneno ya kijana mashuhuri anaesaka uongozi kila pembe aliejulikana kwa jila la Saada Saleh mkaazi wa Chwale Wilaya ya Wete Pemba.

Anasimulia kuwa, maneno hayo na kejeli za watu hayakuwa yakimridhisha, ingawa kwa vile alikuwa na msimamo wa kutafuta basi hawakuweza kupata nafasi ya kumvunja moyo.

 “Lakini niliwashindwa na wamebaki vinywa wazi, yasiyoniridhi nilipitia kwa muda mrefu bila kugombana wala kulipiza kisasi nao hadi nilipofikia”, anasema.

Majirani, marafiki wa karibu na hata kwa baadhi ya ndugu wa familia walikuwa wanasema mengi, lengo lao ni kuona hafikii kwenye malengo yake ya kuwa kiongozi.

 Saada aliamini misemo mbali mbali ya kiswahili kwamba… subra ni ngao, na pia nia njema hairogwi na ndipo alipokaza buti kuona anapamba na adui zake kuhakikisha anafikia malengo.

Alijitolea kwenye masuala mbali mbali ya kimaendeleo, ikiwemo vikundi vya maendeleo vya kuweka na kukopa, jumuiya binafsi, hadi jumuia za Chama cha Mapinduzi.

Hapo ndipo sasa alipoanza mchakato wa kugombea nafasi za uongozi kama kijana, ingawa haikua rahisi kwa mara ya kwanza kufanikiwa.

Saada alipambana na hali hiyo bila kukata tamaa, mwisho wa siku kuona kwamba anayafikia malengo aliyoyakusudia ingawa sio rahisi kutokana changamoto alizokua akizipata.

Miongoni mwa changamoto zenyewe ni pamoja na kukosa ushirikiano kwa baadhi ya watu wake wa karibu, hasa kwenye familia, marafiki kumdharau.

Aliitwa majina mabaya, hasa pale anapotoka kwenda kwenye shughuli zake na kusema kuwa, hana anachokifuata isipokua uhuni, ingawa yapo mengi yamesemwa, lakini msimamo wake ndio njia pekee iliomsaidia.

Anaeleza kuwa changamoto zote hizo alizokumbana nazo kama kijana wa kike, zimeweza kumfungulia milango na kufika pale anapopataka.

Saada ni msichana mdogo lakini amepitia changamoto mbali mbali akiwa kwenye shughuli zake za maendeleo, ingawa zilimfanya awe jasiri zaidi, mahiri, ukakamavu na kujiamini.

“Nilipitia changamoto nyingi, lakini kutokana na subra niliyonayo sikutetereka, kwani nilihakikisha nafikia malengo yangu, ili niondokane na utegemezi kwa wazazi wangu, kama walivyo vijana wengine”, anasema.

   HISTORIA YAKE

Saada alizaliwa Oktoba 24 mwaka 1997 katika hospitali ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba na alisoma elimu yake ya msingi na sekondari katika skuli ya Chwale Madenjani kuanzia mwaka 2003 hadi kumaliza kidato cha nne mwaka 2013.

Mwaka 2017 alijiunga na chuo cha Zanzibar College of Business Education katika fani ya manunuzi na magavi kwa ngazi ya cheti na aliendelea na Diploma mwaka 2018 na kumaliza mwaka 2019.




HARAKATI ZAKE ZA KUGOMBEA

Mwaka 2016 aligombea nafasi ya Makamo Mwenyekiti wa Baraza la Vijana Wete ambapo alishinda kwa kupata kura 31 dhidi mwenzake aliepata kura zisizozidi tano (5) kati ya kura 37 zilizopigwa.

Mwaka 2018 pia Saada aligombea nafasi ya Uenyekiti wa Jumuia ya Vijana wa kike Pemba, Female Youth Organiasation (PFYO) inayosimamiwa na Shirika la Action Aid na kuibuka mshindi.

Kwa vile subira ni ngao, kama kijana asiekata tamaa ya maendeleo, ilipofika mwaka 2020, alichukua fomu ya kugombea nafasi ya ubunge katika Jimbo lake la Kojani, ingawa alikosa.

“Sijakata tamaa, nitaendelea kupambana na itakapofika mwaka 2025 nitaingia tena jimboni kuusaka uongozi”, anaeleza Saada.

 Anafahamisha kuwa, kutokana na vijana wenzake wakike na jamii iliyomzunguka katika jimbo lake kukosa uelewa kuhusu umuhimu wa wanawake kwenye uongozi, basi hawakumpigia kura hata moja.

“Waliona kama wananikomoa lakini hawajui kwamba mwanamke ndie mwenye huruma na anaeweza kuwatetea zaidi kuliko wanaume lakini hiyo ni miongoni mwa changamoto, hivyo nitaigeuza kuwa fursa kwangu”, anaeleza.

 Anafahamisha kuwa, kukosa ubunge kwake haikua mwisho wa kugombea nafasi nyengine, bali ilimuongezea kasi, ari na nguvu mpya kwani baada ya hapo aligombea nafasi ya Uenyekiti wa Baraza la Vijana Wilaya ya Wete na kupata kura 17 kwenye kura 46.

Hivyo hakukata tamaa ambapo mwaka 2022 pia aligombea nafasi nyengine ya Uenyekiti wa UVCCM Wilaya na nikafanikiwa kuibuka mshindi.

“Mwaka 2022 niligombea Uwenyekiti wa UVCCM Wilaya ya Wete hapo sasa ndipo nilipoamini kwamba ‘subira huleta k heri’ kwa kujinyakulia ushindi kwa kupata kura 68 kwenye kura 113 huku mgombea wa pili akipata kura 35”, anaeleza.

Ndani ya Jumuia ya Vijana wa kike ya ‘PFYO’ iliyopo Wete anafanya Miradi mbali mbali ya kimaendeleo kama kujiinua kiuchumi yeye na vijana wenzake.

Ambapo aliufanya kwa kushirikiana na Shirika la Action Aid mwaka 2017 hadi 2020 African Charter on Democracy Election and Good Governance.

Saada hakukata tamaa licha ya kuwa ni  mtoto wa kike aliepambana zaidi kuhakikisha maelengo yake anayafikia, hakujali changamoto za hapa na pale.

“Hapa nilipofikia bado sijafika tamati kwenye uongozi, huu ni mwanzo tu nitahakikisha napambana zaidi kwenye suala la maendeleo kwa kufikia mbali zaidi, mimi na vijana wenzangu,”anasema.

CHANGAMOTO

Miongoni mwa changamoto ni kupewa majina mabaya, kufikiriwa  maovu kwa lengo la kumkatishwa tamaa asifikie malengo.

“Wengine walimfikiria kwamba atakuja kuolewa na kuondoka, wengine wakasema siwezi kuongoza kutokana na jinsia yangu kuwa ni mwanamke,’’anakumbuka.

Changamoto nyinge ambayo anasema iko katika mfumo dume, ni wanaume kumzonga zonga, kila eneo analoweka nia ya kugombea, ingawa kwa vile alishajua ilikuwa kazi rahisi.

MAFANIKIO

Kwake anaona faida kubwa hadi sasa ni kupata marafiki wengi zaidi kwenye maeneo tofauti Zanzibar, Dares-Salaam na Mikoa mengine jirani, pia kujijengea uewelewa zaidi katika uongozi.

Kupamba na changamoto na kujua mbinu za kisasa za kuzitatua, ambazo nyingi anasema alizitumia kama fursa.

‘’Mtu akikwamba uongozi ni uhuni, kwangu najiongeza uwa nisiwe muhuni, nikiambia viongozi waongo, najipanga ili kuwabadilisha mtazamo, na nimefanikiwa kwa kiasi,’’anasema.

Anajigamba kuwa amekuwa mwenyeji ndani ya Chama chake cha Mapinduzi CCM pamoja na serikali, kwa kule kujuana na viongozi mbali mbali.

Sambamba na hayo Saada anaeleza kuwa, nafasi aliyonayo sasa si kwa nguvu zake pekee, bali ni jitihada  zake na nguvu kubwa zaidi kutoka kwa vijana wenzake na viongozi wengine chama na Serikali kwa ujumla.

Akitoa nasaha kwa vijana wenzake hasa wanawake waliopata kuchaguliwa kwenye uongozi, anasema wasijione wamepata kwa ujanja wao ikawa ndio chanzo cha kufanya mambo kwa maslahi yake mtu binafsi.

“Tusisahau tulipokua tunaomba kura, tulikua na maneno ya busara, yenye hekma, wanyenyekevu kwa wenzetu, hivyo utaratibu huo uwe endelevu hadi baada ya uongozi”, anafafanua.

Aliwataka wanawake wengine ambao hawajaingia kwenye uongozi kwa kuhofia, nafasi zipo nyingi za uongozi kwenye chama, tawi na katika jamii.

MAMA MZAZI WA SAADA

Mpaji Shaame Massoud ambae ni mama mzazi wa Saada anaeleza kuwa, Saada ni mtoto wake wa pili kati ya watoto wake tisa aliokirimiwa na Mungu.

“Saada ni mtoto wangu wa pili na anajipambania sana kuhakikisha analeta mafanikio katika jamii yake, hivyo hakujali changamoto alizokumbana nazo,” alisema.

Mama huyo alitoa nasaha zake kwa kijana wake kuwa, aendelee kupiga moyo konde na afanye kazi zake kwa weledi, kujiamini ili kuhakikisha jamii inapata maendeleo.

Ali Juma Ali, Suleiman Massoud Shaame na Hadia Omar Haji wakaazi wa Chwale Wilaya ya Wete walisema kuwa, Saada ni msichana wanaemfahamu tangu utotoni mwake kwamba, ni mcheshi, mchangamfu kwa wenzake na anayependa kutafuta.

“Tunamjua kuwa, ni mkarimu, mtafutaji, mpambanaji na pia hapendi kukata tamaa mapema katika suala la kutafuta maendeleo na hata familia yake ni nzuri”, alieleza.

Hivyo walimtaka kuongoza nafasi yake ipasavyo, ili kukiletea maendeleo chama husika na kujali nguvu za vijana wenzake ambao walimpatia ridhaa hiyo kwa maendeleo na sio majungu.

                                        MWISHO.

 

 

 

 

 

                                                      

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch