Skip to main content

WAZAZI, WALEZI CHAKE CHAKE WAASWA KUSAIDIANA MALEZI, MAKUZI YA AWALI YA MTOTO

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

JAMII ya wilaya ya Chake chake Pemba, imeshauriwa kuendelea kusaidiana, katika malezi na makuzi ya awali ya watoto, ili wakuze ubongo wao, kwa aina ya mazingira wanayoishi.

Hayo yameelezwa leo Januari 23, mwaka 2026 na Mwenyekiti wa Kamati ya Kupambana na Udhalilishaji wilaya ya Chake chake, ambae pia ni Katib Tawala wilaya hiyo, Suleiman Hamad Suleiman, kwenye siku ya pili ya mafunzo ya siku tano, ya ulinzi na hifadhi ya mtoto, yanayofanyika ukumbi wa zamani wa TASAF, kwa ufadhili wa UNICEF.



Alisema, jamii bado haijaona umuhimu wa kushirikiana baina yao, katika malezi na makuzi ya awali ya mtoto, jambo ambalo kwa baadhi ya wakati, huwapa msongo wa mawazo watoto hao.

Alieleza kuwa, jamii isiishie tu kwenye kuwaangalia wasikumbwe na majanga, bali sasa washirikiane katika malezi, makuzi ya awali katika maisha yao.

‘’Niiombe jamii ya wilaya ya Chake chake, wahakikishe wanasaidiana miongoni mwao, katika malezi, makuzi ya awali ya mtoto, ili wakuze ubongo na kuyatawala mazingira yao,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Mwenyekiti huyo wa kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chake chake Suleiman Hamad Suleiman, amwewataka wajumbe wa kamati hiyo, kushirikiana miongoni mwao wanapofanya kazi zao, za kutetea haki na fursa za watoto.

Akiwasilisha mada, ya mahitaji katika maendeleo na makuzi ya awali ya mtoto, Katib wa kamati hiyo Rashid Said Nassor, alisema jamii haielewei kua, mtoto anapokuwa tumboni mwa mama yake, anasikia kila kitu.




Aidha alieleza kuwa, wazazi wasiwajibu uongo watoto wao wanapowauliza maswali, kwani huwaharibu ubongo wao na kukosa uaminifu kwao hapo baadae.

Alifafanua kuwa, kuanzia mwaka mmoja mtoto, akiwa anapenda kuchora, kuuliza, kutembea kwa kasi ni nafasi ya wazazi, kuwaachia kufanya hivyo, ili wazidi kujifunza.

Aliongeza kuwa, kuanzia miaka 13 hadi 18 watoto huchukua nafasi ya kukuza maadili, kufikiria uhuru wa kujitegemea, kuanzisha majukumu mapya katika jamii, kuwa na hisia ya utambulisho.

‘’Jingine katika miaka hiyo ni kuanza kujiamiani, kujifananisha na wakubwa zaidi, jambo ambalo familia zinapaswa, kuwa makini katika malezi yao yenye maadili,’’alifafanua.

Mjumbe wa kamati hiyo ambae pia ni Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali wilaya cha Chake chake, Burhan Khamis Juma, alipinga suala la baadhi ya wazazi, kuwadanganya waototo wao, ikiwa ni njia ya kuwatuliza.




Nae mjumbe wa kamati hiyo Nassra Ali Sagafu, alisema njia nyingine ya wazazi wa kiume, kuwa karibu na watoto wao ni kuwasindikiza wenza wao kliniki.

‘’Mtoto akimuona baba yake eneo la kliniki au hospitali, inamsadia sana kujenga ukaribu wa kudumu katika maisha yake,’’alifafanua.



Kwa upande wake mjumbe kutoka ofisi ya Mufti Pemba, Abdull-taif Abdalla Salim, alisisitiza kwa wazazi kuacha utamaduni wa kuwasemesha uongo watoto wao, ili kuwanyamazisha, bali wawaeleze ukweli.





Katika mafunzo hayo ya siku tano, mada kadhaa zitawasilishwa ikiwemo hifadhi ya mtoto, mikataba ya kitaifa na kikanda ya haki za mtoto pamoja na mahitaji katika maendeleo ya awali na makuzi ya mtoto.                                  Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...