Skip to main content

USHIRIKI WA WANAWAKE WENYE ULEMAVU KATIKA UONGOZI WA KISIASA ZANZIBAR, BADO NI HESABU ZA MADOLE

 


NA ZUHURA JABIRI, ZANZIBAR@@@@@

KATIBA ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 21(2), inatamka wazi kuwa kila raia ana haki ya kushiriki katika masuala ya uongozi na shughuli za kijamii bila kuingiliwa.

 Aidha, Sheria ya Watu Wenye Ulemavu ya Zanzibar nambari 8 ya mwaka 2022 inalinda haki za watu wenye ulemavu, kushiriki kikamilifu katika maisha ya jamii, ikiwemo siasa.

Tanzania pia imeridhia Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Watu Wenye Ulemavu (CRPD) wa mwaka 2006, hatua inayothibitisha dhamira ya kitaifa ya kuhakikisha wanawake wenye ulemavu wanapata haki sawa za kisiasa na kiraia.

Hata hivyo, pamoja na misingi hii imara ya kisheria, uhalisia unaoonekana katika jamii ya Zanzibar unaonesha picha tofauti kabisa.

Maana sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2022, Zanzibar ina jumla ya watu 215,434 wenye ulemavu, sawa na asilimia 11.4 ya idadi yote ya watu.

Ambapo kati yao, watu 6,843 wako katika umri wa miaka 15 hadi 65, kundi linalostahiki kushiriki kikamilifu katika michakato ya kisiasa, ikiwemo kupiga kura na kugombea nafasi za uongozi.

Licha ya idadi hii kuwa kubwa, uwakilishi wa wanawake wenye ulemavu katika vyombo vya uamuzi bado ni mdogo sana.

Kwani kwa sasa, katika Baraza la Wawakilishi lenye jumla ya wajumbe 76, ni wanawake watatu tu wenye ulemavu, wanaoshika nafasi.

Akiwemo Mwantatu Mbaraka Khamis na Aza Januar Joseph wanashika viti maalum kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku Anna Athanas Paul akiteuliwa na Rais wa Zanzibar, kutoka orodha ya watu kumi waliopendekezwa. Tofauti hii kubwa, kati ya idadi ya wanawake wenye ulemavu na nafasi wanazoshika inaonesha wazi pengo kati ya haki zilizoandikwa kisheria na utekelezaji wake halisi.

Changamoto zinazowakabili wanawake wenye ulemavu katika kushiriki siasa ni nyingi na zinagusa nyanja mbalimbali za maisha yao.

Moja wapo anasema mwanaharakati za watu wenye ulemavu Pemba Hidaya Mjaka Aki, kuwam ni miundombinu katika vituo vya kupigia kura, kwani mara nyingi haizingatii mahitaji yao.

Nyingine anataja kuwa ni ukosefu wa njia panda (ramps), sakafu zisizo rafiki, na umbali mrefu wa kutembea hufanya baadhi ya wapiga kura wenye ulemavu, kushindwa kufika vituoni.

 Anafafanua kuwa, jingine ni changamoto za mawasiliano, hasa kuhusu kupata taarifa rasmi zikiwemo wakati wa kuchukua fomu, urejeshaji na masharti makuu.

Omar Haji Mohamed asieona, anasema changamoto nyingine ni ukosefu wa vifaa vya kura kwa maandishi ya nukta nundu (braille), vifaa vya sauti, na wakalimani wa lugha ya alama.



Zaidi ya changamoto za kimazingira, zipo pia changamoto za kijamii na kiutamaduni, ikiwemo kutoonekana kama vile wanamchango kwa jamii yao.

Mitazamo hasi kuhusu uwezo wa wanawake wenye ulemavu bado imeshamiri katika jamii nyingi za Zanzibar.

Maana wingi huamini kimakosa kuwa ulemavu ni sawa na kutoweza, hali inayowakatisha tamaa wanawake wengi wenye ulemavu kuwania nafasi za uongozi.

Vyama vya siasa navyo mara nyingi huwapuuza wanawake hawa katika michakato ya uteuzi wa wagombea, wakiwanyima fursa za kushiriki kikamilifu.

Aneleza kuwa, aidha, upungufu wa rasilimali kama fedha za kampeni, mafunzo ya uongozi, na programu za ulezi (mentorship) huongeza ugumu wa safari yao ya kisiasa.

 

Pamoja na changamoto hizi, zipo dalili za matumaini, maana mwezi Disemba 2024, Zanzibar ilizindua sera mpya ya jinsia inayolenga kuhakikisha uwakilishi wa wanawake kwa asilimia 40 katika miundo ya vyama vya siasa.



Huku ikilenga usawa wa asilimia 50 kwa 50 kwa muda mrefu, hatua hii ni muhimu kwani inafungua milango kwa wanawake wengi zaidi, wakiwemo wenye ulemavu.

Aidha, miradi kama Strengthen Women-In-Leadership (SWIL) unoendeshwa na TAMWA Zanzibar, imekuwa chachu ya mabadiliko kwa kuwapatia wanawake wenye ulemavu, mafunzo ya uongozi, kujiamini, na ushauri wa kitaaluma.

Mifano kutoka Tanzania Bara pia inaweza kutumika kama rejea kwa Zanzibar, maana Shirika la UN- Women kama Women’s Leadership, Empowerment and Rights (WLER) imeonesha kuwa pale wanawake wenye ulemavu wanapopewa mafunzo, fursa za kushiriki katika utungaji wa sera, na msaada wa kifedha.

Kwani imefahamika kuwa, wanaweza kugombea na kushika nyadhifa za uongozi kwa mafanikio.

Maana Programu hizi zinaweza kunakiliwa na kurekebishwa kulingana na mazingira ya Zanzibar, ili kuongeza ushiriki wa wanawake wenye ulemavu katika uongozi.



 

Ili kufanikisha ushiriki wa maana wa wanawake wenye ulemavu katika siasa, hatua za makusudi zinahitajika, serikali ya Zanzibar inapaswa kuhakikisha michakato yote ya uchaguzi inakuwa rafiki kwa watu wenye ulemavu kwa kurekebisha vituo vya kupigia kura na vifaa vyingine muhimu.

 Hata kutoa vifaa vya kura vinavyofikika kwa wote, na kuweka wakalimani wa lugha ya alama.

Kwa upande wa vyama vya siasa Haji Mohamed Issa kutoka ZANAB Pemba, anasema vinapaswa kutekeleza sera za ubaguzi chanya (affirmative action), kwa kutenga asilimia maalum ya nafasi za uongozi au uteuzi kwa wanawake wenye ulemavu.

Anasema hilo pia ni sambamba na kuwapatia mafunzo na ulezi wa kisiasa wanawake hao.

 


Mashirika ya kiraia kama JUWAUZA (Jumuiya ya Wanawake Wenye Ulemavu Zanzibar) na ZANAB yana nafasi muhimu ya kuimarisha utetezi kwa kushirikiana na vyama vya siasa.

Vilevile, kampeni za uhamasishaji wa umma ni muhimu ili kubadili mitazamo hasi, kuonesha mifano ya wanawake wenye ulemavu waliofanikiwa, na kusisitiza kuwa ulemavu si kikwazo cha uwezo.

Mipango shirikishi na bajeti zinazozingatia jinsia zitahakikisha rasilimali zinagawanywa kwa usawa na kuunga mkono wanawake wenye ulemavu katika nafasi za uongozi.

Kwa ujumla, wanawake wenye ulemavu ni sehemu muhimu na yenye uwezo mkubwa katika jamii ya Zanzibar, ushiriki wao kamili katika siasa si suala la hisani bali ni haki ya kikatiba.

Kwani zaidi ya hapo, ni mkakati wa kuimarisha demokrasia na kuhakikisha sera na maamuzi yanawakilisha mahitaji ya wananchi wote.



Kupitia miundombinu rafiki, programu za uongozi, sera za ubaguzi chanya, utetezi madhubuti, na uhamasishaji wa jamii, Zanzibar inaweza kujenga mazingira ya kisiasa yanayompa kila raia.

Kuwezesha wanawake wenye ulemavu ni hatua muhimu kuelekea Zanzibar jumuishi, yenye usawa na uwakilishi wa kweli.

              Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...