Skip to main content

WAJUMBE KAMATI YA KUPAMBANA NA UDHALILISHAJI CHAKE CHAKE YAPIGWA MSASA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAJUMBE wa Kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chake chake, wametakiwa kuongeza nguvu katika ulinzi na hifadhi ya mtoto, ili waendelee kuwa salama katika maisha yao.

Hayo yameelezwa na leo Januari 22, mwaka 2026 katika ukumbi wa zamani wa TASAF Chake chake, na Afisa Elimu na Mafunzo ya Amali wilayani humo, Burhan Khamis Juma, wakati akiyafungua mafunzo ya siku tano ya ulinzi na hifadhi ya mtoto, yaliofadhiliwa na UNICEF.

Alisema, nguvu za pamoja ni hatua moja kubwa, katika kuhakikisha watoto wa wilaya ya Chake chake, wanakuwa salama katika maisha yao ya leo na baadae.



Alieleza kuwa, kuwepo kwa kamati hiyo, iwe ni chachu kwa ulinzi na hifadhi ya watoto, na kuendelea kushirikiana kwa karibu miongoni mwao, ili kuhakikisha watoto hawaingii kwenye majanga.

‘’Niwaombe sana wajumbe wa kamati hii, kuhakikisha mnakuwa na ushirikiano na nguvu za pamoja, katika kuhakikisha watoto wanakuwa salama,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Afisa huyo Elimu na Mafunzo ya Amali wilaya ya Chake chake Burhan Khamis Juma, alisema jamii, itaendelea kuwa na wajibu wa kwanza, katika hifadhi na ulinzi wa mtoto.

Alifahamisha kuwa, familia na jamii kwa ujumla, ndio wenye jukumu la mwanzo na kubwa, katika kuhakikisha watoto wanakuwa salama na kukingwa na majanga.

Katika hatua nyingine, alivikumbusha vyombo vya ulinzi na usalama vinavyofuatilia haki za watoto, kutenda haki wanapofanyakazi zao hizo.



‘’Nivikumbushe vyombo vya ulinzi na usalama ambavyo vinasimamia haki za mtoto, kuhakikisha wanatenda haki kwa watoto wanaodhalilishwa, wapate haki zao mbele ya vyombo vya ulinzi na usalama,’’alifafanua.

Akiwasilisha mada ya hifadhi na ulinzi ya mtoto Katibu wa Kamati ya kupambana na udhalilishaji wilaya ya Chake chake Rashid Said Nassor, alisema wazazi kukataa kuwapa huduma watoto wao ni aina ya udhalilishaji.

Alisema, ijapokuwa udhalilishaji, imeshazoekeleka katika jamii, kuwa ni ubakaji, ulawiti, ndoa za mapema na mimba za umri mdogo, lakini hata suala la kumkosesha chakula ni ukatili.



Alieleza kuwa, kati ya watoto wa kike 20, mmoja amesharipotiwa kufanyiwa udhalilishaji katika maisha yao, ambapo kwa wanaume 10, mmoja alishapitia udhalilishaji katika maisha yao.

Aliongeza kuwa, asilimia 71 ya watoto wa kiume na asilimia 62 ya watoto wa kike waliripoti kupambana na udhalilishaji wa kimwili kabla ya kufikia miaka 18.



Aidha alifafanua kuwa, utafiti unaonesha kuwa, zaidi wanawake saba kati ya 10 na wanaume sita kati ya 10 wenye umri kati ya miaka 12 hadi 24 wameshakumbwa na udhalilishaji.

Katika hatua nyingine aliongeza kuwa, asilimia 12.3 wanawake na wanaume 20.3 waliripotiwa kuitwa majina mabaya na jamii, umegundua utafiti huo wa mwaka 2009 uliofanywa Zanzibar.   

Mjumbe wa kamati hiyo Kassim Ali Omar, alisema bado nguvu za pamoja na zinahitajika, ili kuhakikisha majanga yanayowagusa watoto yanapungua.



Alisema, zipo sheria mpya na kali, kanuni na miongozo kadhaa, ambayo yanalenga kupunguza majanga hayo, ambapo kama ushirikiano haukua nambari moja, wataendelea kudhalilishwa.

Nae Suleiman Said Salim aliomba serikali kwa kushirikiana na wadau wake, kufanya utafiti wa kina kujua chanzo hasa cha kuendelea kuwepo kwa matendo hayo wanayowanyima raha watoto.

Nae mjumbe Robart Migua Ndalami, aliviomba vyombo vya habari, kupunguza madhara wakati wanaporipoti habari zao za udhalilishaji.



Akiwasilisha mada ya hifadhi ya mtoto katika sheria, za kimataifa, kikanda na kitaifa Afisa Hifadhi na mtoto kutoka Unguja, Fatma Maulid, alisema bado juhudi zinahitajika.

Alieleza kuwa, ni vyema kila mmoja, kujenga maslahi bora yam toto, bila ua ubaguzi wowote, kama ilivyolelekeza mikataba na sheria mbali mbali.




Alifahamisha kuwa, sheria zimekuja kuwapa usawa watoto wote, wakiwemo wenye ulemavu, ingawa bado kwenye jamii, hali iko kinyume na mitazamo ya sheria.

Katika mafunzo hayo ya siku tano, mada kadhaa zitawasilishwa ikiwemo hifadhi ya mtoto, mikataba ya kitaifa na kikanda ya haki za mtoto

               Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...