Skip to main content

MIAKA 62 YA MAPINDUZI YALIYOIJENGA PEMBA KIELIMU, YAMEONDOA GIZA LA ELIMU HADI KUFIKIA MNARA WA MAARIFA

 



HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@

HAKUNA tukio lililobadilisha mwelekeo wa maisha ya Mzanzibari kama Mapinduzi ya 12 Januari 1964.

 

Mapinduzi haya yaliibadili kabisa falsafa ya maendeleo ya jamii kwa kutambua elimu kama haki ya kila mwananchi. 

Miaka 62 ya Mapinduzi matukufu Zanzibar nzima  Unguja na Pemba  inasimama kifua mbele kama ushahidi hai wa Mapinduzi yaliyoamua kuwekeza kwenye akili za watu wake.



Kwa mujibu wa viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ), elimu imekuwa uti wa mgongo wa maendeleo ya kijamii, kiuchumi na kisiasa tangu siku za mwanzo za Mapinduzi.

 


ELIMU KABLA YA MAPINDUZI, HISTORIA ISIYOFUTIKA
Kabla ya Mapinduzi ya 1964, sekta ya elimu Zanzibar ilikuwa dhaifu na yenye ubaguzi mkubwa.

 


Watoto wa wanyonge hawakuwa miongoni mwa wenye kuipata elimu na badala yake waliopata fursa ya kusoma ni wachache tena wenye uwezo na mamlaka pekee.

 

Mapinduzi matukufu ya mwaka 1964 yalileta mwanga mpya katika sekta ya elimu kwa kuwaondolea wazawa minyororo ya ujinga na ubaguzi uliokuwepo awali.

 

Kupitia Mapinduzi, elimu ilitangazwa kuwa haki ya kila mwananchi bila kujali asili, jinsia au hali ya kiuchumi.

 

Hatua hii iliwawezesha wazawa wengi kupata fursa ya kusoma na kujiendeleza kielimu, jambo lililoweka msingi imara wa maendeleo ya jamii.


Aidha, Mapinduzi yalihamasisha ujenzi wa skuli  nyingi za msingi, sekondari na taasisi za elimu ya juu katika maeneo mbalimbali.

 

Skuli hizo ziliwafikia wazawa waliokuwa wakiishi maeneo ya pembezoni ambao hapo awali walinyimwa huduma za elimu.

 


Upanuzi huu wa miundombinu ya elimu uliwezesha watoto wengi kuanza masomo na kutimiza ndoto zao.


Vilevile, Mapinduzi yalileta mageuzi katika mitaala ya elimu kwa kuhakikisha kuwa elimu inayotolewa inazingatia mazingira, utamaduni na mahitaji ya wazawa.

 

 

Elimu ikawa chombo cha kuimarisha uzalendo, kujitambua na kujenga fikra huru miongoni mwa wanafunzi.

 

Hii iliwawezesha wazawa kujiona kuwa sehemu muhimu ya ujenzi wa taifa lao bila ya ubaguzi.

 


Mapinduzi pia yaliimarisha mafunzo ya walimu na kuongeza ajira katika sekta ya elimu.

 

Walimu wazawa walipatiwa nafasi ya kusomea ualimu na kuchangia katika kuwalea kizazi kipya chenye maarifa na maadili.

 



Kupitia juhudi hizi, elimu ilizidi kuwa bora na yenye tija kwa maendeleo ya jamii.

 


Kwa ujumla, Mapinduzi yalikuwa chachu ya mabadiliko makubwa katika sekta ya elimu kwa kuwakomboa wazawa dhidi ya ujinga, umasikini na utegemezi.

 

Elimu ikawa nguzo muhimu ya maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kisiasa, hivyo, Mapinduzi yameacha alama isiyofutika katika historia ya elimu na ustawi wa wazawa.  

Katika makala hii naangazia mafanikio ya miaka 62  ya Mapinduzi ya Zanzibar katika sekta ya elimu kisiwani Pemba.

 

Kabla ya Mapinduzi , elimu ya msingi na  Sekondari Pemba  ilikuwa chache sana  na haikutosheleza  mahitaji ya wengi, na hii iliibua  haja ya mageuzi  makubwa kufikiwa kupitia mapinduzi ya 1964.

 

 Takwimu zinaonesha kuwa kabla ya Mapinduzi kwa upande wa kisiwa cha Pemba kulikuwa na skuli za msingi chache, ambapo skuli  za sekondari ilikuwa ni 1 pekee ambayo iliitwa  Sayyid Abdallah  na baadae Fidel Castro.

 

Kutokana na kuwa watoto wa wazawa hawakupata fursa ya kupata elimu hapo kabla ya Mapinduzi ilipelekea kuwa na idadi ndogo mno ya wanafunzi waliosoma kwani hakukuwepo na vyuo vikuu wala wataalamu.


Ali Saleh ni mmoja wa walimu wastaafu wa Pemba anakumbuka na kusema “Tulikuwa tunafundisha wanafunzi wengi sana katika mazingira magumu mapinduzi yalipokuja, yalitupa heshima na dira mpya ya ualimu.”


MAPINDUZI NA MAGEUZI YA MIUNDOMBINU YA ELIMU
Tangu mwaka 1964 hadi 2026 ambapo inatimia miaka 62 ya mapinduzi, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandika historia mpya ya elimu kwa vitendo na kwa takwimu.


Skuli  za msingi na  maandalizi Pemba zimefikia 113, wakati skuli za msingi pekee ni 35, na skuli za maandalili pekee ni 47, zikiwa jumla ya skuli hizo kufikia 196.

 

Kwa upande wa skuli za sekondari kutoka skuli moja hadi kufikia skuli 96 jambo ambalo ni faraja kubwa wa wananchi.

 

Kwa mujibu wa takwimu kutoka wizara ya elimu Pemba na  bajeti ya 2024/2025 jumla ya wanafunzi wote Pemba ni 201,729 wakati hapo kabla waliopata fursa ya elimu ni wachache mno wakiwemo watoto wa mabepari na matajiri peke yao.

 

Kwa upande wa wanafunzi wa sekondari ni 43,013, wanawake 23,616, wanaume 19,397 huku wanafunzi wa msingi wakiwa ni 130482, wanawake 63342 na wanaume 67140.

 

Wanafunzi wa maandalizi ni 20971, wanawake 10344 na wanaume 10627, ambapo kwa wanafunzi wa skuli za jamii (Tutu) ni 7263, wanawake 3644 na wanaume 3619.


Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Lela Mohamed Mussa amewahi kueleza“Mapinduzi yaliamua kwa makusudi kuifanya elimu kuwa msingi wa maendeleo ya Zanzibar, hii ndiyo sababu uwekezaji wake umeongezeka kila mwaka.”


SKULI ZA GHOROFA ALAMA YA ELIMU YA KISASA YA MAPINDUZI
Moja ya mafanikio makubwa zaidi ya SMZ ni ujenzi wa skuli za ghorofa, ambao umeleta sura mpya ya elimu Zanzibar nzima.

 

Mwaka 1964 hakukuwa na hata skuli moja ya ghorofa leo hadi 2026 Zanzibar nzima imebarikiwa kuwa na skuli za ghorofa ambapo kwa Pemba zimefikia 23 huku kukiwa na nyengine 18 ziko katika hatuwa ya ujenzi.

 

Skuli hizi zimejengwa katika wilaya zote, kuanzia Mkoani, Chake chake, Wete na  Micheweni ambapo 7 zipo wilaya ya Mkoani ,5 Chake ,5 wete na 6 Micheweni.

 

Makamu wa Pili wa rais Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla katika hotuba moja ya kielimu alisema “Skuli za ghorofa ni mkakati wa kimapinduzi unaotuwezesha kutumia ardhi kidogo kutoa elimu kwa watoto wengi zaidi.”


Kwa upande wao, walimu wanasema skuli za ghorofa zimeleta mabadiliko makubwa kwani kila mmoja anapata nafasi ya kusoma sawa na mwengine. 

Mwalimu wa skuli ya Sekondari ya Makombeni Wilaya ya Mkoani Khamis Mohamed Ussi anasema “Tuna madarasa ya kisasa, maabara na mazingira bora ya kufundishia, hili halikuwepo miaka ya nyuma.”


WALIMU NA WATAALAMU WA ELIMU 
Kabla ya mapinduzi mwaka 1964, idadi ya walimu na wataalamu wa elimu ilikuwa ndogo sana.

 

Leo Zanzibar katika kisiwa cha Pemba kina maelfu ya walimu wa maandalizi, msingi na sekondari.


kwa mujibu wa Takwimu Wizara ya elimu Pemba walimu wa  maandalizi na msingi ni 3676, wanawake 2856 huku wanaume wakiwa 820 wakiwa ni wazalendo.

 

Kwa upande wa sekondari walimu ni 1881, wanawake 847 na wanaume 1034, huku wataalamu wa mitaala wakifikia 5 mwanamke mmoja na wanaume 4.

 

Kabla ya mapinduzi hakukuwa na vyuo vikuu ,kati na uwalimu wala wahadhir ambapo kwa sasa vyuo hivyo vipo  13, vikiwa 6  vya Serikali na 7 binafsi.

 

Wahadhir wapo 162, wanaotowa fani mbalimbali, kwa upande wa wakaguzi wa elimu wapo 43, wanawake 18 na wanaume 25.

 


Afisa Mdhamini Wizara ya Elimu Pemba Mohamed Nassor Salim anasema“Kupitia sera za Mapinduzi, walimu wamepata mafunzo endelevu na hadhi yao imeimarika.”

 ELIMU BURE AHADI YA MAPINDUZI KWA WANANCHI

 Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendelea kutekeleza sera ya elimu bure kuanzia maandalizi hadi sekondari.

 

 Hatua hii imeongeza uandikishaji wa wanafunzi na kupunguza idadi ya watoto waliokuwa nje ya mfumo wa elimu.

 


Mzazi Amina Bakar Mohamed wa Machomane Chake Chake anasema “Leo mtoto wa maskini anasoma sawa na mtoto wa tajiri, hili ni tunda la Mapinduzi.”


SERA, SHERIA NA MIKAKATI YA KUKUZA ELIMU


Sera ya Elimu Zanzibar inasisitiza kuwa elimu ni haki ya msingi kwa kila mtoto na lazima itolewe kwa usawa bila ubaguzi wa jinsia, dini au hali ya kiuchumi.

 

Sera hii inalenga kuhakikisha upatikanaji wa elimu bora kwa wote, kuanzia elimu ya awali hadi elimu ya juu.

 

Kukuza elimu ya amali na ufundi stadi ili kuandaa rasilimali watu wenye maarifa, ujuzi na maadili mema kwa maendeleo ya taifa.

 

Sheria za elimu Zanzibar  zinalazimisha wazazi na walezi kuhakikisha watoto wanapata elimu ya lazima, sambamba na kudhibiti uendeshaji wa skuli za umma na binafsi.

 

Pia sheria zinaweka viwango vya ubora wa elimu, nidhamu maskulini, haki na wajibu wa walimu pamoja na ulinzi wa watoto katika mazingira ya skuli.


Mikakati ya kukuza Elimu Zanzibar inalenga kuboresha miundombinu ya skuli, kuongeza idadi na ubora wa walimu, kuimarisha mitaala na matumizi ya TEHAMA katika elimu.

 

Mikakati hiyo pia inahusisha kutoa mafunzo endelevu kwa walimu, kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia, pamoja na kushirikisha jamii na wadau mbalimbali.

 

Ili kuhakikisha elimu inakuwa chombo cha maendeleo endelevu ya kijamii na kiuchumi ndio maana bajeti ya elimu ikafikia zaidi ya Shilingi bilioni 864 kwa mwaka 2025/2026.


Kwa mujibu wa Katibu Mkuu Wizara ya Elimu Zanzibar Khamis Abdalla Said anasema “Sheria na sera hizi zimeweka msingi wa elimu yenye ubora, ushindani na inayojibu mahitaji ya maendeleo ya Zanzibar.”

 


WANANCHI WANAVYOSHUHUDIA MAFANIKIO YA ELIMU 


Asha Omar wa Chake chake na Fatma Abdalla wa Vitongoji wanasema mabadiliko ya elimu yanaonekana kwa macho skuli zimekaribia jamii mazingira ya kujifunzia yameimarika fursa za elimu zimeongezeka.

 

Asha Muhidini wa  Micheweni anasema“Skuli za ghorofa zimekuwa fahari ya maeneo yetu, hii ni Zanzibar mpya.”

 

Ali Bakar Kombo wa Mwambe anasifia kwa furaha kuwa kwa sasa wanafunzi wanasoma bila ya kubanana madarasani, ni faida kubwa kwa wananchi.

 

Mapinduzi yamejithibitisha kupitia elimu
miaka 62 baada ya Mapinduzi, sekta ya elimu Zanzibar katika kisiwa cha Pemba imegeuka kutoka mfumo dhaifu hadi nguzo ya maendeleo ya taifa.

 

 MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...