Skip to main content

MATUMIZI YA POMBE, DAWA ZA KULEVYA KWA WAZAZI NI BALAA KWA WATOTO



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MATUMIZI ya pombe na dawa za kulevya kwa wazazi na walezi, imetajwa kuwa ni chanzo cha watoto wao, kuishi katika mazingira magumu, yanayoweza kuwaingiza katika majanga.

Hayo yameelezwa leo Januari 24, 2026 na mtoa mada Rashid Said Nassor, alipokuwa akiwasilisha mada ya kuwasaidia wazazi na familia, kwenye muendelezo wa mafunzo ya siku tano, ya ulinzi na hifadhi ya mtoto, yanayofanyika ukumbi wa zamani wa TASAF, yakifadhiliwa na UNICEF.

Alisema, matumizi ya pombe na dawa za kulevya, huwapa wakati mgumu wazazi hao, katika kupanga mipango na mikakati ya malezi ya watoto wao, jambo ambalo linaweza kuwaingiza kwenye majanga.



Alieleza kuwa, watoto hao wanaweza kujiongoza wenyewe kwenye malezi na makuzi yao, na ikiwa jamii iliyowazunguruka ni yenye tabia mbaya, huwa rahisi kwa watoto hao kudhalilishwa.

Rashid alifafanua kuwa, khatma ya matumizi ya pombe na dawa za kulevya kwa wazazi na walezi, ni kuwakosa watoto waliozaliwa ndani ya familia, kimalezi na kimakuzi.

‘’Tuwaombe wazazi na walezi, waache matumizi ya pombe na dawa za kulevya, kwani hukosa muda wa kuendeleza malezi sahihi ya watoto wao,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, alisema ni vyema wazazi wakaunda mitandao ya kijamii yenye tija kwa maslahi yao ya sasa na baadae, kwani huwa ni dalili ya kuwa na watoto wema.

‘’Familia ikiwaunganisha watoto na majira wema, wajomba, kaka na ami zao, huwa na uhakika wa kuishi katika mazingira salama,’’alifafanua.



Aidha aliwashauri wazazi na walezi hao, kuwashirikisha watoto kwa mambo yanayowahusu, ikiwemo eneo la kupata elimu kwa maendeleo yake.

Hata hivyo amewakemea wazazi kuacha kuwafanyia ukatili watoto wao, kwani hujenga ukuta mbovu wa maelewano, na kuwakosa katika namna ya kujenga familia bora.

‘’Wazazi ukimfanyia udhalilishaji ama jinai nyingine mtoto wako, huwa ni changamoto endelevu, na kusababisha kuvunja uhusiano wa milele,’’alifafanua.



Afisa ustawi wa Jamii kutoka Unguja Fatma Maulid, alisema changamoto nyingine iliyopo kwa watoto, ni kutolewa na baadhi ya familia zao na kutumikishwa kwa kazi za ndani.

Alisema, ijapokuwa bandarini ya Unguja, wapo maafisa wao, ambao wakati mwingine huchukua hatua, wanapowagundua na kuwasafirisha walikotoka, ikiwa wameingia Zanzibar kwa lengo la kufuata ajira.

Akiwasilisha mada ya madhara ya udhalilishaji kwa mtoto, mtoa mada Husna Haji Othman ambae ni Afisa Ustawi wa Jamii wilaya ya Chake chake, alisema kufanya hivyo kunaweza kumsababishia kukosa kutimiza ndoto zake.



Alieleza kuwa, athari nyingine, ni kuwepo kwa msongo wa mawazo, jambo ambalo linaweza kumsababishia hata kifo hapo baadae.

Katika hatua nyingine, alisema aina nne kuu ambazo zimeanishwa kwenye kanuni ni udhalilishaji wa kingono utekelezaji, kihisia na udhalilishaji katika ajira.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, walisema suala la kumuadabisha mtoto huwa sio kosa kisheria, bali jambo baya ni kumuadhibu kama ilivyo baadhi ya wazazi.

Kassim Ali Omar, alisema suala la kumuadabisha mtoto, ni jambo la kawaida, ili mtoto ajue namna ya kuishi na jamii yake.







Mdau wa haki za watoto, Abduu Salim Mohamed alisema uwepo wa mikataba na sheria aa kupinga adhabu kwa watoto, ni eneo jipya la kulea watoto bila ya adhabu kama ilivyokuwa zamani.

Mafunzo hayo ya siku tano yalioandaliwa na Kamati ya kupamba na udhalishaji ya wilaya ya Chake chake, yamefadhiliwa na UNICEF na mada kadhaa ikiwemo malezi, makuzi ya awali ya mtoto pamoja na madhara ya udhalilishaji ziliwasilishwa.

                mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...