Skip to main content

MIAKA 62 YA MAGEUZI MAKUBWA YA SEKTA YA AFYA KUTOKA UHABA, MARADHI NA VIFO VINAVYOZUILIKA HADI HUDUMA ZA KISASA KISIWANI PEMBA.

 


HABIBA ZARALI, PEMBA@@@@


Mapinduzi ya 12 Januari 1964 ni tukio la kihistoria lililobadili mwelekeo wa maisha ya Mzanzibari katika nyanja zote za kijamii.

 

Mapinduzi ya mwaka 1964 yalikuwa ni Mapinduzi ya uhai yakitambua kuwa bila afya bora, hakuna maendeleo, hakuna elimu, wala hakuna uchumi.

 

Miaka 62 ya mapinduzi hayo, sekta ya afya Zanzibar nzima inasimama kama ushahidi usiopingika kwamba Mapinduzi yamelinda  maisha ya wananchi kwa vitendo.

 

KABLA YA MAPINDUZI


Kiuhalisia kwa upande wa kisiwa cha Pemba  kabla ya Mapinduzi matukufu ya 1964, huduma za afya zilikuwa katika hali ya kusikitisha.


Kwa vile Zanzibar nzima ilikuwa na hospitali kuu moja tu ya  Mnazi Mmoja ni wazi kuwa kwa upande wa Pemba ilikuwa na huduma finyu sana za afya.


Hakukuwa na hospitali kuu badala yake kulikuwa na hospitali 2 ya Chake chake na Wete, kwa upande wa vituo vya afya vilikuwa ni 14 tu huku vikiwa  havina dawa wala wataalamu wa kutosha.

 

Madaktari wazalendo walikuwa 4  ambapo madaktari bingwa hawakuwepo, wauguzi walikuwa wachache jambo ambalo lilichangia wananchi wengi kupoteza maisha kwa magonjwa yanayoweza kuzuilika.



 

 

Hakukuwa na huduma za kibingwa, akina mama wengi walijifungulia majumbani bila msaada wa kitaalamu.

 

 

Kutokana na hali hiyo kabla ya mapinduzi wananchi wanyonge walishindwa kupata huduma za afya na badala yake walikuwa wagonjwa wengi wasio na tiba.

 

Kwa kweli maisha ya wanyonge yalikuwa hatarini kwani hata vifaa vya matibabu havikuwepo na vilivyokuwepo ni vya watu maalum.

 

Kabla ya Mapinduzi upatikanaji wa dawa  ulikuwa ni mdogo na zaidi zilikuwa zinapatikana kwa tabaka tawala.

 

Kabla ya Mapinduzi hapakuwa na ghala maalumu la kuhifadhia dawa.

 

 

Huduma za uchunguzi zilikuwa zinapatikana kwa kiwango cha chini na mara nyingi zilipatikana kwa tabaka tawala pekee.

 

Hakukuwa na huduma za uchunguzi kwa njia ya mionzi, ambapo kwa sasa kuna huduma za uchunguzi kwa njia ya mionzi (X-ray, atrasound, CT scan ,MRI)

 

Huduma ya matibabu ya figo haikuwepo(dialysis) , hakukuwa na gari maalum ya kubebea wagonjwa (Ambulance), wala hakukuwa na  mtambo wa kuzalishia Oxygen kisiwani Pemba

 


Wakati huo hakukuwepo na mtambo wa kuchomea taka,taka za hospitali zilikuwa zinachomwa katika incenarator ndogo za hospitali

 

Kabla ya Mapinduzi ya mwaka 64, Wizara ya Afya Pemba ilikuwa na nyumba 10 tu ambazo zilikuwa zinaishi familia 26, nyumba hizo zilikuwepo Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba.

 

 

 

 
BAADA YA MAPINDUZI

 

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeiweka afya kama haki ya msingi ya mwananchi.

 

 

Ndani ya miaka 62, sekta ya afya imepanuka kwa kiwango kikubwa kuanzia
miundombinu ya Afya.

 

Kisiwa cha Pemba zipo hospitali 4 za ngazi ya Wilaya ikiwemo ya Chake - Vitongoji, Hospitali ya wilaya ya Wete - Kinyasini, Hospitali ya  wilaya ya Micheweni na Hospitali ya Wilaya ya Mkoani .

 

Kwa upande wa hospitali ya Mkoani hutumika kama hospitali ya rufaa kwa kisiwa cha Pemba kutokana na huduma zinazotolewa.

 

Aidha, kwa sasa Pemba kuna hospitali maalum ya matibabu ya wagonjwa wa afya ya akili ambayo ipo Pandani na imefunguliwa rasmi tarehe 01/01/2026.

 

 

Wizara ina jumla ya vituo afya 72 vinavyotoa huduma za afya za msingi kisiwani Pemba.

 


Katika hivyo kuna dispensari 51 na health Center 21 ambazo Health center hizo zinatoa huduma za msingi na ziada (zikiwemo za huduma za uzazi, maabara na huduma za meno).

 

 

Aidha, wizara inaendelea na ujenzi wa health center 6 Konde, Maziwang'ombe, Jadida, Kiuyu Minungwini, Chonga na Mtambile.

 

Baada ya kukamilika vituo hivi vitatoa huduma za matibabu yakiwemo ya wagonjwa wa nje, wagojwa wa kulazwa.

 

 Na kila kituo kitakuwa na uwezo wa kulaza wagonjwa 25 kwa wakati mmoja.

 

Huduma za mama na mtoto, huduma za upasuaji mdogo (minor theater) huduma za maabara, huduma za ultrasound na huduma za X - ray.

 

 

Kwa upande wa madaktari bingwa (speacialist) wapo 16 ambao wote ni wazawa.

 

Wizara ina madaktari MD 70 wazalendo na madaktari 8 tu ndio wakigeni, wauguzi 578 ambao wanafanyakazi katika hospitali na vituo vya afya vyote.


 

Upatikanaji wa dawa ni mkubwa kwa sasa umefikia asilimia 80 ya dawa muhimu ambazo zinatolewa bila malipo kwa wananchi wote.

 

 

Aidha katika uboreshaji wa upatikanaji wa dawa, Wizara imejenga ghala (bohari) la kuhifadhia dawa Vitongoji ili kuhakikisha wananchi wote wanapata dawa kwa wakati.

 

Huduma za uzazi zimeimarika na zinatolewa bure kwa wananchi wote wa mijini na vijijini , hali hii imepelekea wananchi walio wengi kujifungulia katika vituo vya afya,  ambavyo vinapatikana katika wilaya na majimbo yote na vinafanyakazi kwa masaa 24.

 

Huduma za uchunguzi wa maabara zimeimarika kwa kiwango kikubwa, zinapatikana katika kila Wilaya kupitia hospitali na vituo vya afya (health center).

 

Huduma za x-ray zinapatikana katika hospitali za wilaya, wakati huduma za ultrasound zipatikana katika baadhi ya vituo vya afya vinavyotoa huduma za uzazi na hospitali zote.

 

Aidha, huduma za Ct Scan na MRI zinapatikana katika hospitali ya Abdulla Mzee Pemba.

 

Huduma za matibabu ya figo inapatikana kwa wakati wote katika hospitali ya Abdulla Mzee.

 

Kwa sasa Pemba ina Amblance 9 ambazo zinafanya kazi ya kubebea wagonjwa kila wilaya.

 

Wizara ya Afya imefunga mtambo wa kuzalishia Oxygen ambao upo Vitongoji kitu ambacho kwa sasa hakuhitajiki kusafirisha mitungi ya gesi kwenda Unguja kujaza oxgen.

 

La kujivunia ni kuwa gesi hiyo imeunganishwa na kitanda cha mgonjwa moja kwa moja

 

Kwa sasa kuna mtambo mkubwa wa kuchomea taka zinazozalishwa katika hospitali na vituo vya Afya vyote vya Serikali na Binafsi.

 



Kwa upande wa  majengo  ya ghorofa yapo  7 ambayo kwa pamoja yana uwezo wa kuchukuwa familia 120.

 

Katika hizo block 4 za familia 76 zipo  Abdalla mzee , block 1 ya familia 16 ipo Kinyasini hospitali, block 1 ya familia 12 ipo hospitali ya wagonjwa wa akili Pandani.

 

Wakati block nyengine 1 ya familia 16 ipo katika hatua za umalizaji wa ujenzi hopitali ya vitongoji.


Miongoni mwa hospitali muhimu kisiwani Pemba ni ile ya Abdalla Mzee Mkoani ambayo ni jicho la wananchi kisiwani humo, hospitali ya vitongoji , hospitali ya Chake, hospitali ya Wete na Micheweni.

 


Hii inaonesha wazi kuwa Mapinduzi hayakujenga afya mjini pekee, bali Zanzibar nzima na wananchi wote wanafikiwa na huduma bora za matibabu.

 

 

Makamu wa Rais wa Zanzibar Hemed Suleiman Abdulla anasema
“Mapinduzi hayawezi kuwa kamili bila kulinda uhai wa wananchi.”




Katibu Mkuu Wizara ya Afya Zanzibar Dkt Mngereza Mzee Miraji anasema “Lengo la Mapinduzi lilikuwa kuhakikisha hakuna Mzanzibari anayekosa huduma za afya kwa sababu ya mahali alipo.”

 


“Kwa kweli tunao wataalamu wa afya mbalimbali wakiwemo wa upasuaji, magonjwa ya wanawake na watoto, moyo, figo, maabara, mionzi (Radiology), usingizi (Anesthesia) na magonjwa mengine mengi.”anasema.

 


Daktari wa upasuaji hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani Haji Machano Mussa anasema leo wanafanya upasuaji ambao zamani ulilazimisha wagonjwa kusafiri nje ya Pemba.

 

 “Haya ni matunda ya Mapinduzi vifaa vya kisasa vya matibabu vipo”,anasifia kwa bashasha,

 

Mapinduzi ya Teknolojia ya Afya kabla ya Mapinduzi ya mwaka 1964 hakukuwa na CT Scan, hakukuwa na ICU za kisasa
Maabara zilikuwa za msingi sana.

 

Muuguzi wa hospitali ya Abdallah Mzee Pemba Rabia Mohamed Ussi anasema
“Vifaa vimepunguza vifo na wagonjwa wanapata huduma kwa wakati.”


Afya ya mama na mtoto mafanikio yanayoonekana kupitia sera za Mapinduzi.


Vifo vya akina mama wajawazito vimepungua kwa kiasi kikubwa, huduma za uzazi zimeimarika,chanjo za watoto zimeenea Zanzibar nzima

 

SAUTI ZA WANANCHI


Mwananchi wa Micheweni, Ali Kombo akitowa ushuhuda wa mafanikio anasema “Zamani tulivuka bahari kwenda Unguja, leo tuna hospitali yetu tunatibiwa hapa hapa Micheweni liwe kubwa ndo tunapelekwa Abdalla Mzee bado tuko Pemba.”


“Afya imekuwa karibu na wananchi hasa pale wanapopata matibabu katika hospitali za karibu” anasema Fatuma Vumba wa Mwambe

 

Anasema jambo la kujivunia kuona wananchi humalizia hospitali ya Abdalla mzee kwa matibabu makubwa bila hata kwenda nje ya Unguja ama Tanzania Bara.


 Khadija Ali wa Chokocho anasema “Leo tunajifungulia hospitali salama, zamani ilikuwa hatari sana mapinduzi yameokowa maisha ya watu wengi tena walio  wanyonge.”

 

 

Sekta ya afya imeimarishwa kupitia
Sera ya Afya Zanzibar isemayo afya kwa wote, huduma bora na nafuu, kipaumbele kwa mama na mtoto.


Sheria ya Afya ya Umma, udhibiti wa ubora wa huduma, usalama wa wagonjwa,usimamizi wa sekta binafsi.


Mikakati ya Kitaifa, ujenzi na ukarabati wa hospitali mafunzo ya wataalamu ndani na nje ya nchi, ununuzi wa vifaa tiba, ushirikiano na wadau wa maendeleo.

 


Miaka 62 ya Mapinduzi ya Zanzibar imeandika historia mpya ya sekta ya afya kutoka hospitali moja hadi mtandao wa hospitali, vituo vya afya , kutoka madaktari wachache hadi maelfu ya wataalamu.

 

Kutoka vifaa duni hadi teknolojia ya kisasa  huu ni ushindi wa Mapinduzi kwa uhai wa Mzanzibari.


Hii si hadithi ya sifa, bali ni ushahidi wa takwimu kwamba Mapinduzi yameokoa, yanalinda na yataendelea kulinda maisha ya wananchi wa Zanzibar.


 MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...