Skip to main content

WAANDISHI WAPEWA SOMO HABARI JUMUISHI NA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

 


NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@

WAANDISHI wa habari nchi wametakiwa kujikita katika kuandika  habari  jumuishi na haki za watu wenyeulemavu, ili kuongeza upatikanaji wa haki na michango yao katika maendeleo ya taifa. 

Wito huo umetolewa na Afisa Programu na Mawasiliano wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania (TAMWA - Zanzibar) Khairat Ali Haji wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari juu ya uwandishi jumuishi. 

Akizungumza katika mafunzo hayo alisema waandishi wananafasi kubwa katika kubadilisha mitazamo hasi kuhusu watu wenye ulemavu, hivyo ni vyema  kutumia nafasi walizonazo ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanashirikishwa katika hatua za kimaendeleo. 

" Waandishi wa habari wanakua na mchango mkubwa katika kubadili mitazamo iliomo katika jamii, hivyo ni muhimu kutumia nafasi hii kubadili mitazamo hayo, kwa kuwaibua na kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika kila hatua za kimaendeleo"alisema.

Aliongeza kua, mafunzohayo ni miongoni mwa juhudi za kuhakikisha vyombo vya habari vinashiriki katika utetezi wa haki za watu wenye ulemavu, kwa kuibua sauti zao pamoja na uonyesha uwezo walionao katika kushiriki kwenye hatua mbali mbali za kukuza maendeleo ya nchi. 

Akiwasilisha mada katika mafunzo hayo Mwenyekiti wa baraza la watu wenye Ulemavu Zanzibar Salma Haji Saadati alisema, ulemavu ni hali ya upungufu wa kimwili, kiakili au kihisia unaomzuia mtu kushiriki katika shughuli za kijamii kama wanavyoshiriki wengine. 

Alieleza kua, kumekua na ongezeko la watu wenye ulemavu duniani kote, hii nitokana na sababu mbali mbali, ikiwemo maradhi, ajali, vita, utapiamlo utokanao na lishe duni pamoja na umasikini. 

Alifafanua kua kwa mujibu wa ripoti ya Shirika  la Afya Ulimwenguni (WHO), 2025 watu wenye ulemavu wamefikia asilimia 16 ya watu wote duniani, ikiwa ni ongezeko la asilimia  moja kutoka asilimia 15 ya mwaka 2011.



Aidha alieleza  kua matokeo ya Sensa ya watu na makaazi ya mwaka 2022, yameweka wazi kua asilimia 11.2 ya watu wote  Tanzania bara ni wenye ulemavu, huku Zanzibar ikifikia asilimia 11.4 kati ya watu Milioni 1.8 ikiwa ni ongezeko la asilimia 5 kutoka mwaka 2012.

" Takwimu zinaonesha kua kunaongezeko la watu wenye ulemavu kila uchao, na nikutokana na sababu mbali mbali, ikiwemo maradhi, ajali, vita na mengineyo, na asilimia 50 ya ulemavu unatokana na umasikini na asilimia 20 ni kutokana na utapiamlo, ambapo mawili haya yanaweza kuzuilika" alieleza. 

Alieleza kwamba, changamoto wanazokutana nazo watu wenye ulemavu mara nyingi husababishwa na jamii husika, hii ni kutokana na mitazamo hasi ilionayo jamii jambo linalopelekea unyanyapaa, kutengwa na kudharauliwa. 

Aliongeza kua, mara nyingi jamii humuangalia mtu mwenye ulemavu kama ni mtu tengemezi katika kila kitu, jambo linalopelekea kumnyima fursa mbali mbali anazostahili, ikiwemo elimu, uchumi, na ushiriki katika nyanja za siasa. 

Alisisitiza kua, pamoja na kuwepo kwa sera, sheria na mikataba mbali mbali yanayoeleza haki za watu wenye ulemavu, lakini bado jamii haijazingatia ipasavyo kuhusu umuhimu wa  sera, kanuni, shria na mikataba hiyo. 

Hivyo ametoa wito kwa washiriki wa mafunzo hayo, kuhakikisha wanaielimisha jamii kuhusu haki na umuhimu wa ushiriki na ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu katika shughuli mbali mbali za kimaendeleo, ili kubadilisha mitazamo hasi iliomo katika jamii juu ya watu wenye ulemavu. 

Nao washiriki wa Mafunzo hayo walisema, watatumia mafunzo waliopatiwa katika kuhakikisha wanawajumuisha, kulinda na kutetea haki za watu wenye ulemavu, ili kuongeza uwelewa kwa jamii juu ya uwezo na mchango mkubwa walionao watu wenye ulemavu katika maendeleo ya nchi. 

Mafunzo hayo ni miongoni mwa utekelezaji wa mpango 'Collective Actions for Disability Right ' unaolenga kunyanyua sauti, haki, ushiriki na ushirikishwaji wa watu wenye ulemavu katika jamii kupitia vyombo vya habari, sera na mipango ya maendeleo. 

Mradi huo unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya TAMWA-Zanzibar, ZANAB na Baraza la Taifa la Watu wenye Ulemavu Zanzibar. 

                                                                 MWISHO


Comments

Post a Comment

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...