Skip to main content

WANAOJIFUNGULIA MAJUMBANI WAZUNGURUKWA NA MAJANGA LUKUKI, KIFO KUPOTEZA DAMU VIMO

 

NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@

‘MIMBA yangu ya nne manusura niiage dunia’.

Asha Said mama wa watoto wanne ambae sio jina lake halisi anasema, mimba yake ya pili alijifungulia nyumbani, na alipata tatizo la kutokwa na damu nyingi, na kupelekea hadi kupoteza fahamu.

‘’Baada tu ya kujifungua sikujifahamu tena, mpaka nilikuja kuzinduka nimewekewa chupa ya maji hospitali ya Micheweni,’’anaeleza.

Mume wa mama huyo ambae hakupenda jina lake lichapishwe, anasema baada ya kuona hali ya mke wake imeshakuwa mbaya, ndipo usiku huo, alipokodi gari na kumpeleka Hospitali.

Hivyo alipatwa na huzuni, hali ambayo ilipelekea kupoteza gharama kubwa ya matibabu, kwa ajili ya kuokoa maisha ya mke wake, pamoja na mtoto.

 ‘’Nilipata funzo na sasa nikimuona tu uchungu umeanza namuwahisha hospitali haraka, kwani huko akipata matatizo anaweza akawahiwa mapema na watalamu wa afya,’’anaeleza.

 Maryam Said mkaazi wa Chake chake ambae anaishi na virusi vya ukimwi kwa muda wa miaka 18, alimuambukiza mtoto wake wa mwanzo mambukizi ya virusi vya ukimwi.

Kwani mimba yake ya kwanza, alijifungulia nyumbani, kwa hofu ya kwenda hospital kwa kuogopa kunyanyapaliwa na wahudumu wa afya kwa wakati huo.

‘’Hadi leo najilaumu, na najutia nafsiyangu, kwa kitendo cha kutokimbilia hospitali kwa ajili ya kwenda kujifungua, nikidhani kwamba nyumbani ni salama,’’anasimulia.

 Kwa sasa ameshajifungua watoto wingine watatu, ambao wako salama na vvu, baada ya kusikiliza na kutekeleza kwa vitendo, ushauri wa watalamu wa afya.

Kumbe hata Halima Juma wa Mjini Kiuyu wilaya ya Wete nae amepitia machungu kwa kule mimba zake tatu kujifungulia nyumbani.

Linalomkimbiza hosptali anasema ni lugha za madaktari, nenda rudi isiyozaa matunda na hata suala la uhaba wa watalamu halimshawishi kujifungulia hospitali.

Khadija Khamis mama wa watoto watano, mkaazi wa Sizini hadi leo hii bado hajafikiwa na elimu ya kuhudhuria kliniki, na ndio maana hufika kwa watalamu baina ya miezi sita hadi saba ya ujauzito.

 ‘’Mimi sipendi kwenda kituo cha afya ikiwa bado mimba ni changa, si pendi ile kila siku nenda na keshokutwa uje tena naona tabu,’’anfafanua.



Amina Omar Msellem mkaazi wa Chake chake anasema amejifungua mimba saba na zote ni kituo cha afya, wala hajapata changamoto yoyote yeye wala watoto wake.

‘’Tuache kuzaa changamoto zetu wenyewe, kama hatutaki kuhudhuria kliniki tukae kimnya, lakini unapokwenda unapewa huduma kama ilivyotakiwa, maana daktari hajiskii vizuri kumpokea mjamzito kisha kufariki,’’anasema.

MTAALAMU WA AFYA HUDUMA YA MAMA NA MTOTO

Akieleza athari anazozipata mama mjamzito anapojifungulia nyumbani Maryam Ali Said Mratibu wa huduma za mama na mtoto Pemba, anasema moja ni kukosekana kwa  huduma za mapema za kimataibabu.

 ‘’Inawezekana mama hawezi kujifungua kwa njia ya kawaida, analazimika afanyiwe upereshini, lakini mkunga wa jadi hana taluma ya kujua hilo,’’anaeleza.

 Anasisitiza kuwa, kuhudhuria kituo cha afya kuanzia wiki ya mwanzo ya ujauzito hadi kufikia kujifungua ni lazima kwa mjamzito, ili kujikinga na majanga.

‘’Kujifungulia nyumbani ni sawa na kununua mauti, ya mama na mtoto wake, maana hakuna mtalamu, vifa vya kinga ya maradhi na wengine wanaishi mbali na vituo vikuu vya afya,’’anasema.

Fatma Suleiman Daudi msimamizi wa huduma ya mama na mtoto hospital ya Chake chake, anaeleza kuwa, mjamzito akijifungulia nyumbani, huwa rahisi mno kumuambukiza maradhi mtoto wake na  mkunga.

‘’Kama mama atakua ana mambukizi kama vile homa ya Ini au Virusi vya ukimwi, bila ya kutumia kifaa kinga cha aina yoyote, anaweza kusababisha mtoto, mkunga kupata mambukizi,’’anaeleza.

 Mjamzito anaejifungulia nyumbani, anaweza kupata athari kiwemo kukaa kwa muda mrefu na uchungu, jambo ambalo linaweza likasababisha kuchanika haraka kwa fuko lake la uzazi.

‘’Mara nyingi wanapokuja Hospitali inakua mama ameshachoka, hali taabani, mpaka iwe wameshashindwa, hata ukija ukitoa tena hizo tiba muda umeshapita,’’afafanua.

Kumbe unapochanika kwa fuko la uzazi maranyingi mama, hutokwa na damu nyingi ambayo inaweza kusababisha hata kifo chake.

‘’Unapochanika kwa fuko la uzazi, hatuwezi kusema kama ndio mwisho wa maisha, lakini kama hukuwahiwa mapema kupatiwa matibau unaweza ukapoteza maisha,’’anafafanua.



 ‘’Kuna siku tulimpokea mama na alikuwa ni ujauzito wa tatu, alivyo kuja akapelekwa kwenye chumba cha kujifungulia, kabla ya kumlaza kwa ajili ya kujifungua, tulimuhisi kalala kumbe ameshafariki,’’anasimulia.

WANAUME WANASEMAJE?

Abdalla Nassor Abdala mwananchi wa Chake chake anasema, mama anapojifungulia nyumbani, mazingira  ya usafi pamoja na usalama wa mama kujifungua salama yanakua, hayatoshelezi.

Mkewake amejifungua mimba nane, na zote alikua anampeleka hospitali wakati anapoumwa tu na uchungu, na hawajahi kulalamikia huduma,’’anafahamisha.

Khamis Haji Omar, anasema ameshamsindikiza mke wake hospitali kujifungua mara nne, bila ya changamoto yoyote.

SERIKALI

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja anasema ni vyema kwa wizara ya Afya, kuongeza mkakati wa elimu ili wanawake washawishike kujifulia hospitalini.

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui anasema wizara imeimarisha miundombinu ya kutolea huduma hospitalini, ili kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi.

 Afisa Mdhamin wizara ya Afya Khamis Bilal Ali, amewataka wahudumu wa afya kuwa na lugha nzuri kwa wajawazito, ili iwe ni sehemu ya ushawishi ya kuhudhuria kliniki.

‘’Wizara kwa upande wake inaendelea kuimarisha miundombinu bora ikiwemo vifaa tiba dawa, lakini ni nafasi kwa watalamu wetu wa afya, nao kutumia lugha laini ili kufanikisha hilo’’,anasema.

Wizara ya Afya Zanzibar imechukua hatua kadhaa kuhakikisha wajawazito wanapata huduma bora wakati wa kujifungua. Hapa ni baadhi ya mikakati na hatua wanayochukua:

Mikakati mwingini ni upatikanaji wa Huduma za Afya, ambapo Wizara inahakikisha kuwa vituo vya afya vinapatikana kwa urahisi, ili wajawazito waweze kujifungulia salama.

Mkakati wa elimu kwa wajawazito, hapa Wizara inaendelea kutoa elimu kwa wajawazito kuhusu umuhimu wa kujifungulia hospitalini na athari za kujifungulia nyumbani.

 

Eneo jingine ni kuimarisha vifaa tiba, ambapo hapa wizara inahakikisha kuwa hospitali zina vifaa tiba vya kutosha kwa ajili ya kujifungulia, ikujumisha vitanda, vifaa vya upasuaji, na dawa.

 

Hata hivyo wizara hiyo imesema katika kuwavuta wajawazito kujifungulia hospitali, wanaimarisha ufuatiliaji kwa kufuatilia takwimu za kujifungua, ili kubaini maeneo yanayohitaji kuimarishwa zaidi.

 

TAKWIMU

Kwa mujibu wa takwimu kutoka ofisi ya mama na mtoto Pemba, inaonyesha kuwa, mwaka 2022 wajawazito 2019, walijifungulia nyumbani, kati ya hao  wanne [4] walifariki.

Waliojifungulia hospital ni 1,6269 kati ya hao, Micheweni ni 985, Mkoani 754, Wete 9445 na Chake chake 5365, ambapo waliofariki kutoakana na uzazi ni 15.

Kuanzia mwezi Januari hadi Juni mwaka 2023, wajawazito waliojifungulia nyumbani ni 1,450, kwa upande wa wilaya ya Mkoani walikua ni  270, Chake chake 99, Micheweni 230 na Wete ni 292.

Ingawa wanaojifungulia Hospital kwa Pemba ni 8481, ambapo kwa  wilaya ya Mkoani ni 1562, Chake chake 2601, Wete 2140 na Micheweni 2178, huku vifo vikiwa tisa [9], ambapo Wete na Micheweni kulikuwa na vifo vitatu vitatu.

                                   MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan