Skip to main content

SIKU YA MTOTO WA AFRIKA, FAMILIA ZIWAPE UHURU WA KUCHEZA WATOTO WENYE ULEMAVU KUWAFUNGIA NI KUDIDIMIZA VIPAJI VYAO

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SIKU ya mtoto wa Afrika, ni siku maalum inayoadhimishwa kila mwaka, kwa lengo la kujenga ufahamu na kuongeza juhudi za kuimarisha hali ya watoto barani Afrika.

Ambapo kilele cha siku hii, iliadhimishwa Juni 16 ya kila mwaka, kwa lengo la kuwakutanisha watoto, kujadili mafanikio na changamoto zao.

Siku hii, inaanzia pale mwaka 1991, wakati wa mkutano wa kwanza wa baraza la mawaziri wa Umoja wa nchi za Afrika (OAU).

Ulifanyika nchini Cairo Misri, ambapo katika mkutano huo, baraza la mawaziri, lilipendekeza kuanzishwa kwa siku ya maalum ya mtoto wa Afrika.

Ukitaka kuiweka haki na ustawi wa watoto, kwenye ajenda ya kisiasa, kiutamaduni na kijamii barani Afrika.

Ndipo hapo, ilipozaliwa Juni16 ya kila mwaka, iwe ni siku ya mtoto wa Afrika, kutokana na tukio la kusikitisha lililotokea mwaka 1976, Soweto nchini Afrika Kusini.

 Siku hiyo, taarifa zinaeleza kuwa, maelfu ya wanafunzi wa skuli za upili, walijitokeza kuandamana kupinga ubaguzi wa rangi katika elimu.

Kisha Jeshi la Polisi nchini humo, liliwakabili kwa ukatili, na maandamano hayo, yalisababisha vifo vya watoto wengi.

 Tukio hilo lilikuwa ni ishara na azma ya kupigania haki na ustawi wa watoto barani Afrika, na tarehe hiyo ikachukuliwa kama ishara ya kutambua mapambano yao.



Sasa kupitia siku ya mtoto wa Afrika, serikali, mashirika ya kijamii, na wadau wingine, wanajitahidi kuongeza ufahamu juu ya masuala yanayowakabili watoto barani Afrika.

 

Zanzibar nayo kama sehemu ya duniani, kila mwaka tarehe 16 Juni, huugana na nchi nyingine za Afrika, kuadhimisha siku hiyo.

 

Ambapo chimbuko la maadhimisho haya, ni Azimio lililopitishwa na uliokuwa Umoja wa nchi huru za Afrika (OAU) mwaka 1990.

Kwa lengo la kuwakumbuka watoto wa kitongoji cha Soweto nchini Afrika ya Kusini, waliouawa tarehe 16 Juni, 1976 kutokana na ubaguzi wa rangi.

Watoto hao, walikuwa wakidai haki zao za kutobaguliwa, pamoja na haki nyingine za kibinadamu, ikiwemo haki ya kupata elimu bora.

Leo Zanzibar, tukiadhimisha siku ya mtoto wa Afrika, ikiwa ni miaka 46 imeshapita, bado kundi kundi la watoto wa kike hasa wenye ulemavu, wanaendelea kunyima haki zao.

 

Maana Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, anasema watoto wa kike wenye ulemavu, wanayohaki ya kupewa uhuru wa kucheza, michezo waipendayo.

 

‘’Kwa mfano watoto wa kike wenye ulemavu, huwaoni wakicheza michezo ambayo wanaweza kuibuliwa vipaji na kisha kujiajiri, jambo linalokumbusha mateso ya Soweto,’’anasema.

 

Khalfan Amour Mohamed, Mratibu wa Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili, anasema bado mateso ya Soweto, yapo ndani ya jamii, kwa kule kuwafungia watoto wenye ulemavu wa akili ndani.

 

Wakati Zanzibar, ikiungana na matifa mingine, katika kuadhimisha siku ya mtoto wa Afrika, ni lazima minyororo iliyofungiwa watoto wa kike wenye ulemavu,  ili wasishiriki michezo waipendayo, ikatwe.

 

‘’Leo watoto wa kike wenye ulemavu huwaoni kwenye michezo ya riadha, kuogelea, kuendesha baiskeli, mpira wa kikapu, mikono na wamefungiwa ndani,’’anasema.

 

Mratibu wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Fat-hya Mussa Said, anasema bado watoto wa kike wenye ulemavu, hawajatekelezewa haki zao.

 


‘’Badhi ya nchi tena za Afrika, unawakuta wanashirikishwa kwenye michezo kama ya mpira wa mikono, meza, kikapu, riadha na kurusha tufe, lakini hapa kwetu wamefungiwa,’’analalamika.

 

Anasema pamoja na ujio wa mradi maalum ambao utawawezesha waandishi kuibua changamoto hizo, lakini jamii iamke na iwashirikishe watoto wa kile, katika michezo waipendayo.

 

Mrajisi wa vyama vya michezo Zanzibar Abubakar Mohamed Lunda, anasema, pamoja na kutokuwepo kwa mipango thabiti kwa watoto wa kike wenye ulemavu kushiriki michezo, lakini ndani ya jamii hakuna uwelewa.

‘’Leo tunasherehekea siku ya mtoto wa Afrika, lakini hatuna miundombinu imara ya mtoto wa kike mwenye ulemavu kushirikia michezo’,’alinukuliwa akisema.

 

Afisa Mradi wa kukuza usawa wa kijinsia na ujumuishi kwenye michezo, Khairat Haji anasema  Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania-TAMWA- Zanzibar, anasema wameona ipo haja ya kushirikiana  na vyombo vya habari, kuibua changamotio za aina hiyo.

‘’Lengo ni kuondoa mifume dume na yale mawazo mgando ambayo ni vikwazo dhidi ya wanawake kushiriki katika michezo, kupitia mradi wa michezo kwa maendeleo unaodhaminiwa na shirika la Ujerumani (GIZ),’’anasema.

 

WAZAZI

Khadiha Omar Haji wa Wawi, anakiri kuwa, kutokana na miundombinui kutokuwa rafiki, ni kweli wanalazimika kuwafungia ndani watoto wa kike kutoshiriki michezo.

‘’Kwanza huoni hata viwanja kwa ajili yao, vifaa ghali, uwelewa baadhi ya wazazi uko chini, haya yanachangia kudidimiza vipaji vyao,’’anasema.

 

Khamis Shehe Khamis wa Madungu, anasema watoto wa kike na hasa wenye ulemavu, imekuwa ni shida kuwashirikisha kwenye michezo, kutokana na mazingira.

 

‘’Kwanza hakuna viwanja ambavyo ni rafiki kwao, lakini ushajiishaji serikalini haupo wa kutosha, sasa haya yanachangia waendelee kukaa ndani,’’anasema.

 

WATOTO WENYEWE

Asma Maulid Khamis wa Mtoni Chake chake, anasema taasisi za michezo hazijakuwa tayari kuwatoa nje, kwa ajili ya kushiriki michezo waipendayo.

 

‘’Mbona kuna ligi ya mpira wa miguu, kikapo, mikono lakini hakuna hata mchezo mmoja, uliosajiliwa na kutangaazwa kwa ajili ya wanawake wenye ulemavu,’’anaeleza.

 

Khadija Rashid Issa wa Kengeja Mkoani, anasema jamii sio ya kulaumiwa kwa wao kutoshirikishwa michezo, bali sera na mikakati iliyopo imewatenga.

 

‘’Kuanzia skuli hadi vyuo vikuu, lazima ushirikishwaji nzuri kwetu sisi wanawake wenye ulemavu kushiriki michezo, sasa familia inatumaliza tu,’’anaeleza.

 

WIZARA HUSIKA YA MICHEZO

Kaimu Mratib wa Idara ya Utamaduni na Michezo Pemba, Khamis Hamad Juma, anasema haijawahi kutokeza hata mwaka mmoja, kuwepo kwa mashindano maalum ya mchezo wa aina yoyote kwa watoto wa kike wenye ulemavu.

 

‘’Hata bonanza la michezo ambalo ni maalum kwa ajili ya watoto wa kike wenye ulemavu, sijawahi kuliona wala kusikia,’’anafafanua.

Baraza limevisaidia vyama vitatu (3) vya michezo ya watu wenye ulemavu, katika kuandaa na kushiriki mashindano kadhaa, yakiwemo taifa ya michezo ya watu wenye ulemavu wa akili yaliyofanyika mwaka 20202.

Hayo yamefahamika wakati Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Tabia Maulid Mwita, akisoma bajeti ya mwaka wa fedha 2022/2023.

 

Akasema Zanzibar, ilifanikiwa kupata medali 20 zikiwemo dhahabu nane, fedha moja, na shaba11, katika michezo tofauti, kupitia timu za watu wetu wenye ulemavu wa akili.

Waziri Tabia anasema, kwenye michezo ya watu wenye ulemavu wa mguu na mkono mmoja, wizara imelisaidia Shirikisho la mchezo huo, na kushiriki mashindano ya kitaifa yaliyofanyika Arusha.

 

Lakini pia shirikisho la michezo ya viziwi Zanzibar (SHIMIVIZA), anasema limesaidiwa kuandaa bonanza kwa ajili ya shamra shamra ya kuadhimisha siku ya viziwi duniani.

 

Katika eneo jingine, moja ya vipaumbele vya mwaka wa fedha wa 2023/2024, ilikuwa ni kuimarisha na kuendeleza miundombinu ya michezo, kwa kufanya ukarabati mkubwa wa uwanja wa michezo wa Amaan na Gombani na kujenga viwanja vya michezo vya kisasa kwa kila wilaya.

 

                 Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan