Skip to main content

USHIRIKA 'JAMBO NIA' MFIKIWA KUVUNA 'MAHELA' KWA UVUNAJI ASALI

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAUSHIRIKA wa ‘jambo nia’ wa kijiji cha Fuuweni shehia ya Mfikiwa wilaya ya Chake chake, wanaojishughulisha na ufugaji wa nyuki, wamesema wanategemea, kujiingizia wastani wa shilingi milioni 1.6, ikiwa mizinga yao 13, itazalisha chupa 65 za asali.

Walisema, fedha hizo wanategemeza kuzipata, miezi minne ijayo kutoka sasa, kupitia mzinga yao 13 walioitega mwaka jana.

Walieleza kuwa, fedha hizo zitatokana na kuuza chupa 65, wastani wa shilingi 25,000 hadi 30,000 kwa chupa moja, yenye ujazo wa lita moja.

Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kijijini hapo, walisema waliamua kuanzisha kilimo cha nyuki, kwa malengo kadhaa, ikiwemo kujipatia kipato na kuhifadhi mazingira.

Walieleza kuwa, kupitia mizinga hiyo 13, kama hakutavuna upepo mkali ukiambatana na mvua, wanategemea kila mzingia, kuvuna chupa tano, na kujipatia chupa 65 kwa mizinga yote.




Mwenyekiti wa ushirika huo Hassein Khamis Salum, alisema wazo hilo, lilikuja kuanzia mwaka 2022, baada ya fedha zao za hisa kukua.

Alieleza kuwa, kutokana idadi ya wanachama wao 23, walikuwa na uwezo wa kukusanya shilingi 506,000 kwa mwezi na kujikuta wanatimiza zaidi ya shilingi milioni 6, kwa mwaka na kuamua kuanzisha mradi wa huo.

‘’Ilipofika mwisho wa mwaka tuliamua tusigawe, bali tukopeshane, ingawa wastan wa shilingi 700,000 tulielekeza kwenye ufugaji ya nyuki, na ndio hizo tunatarajia zikazae shilingi milioni 1.6,’’alieleza.

Kwa upande wake Msaidizi Katibu wa ushirika huo Salim Msellem Salum, alisema huku hisa inaendelea na ufugaji nyuki ukiendelea, kwa lengo la kujisaidia maisha.

‘’Tumeshaona kuwa serikalini ajira hazitosehelezi, na ndio maana tukamua kuunda ushirika huu, ili kujiwekea hisa na kisha kukopeshana, na kuanzisha mradi wa ufugaji nyuki,’’alieleza.

Alieleza kuwa, malengo yao ya baadae ni kuangalia uwezekano kwa wanachama wao 23, waweze kujiajiri na kisha nao kuwaajiri wingine.




Mwanachama wa ushirika huo Ali Thabiti Ali, alisema tokea aingie kwenye ushirika huo, manufaa makubwa anayaona na kuwa na sehemu ya uhakika ya kukopa.

‘’Kabla sijaingia kwenye ushirika wetu wa ‘jambo nia’ sikua na uhakika wapi naweza kukopa kati ya shilingi 200,000 hadi shilingi 300,000 lakini sasa nnapo,’’alieleza.

Hata hivyo wanaushirika hao, wamewaomba wafadhili kuangalia uwezekano wa kuwapa mafunzo na mbinu zaidi za ufugaji nyuki, na kuongezewa idadi ya mizinga.

Sheha wa Mfikiwa Bimkubwa Rajab Tangwi, alisema amekuwa bega kwa bega kwa ushirika huo, ili kuhakikisha anawasaidia, ikiwemo upatikanaji mikopo.

 ‘’Miongoni mwa ushirika ambao unafanyakazi kwa bidii na kwa malengo ni huu wa ‘jambo nia’, hivyo nimeshausaidia mambo kadhaa ikiwemo mafunzo na kuwaunganisha na wataalamu,’’alifafanua.

Baadhi ya wananchi wa shehia hiyo, walisema vijana hao wamekuwa mstari wa mbele, kufanyakazi kwa bidii na malengo.




Waziri wa Nchi Afisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Sharif Ali Sharif, wakati akiwasilisha hutuba ya bajeti ya mwaka 2024/2025, alisema serikali, inaimarisha sekta ya ushirika, ili kuleta ufanisi wa kutoa ajira, kunyanyua pato la mwananchi na uchumi wa nchi.

Sekta hiyo inashajiisha uundaji wa vyama vya ushirika, kwa lengo la kuwaweka pamoja, ili kupata huduma kadhaa, ikiwemo mafunzo ya ujuzi na mitaji.

Ndio maana, alieleza kwa mwaka wa fedha 2023/2024 wizara imesajili vyama vya ushirika1, 560 ikilinganishwa na vyama 1,822 kwa mwaka 2022/2023.

Waziri Sharif anasema, wamepiga hatua katika utoaji wa mafunzo kwa wajasiriamali, katika maeneo ya ufugaji wa nyuki, usarifu wa matunda na mboga, utengenezaji wa vifaa vya sola, masoko, ujasiriamali na mafunzo ya uokaji.

Hili linatajwa kuongezeka kutoka wajasiriamali 1,239 kwa mwaka 2022/2023 hadi kufikia 3,979, ambapo Unguja ni 1963 na Pemba 2,016, kwa mwaka 2023/2024.

               Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan