Skip to main content

PACSO, YAJENGA DARAJA KWA WAANDISHI, WANAASASI PEMBA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WAANDISHI wa habari na wana asasi za kiraia Pemba, wametakiwa kufanyakazi kama mwili mmoja, ili wanapofuatilia kero za wananchi, iwe kazi rahisi kuzipatia ufumbuzi.

 

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ Mohamed Najim Omar, wakati akiufungua mkutano wa siku moja, kwa waandishi hao wa habari na wanaasasi za kiraia Pemba, mkutano uliofanyika leo Juni 21, 2024 ukumbi wa Maktba Chake chake.

 

Alisema, waandishi wa habari na wanaasasi za kiraia, imegundulika wote wanawatetea wananchi wanaokabiliwa na changamoto, mfano ya ukosefu wa barabara, hivyo ni vyema wakashirikiana katika hilo.

 


Katika hatua nyingine Najim, alisema ushirikiano kati ya pande mbili hizo, unaweza hata kubadilisha sera na sheria, ambazo zinaonekana kupitwa na wakati, katika uendeshaji wa shughuli zao.

 

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa ‘PACSO’ Sifuni Ali Haji, alisema anategemea baada ya kumalizika kwa mradi huo, kuweko na mabadiliko makubwa ndani ya jamii.

 


‘’Kwa mfano kundi la wanawake na watoto, limekuwa likikumbwa na majanga mbali mbali na kisha hukosa haki zao, hivyo ushirikiano wa waandishi wa habari na wanaasasi unaweza kusaidia,’’alieleza.

 

Akiwasilisha mada ya umuhimu wa ushirikiano kati ya waandishi wahabari na wanaasasi za kiraia, Afisa Mawasiliano wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba Gaspery Charles, alisema lazima kila mmoja ajue kuwa anategemewa na mwenzake.

 




Alieleza kuwa, waandishi wa habari moja ya vyanzo vyao ni wanaasasi, kama ilivyo kwao, kwamba hawawezi kufanikiwa pasi na kuvitumia vyombo vya habari.

 

Wakichangia mada kwenye mkutano huo, washiriki hao walisema, wamepata uwelewa na njia za kushirikiana na waandishi wa habari, katika kazi zao.

 

Khadija Sultan, alisema kilichobakia sasa baada ya mkutano huo, ni kukaa pamoja na vyombo vya habari, ili sasa kushirikiana katika kazi zao.



 


Mwandishi wa ZBC Khadija Kombo, Is-haka Mohamed wa ZENJ FM na Khadija Ahmed wa Redio jamii Mkoani, walisema, umoja na mshikamano unaweza kufanikisha kila kitu.

 

Walieleza kuwa, baada ya mafunzo hayo, watazidisha ushirikiano kati yao na wanaasasi za kiraia, kwa ajili ya kuyaripoti maono na changamoto zao.

 

Akiufunga mkutano huo, Mwenyekiti wa PACSO Mohamed Ali Khamis, alisema atafurahi kama maazimio sita yalioibuliwa hapo, yatafanyiwa kazi.

 

Alieleza kuwa, wazo la kufuatilia ahadi za ujenzi wa barabara ya Chake chake- Mkoani, vitendo vya udhalilishaji, mporomoko wa maadili, dawa za kulevya na uharibifu wa msitu wa Ngezi ni maeneo ya kuwekewa mkazo.

 

 Mkutano huo, ni sehemu ya utekelezaji wa mradi wa ‘uraia wetu’ unaotekelezwa na ‘PACSO’ kwa muda wa miaka minne, kwa ufadhili wa The Foundation For Civil Society kupitia Umoja wa Nchi za Ulaya ‘EU.’

                  Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

…….SUZA WATOA USHAURI WA ADHABU YA KUNYONGWA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WANAFUNZI wanaosomea uwalimu Chuo cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ kampasi ya Benjamin Wiliam Mkapa Wete Pemba, wamependekeza adhabu ya kunyongwa hadi kufa, kwa mtu atakaetiwa hatiani, kwa kosa la dawa za kulevya. Walisema, haiingii akili kuona, mahkama imeshamtia hatiani mtu kwa kukutwa na dawa za kulevya, ambazo huathiri nguvu kazi ya taifa na kisha, kupewa hukumu ya kifungo pekee. Wakizungumza leo Juni 26, 2024 kwenye kongamano la vyuo vikuu, juu ya masuala ya msaada wa kisheria, kuelekea wiki ya msaada wa kisheria Zanzibar, lililofanyika Chuoni hapo, walisema wakati umefika sasa kutolewa kwa hukumu hiyo. Walipendekeza kuwa, ni vyema kwa mtu anayetiwa hatiani asibakie chuo cha Mafunzo pekee kuitia tena hasara serikali kwa chakula na wakati mwingine matibabu, wakati tayari ameshasababisha madhara, kwa vijana. Mshiriki Juma Nafasi Juma, alifafanua kuwa kama mtu ameamua kuliumiza taifa kwa kuingiza, kusafirisha, kusambaaza dawa za kulevya, hivyo ni vy

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan