Skip to main content

''MKIENDELEA KUWAFICHA, KUWATENGA WATU WENYE ULEMAVU WA AKILI MNAZIDI KUWAFUBAZA''

 

 


NA MWANDISHI WETU, PEMBA@@@@

JAMII imetakiwa kuendelea kuwasimamia na kuwapatia huduma stahiki ndugu zao ambao wamejaaliwa kuwa ni walemavu wa akili, kwani kuwatenga na kuwaficha kutazidi kuwafubaza kifkira na kimakuzi.

 

Wito huo umetolewa na Afisa Mdhamini Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Ahmed Abuubakar alipokuwa akizungumza na wazazi na walezi, wenye watoto wenye ulemavu wa akili na wananchi, waliohudhiria katika ftari ya pamoja iliyofanyika Tibirinzi Kiwanja cha Kufurahishia watoto wilaya ya Chake chake.

 


Alisema licha ya kujaliwa kuwa na ulemavu wa akili lakini, watu wa kundi hilo wanakuwa na mitazamo mizuri pale wanapokuwa hawatengwi na familia, au jamii kwa kuweza kushirikishwa katika mambo tofauti.

 

Mdhamini huyo alilisisitiza, umuhimu wa kuwatoa watoto na watu wenye ulemavu kujumuika na kupatiwa haki zao mbali mbali ikiwemo elimu, afya pamoja na kuweka mazingira ya kujichanganya na wenzao.

 

Hata hivyo amesifu mwamko wa wazazi na walezi wa kuwasimamia vyema vijana wao, wenye ulemavu wa akili kwani kwa juhudi hizo za kuwasimamia na kuwa nao karibu kwa kuwashirikisha kwa sasa imekuwa nadra kuwakuta watu hao.

 Katika hatua nyengine Afisa Mdhamini huyo, ameipongeza jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar, ZAPDD kwa hatua ya kuwaweka pamoja watu wanye ulemavu wa akili katika futari hiyo.

 

Aidha Mdhamini huyo amesema Ofisi ya Makumu wa Kwanza wa Rais ambayo ndiyo yenye dhima ya kusimamia watu wenye ulemavu Zazniabar, itasimamia na kupigania upatikanaji wa maslahi ya watu wenye ulemavu kwa wakati.

 

Naye Mjumbe wa Kamati Kuu ya Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili Zanzibar ‘ZAPDD’ Mkubwa Ahmed Omar amesema kuwa walikuwa na utaratibu wa kuandaa futari kwa wanachama wao kwa ngazi ya mkoa, ingawa kwa mwaka huu wameamua kuwakutanisha kwa pamoja.

 

Amewaomba wadau kuwa mstari wa mbele katika kutetea haki za watu wenye ulemavu, pamoja na kuwashirikisha katika shughuli mbali mbali za kijamii na wasiwachukulie kama ni watu wa kichekesho au kiburudisho.

 

Kwa upande wake Mratibu wa Ofisi ya Mufti Pemba Sheikh Said Ahmad Mohamed, amesema jamii haipaswi kuwatesa watu wenye ulemavu wa akili, kutokana na hali zao kwani ni matakwa ya Muumba mwenyewe.

 


Aidha Shekh Said ameahidi kushirikiana na watu wenye ulemavu wa ajili na makundi mengine ya watu hao, na kusema milango ya Ofisi ya Mufti Pemba ipo wazi wakati wote kwa ajili ya kushikiana nao.

 

Mapema Mratibu wa Jumuiya ya Watu wenye ulemavu wa akili Pemba Khalfan Amour Mohamed amewashukuru wadau mbali mbali waliofanikisha ftari hiyo sambamba na kuwaomba kutosita kuwaunga mkono pale watakapokuwa na uhitaji.

 


Aidha amemwomba Ofisa Mdhamini Ofisi  ya Makamu wa Kwanza wa Rais kuendelea kuwapa ushirikiano zaidi  katika  kuzitatua na changamoto na kutetea haki za watu wenye ulemavu.

       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch