Skip to main content

BIASHARA YA BODABODA ENEO JIPYA LA AJIRA VIJANA PEMBA

 




NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

“TULIKUWA tunazurura ovyo mitaani, kukaa vijiweni, hali ambayo ingeweza kuhatarisha maisha yetu, kwani tungejiingiza katika makundi hatarishi na hatimae jela, lakini kwa sasa tupo busy kutafuta pesa”, …hayo ni maneno ya baadhi ya vijana waliokabidhiwa mkopo wa bodaboda Wilaya ya Chake Chake Pemba.

Vijana hao waliopatiwa mkopo wa bodaboda na Serikali kupitia benki ya CRDB kwa lengo la kuwainua kiuchumi, ambapo kwa sasa wameimarisha maisha yao kupitia ajira hiyo.

Ali Issa Ali mwedesha bodaboda anasema, uendeshaji wa huo wa bodaboda umempa mafanikio kwa sababu kabla ya kupata mkopo huo alikuwa na maisha duni kiasi ambacho alikuwa hajui atapata wapi kazi ya kuendesha maisha yake.

“Ilikuwa sina kazi hata moja, kazi yangu kubwa ni kuzurura tu mitaani, lakini kwa sasa nashkuru nimejiajiri na napata pesa ya kujikimu kimaisha, Dk. Mwinyi amefanya kitu cha muhimu kwetu vijana, tunampongeza”, anaeleza.

Anasema, kipato anachopata kutokana na uendeshaji wa bodaboda unakidhi mahitaji yake ni tofauti kabisa na kukaa nyumbani bila ya kazi yeyote.

Kijana ambaye hakutaka jina lake litajwe anaeleza kuwa, wamenufaika sana na mkopo huo kwani vijana wengi wamejiepusha na madawa ya kulevya pamoja na uzururaji usio na maana.

“Muda wote vijana wapo kazini, hawana muda wa kukaa vijiweni kufanya mambo yasiyofaa, tunamshukuru Rais wetu kwa kutuwezesha kupata hizi bodaboda, kwa sababu zamani tajiiri alikuwa anataka kila siku 10,000 lakini kwa sasa anataka 8000”, anasema.    

Ali Mohamed Juma anasema, amenufaika sana kwa biashara hiyo ya bodaboda kwani ameweza kuwasomesha watoto wake ambao anaamini wakipata elimu itakuwa tegemeo la maisha yao ya baadae kwa kuwa elimu ndio ufunguo wa maisha.

Anasema kuwa, kwa siku anaweza kupata zaidi ya elfu 50, hivyo anapata kiasi cha kukidhi mahitaji yake kwa siku, ingawa sio kingi lakini amepiga hatua kubwa kimaisha tofauti na mwanzo.

“Inategemea na abiria wenyewe lakini tunashukuru kupata mkopo huu, kwani umetutoa katika hali duni tuliyokuwa nayo kipindi cha nyuma, kwa kweli hakuna kupata kudogo”, anaeleza.

Mohamed Nassor Mohamed anasema, wamenufaika na mkopo wa bodaboda waliopewa na Rais kwani wameondokana na dimbwi la umasikini, kukaa ovyo bila ya kazi yeyote na kupungua kuitwa wizi.

“Kwa sasa nahudumia familia yangu kwa kile ninachokipata, tunapata kiasi si kama kukaa tu na kusubiri wazee watulishe, hii ni faraja kubwa kwetu”, anaeleza. 

Hamad Maulid Suleiman anaeleza kuwa mkopo huo umewanufaisha sana kutokana na vijana wengi walikuwa hawana kazi, lakini kwa sasa wamejiajiri kupitia bodaboda na maisha yanakwenda vizuri.

“Sasa tupemapata ajira, tulikuwa vijana wa maskani tu hatujui tufanye kitu gani ili kupambana na maisha lakini tunaishukuru Serikali hii ya awamu ya nane kwa kutuona sisi vijana na kututafutia ajira”, anaeleza.

Anafafanua kuwa, wakati wa kampeni yake Dk. Mwinyi aliahidi ajira laki tatu kwa wananchi wakiwemo vijana na wameliona hilo kwa sababu vijana wamepata mikopo ya bodaboda na wengine wamepata mikopo ya kuwawezesha katika vikundi vyao vya ujasiriamali.

“Kwa kweli Rais wetu amaejitahidi sana kwa hili, kinyume chake vijana wengi tungepotea njia kwa kujiingiza katika makundi maovu na hatimae kuishia jela”, anasema.

Mwenyekiti wa bodaboda ambazo zina leseni Seif Hamad Said anaeleza, mafanikio wanayopata kuwa ni mazuri kwani vijana ambao wengi hawana kazi wapepata biashara ya kuendesha bodaboda, ambapo kwa sana wana uhakika wa kupata milo mitatu kwa siku.

“Kuna vijana walikuwa wameanza kujiingiza katika vitendo vya wizi, uvutaji bangi na mambo mengine mabaya lakini kupitia mkopo huo umefanya yote hayo wayaache na watafute fedha za halali za kujikimu kimaisha”, aneleza.

Kwa mujibu wa taarifa za Mkoa wa Kusini Pemba za mwaka 2022 kuna jumla ya bodaboda 145 walizopewa vijana kwa mkopo, kati ya hizo bodaboda 100 zinatoka Wilaya ya Chake Chake na 45 kutoka Wilaya ya Mkoani.

Mathalani Wilaya ya Chake Chake, yenye bodaboda 100 ikiwa kila dereva moja atakuwa na familia isiyopungua ya watu watatu basi wastani wa watu 300 watakuwa ni wanufaika na uchumi unaotokana na bodaboda hizo kila siku.



CHAGAMOTO ZINAZOWAKABILI VIJANA HAO

Mwendesha bodaboda Hussein Saleh Khamis anaeleza kwamba, pamoja na kunufaika sana na mkopo huo, lakini wanakabiliwa na changamoto ya urejeshaji wa mkopo kwani watu wa benki hawajui kuumwa wala kukosa pesa, wanachojua wao ni kulipwa pesa zao tu kila siku.

“Tunajitahidi kadiri ya uwezo wetu kulipa, lakini wakati mwengine mtu hajaweza kutoka kwa kuumwa ila kila siku anatakiwa arejeshe shilingi 8000, jambo ambalo ikiwa unaumwa ni ngumu kuipata, kwa sababu hata kuendesha mtu mwengine hawaruhusu”, anaeleza.

Anasema kuwa, Dk. Mwinyi aliwapa muda wa mwaka mmoja na nusu kurejesha mkopo hiyo, ingawa ikifika mwezi hujalipa wanazichukua bodaboda, jambo ambalo linawanyima amani.

Anafafanua kuwa, angalau wangesubiri kijana aliefika miezi mitatu mpaka sita ikiwa hajalipa au hajafikia hata nusu ya kiwango kilichowekwa, ndipo waichukue bodaboda hiyo.

“Ikiwa amekwama wiki mbili mpaka mwezi kwanza afuatiliwe na kuangaliwa hali yake anaendeleaje? Na sio kuchukua maamuzi ya kuichukua pikipiki tu, pengine mtu ni mgonjwa, ataitoa wapi pesa?”, anasema.

Mohamed Nassor Mohameda anaeleza kuwa, changamoto ni kutokuwa na amani wanapokuwa barabarani kwa sababu, walipopewa mkopo waliambiwa kuwa hawatakuwa na shida yeyote kwani itakuwa na bima kamili na vitu vyote vimekamilika kweli, ingawa askari wamekuwa wakiwasumbua muda wote.

“Kwenye urejeshaji wa mikopo sijapata usumbufu wowote, lakini wenzangu nawasikia wanasema, wanapochelewesha kupeleka pesa wastani wa siku moja, mbili basi wanapokonywa pikipiki na wanaziweka mpaka utakapokwenda kulipa, hii inazorotesha maendeleo yao kwa kweli”, anasema.

 “Vikoti tulipewa siku tuliopokabidhiwa pikipiki, lakini kinachotushangaza sasa hivi tunaambiwa tununue vikoti vyengine ambavyo vinauzwa shilingi 25,000, hii inazorotesha maisha yetu, kila siku watu waibue mbinu mpya ya kututoza pesa tu kiholela”, anasema dereva Hamad Maulid Suleiman.

NINI KIFANYIKE ILI KUBORESHA ZAIDI

Huessein Ali Khatib anasema, Serikali iangalie katika utendaji wao wa kazi katika urejeshai wa mikopo kwa sababu biashara ni ngumu kutokana na hali ya mzunguko wa watu kisiwani hapa kuwa ni mdogo huku wana familia zinawategemea.

“Siku nyengine chombo kinahitaji matengenezo kwa hiyo lazima uweke pesa ya hakiba kwani ni sawa na mtoto inahitaji kulishwa, kwa hiyo watufanyie ahueni kidogo”, anasema.

 Mohamed Nassor Mohamed anasema, kuna mambo ambayo hayafuati utaratibu, kwa sababu kuna ajenda ya kikoti lakini wanatakiwa kupewa wale waliokamilisha usajili, ingawa kwa sasa anapewa yeyote, jambo ambalo linawaumiza wao ambao wameshafuata taratibu zote. 

WANANCHI/ABIRIA 

Hafsa Ali Said anasema, jambo alilolifanya Dk. Mwinyi ni la maana sana kwa sababu amewatoa vijana katika dimbwi la matatizo na kuwapeleka katika mwanga, hivyo vijana waendelee kuzitumia fursa hizo kwa lengo la kujikwamua kiuchumi.

“Vijana wengi siku hizi wanaendesha bodaboda na bajaji, wamepunguza uzururaji, hivyo Serikali iendelee kuwawezesha vijana kwa kuwapa mitaji itakayowasaidia katika maisha yao ya kila siku”, anasema.

Fatma Ali Yussuf anasema, usafiri wa bodaboda umewarahisishia safari zao, kwani hata unapokweda sehemu zisizofika gari wao wanafika, wanajivunia kwa kweli.

“Zamani mtu anakuwa na mzigo, anapokwenda daladala hazifiki, tulikuwa tunapata usumbufu kwa sababu hupati hata mtu wa kukupelekea mzigo, lakini kwa sasa maisha yamekuwa rahisi mno kwa usafiri wa bodaboda.

Suleiman Khamis Ali anawataka waendesha bodaboda kupunguza mwendo wakati wanapokuwa barabarani, ili kuepusha ajali zinazoweza kuepukika.




SERIKALI YA WILAYA 

Khatibu Juma Mjaja ambae anakaimu Wilaya ya Chake Chake anasema kuwa, Serikali imekuja na mikakati tofauti kuhakikisha inaondoa tatizo la ajira kwa wananchi wake, ikiwa ni pamoja na kutoa mikopo kwa wajasiriamali.

‘’Boda boda zilikuwepo ingawa hazikuwa nyingi, lakini Serikali imewekeza kwa kuwapatia vijana bodaboda za mkopo kwa lengo la kupata ajira, wajitegemee na waweze kujikwamua kimaisha’’, anaefahamisha.

Anaelezea mafanikio yaliyopatikana kuwa ni vijana kujiajiri, kuoa na kuweza kuhudumia familia zao, kupunguza kukaa vijiweni hali iliyosaidia kutokujiingiza katika makundi hatarishi.

‘’Kuna vijana walishindwa kuoa kutokana na kukosa ajira, lakini baada ya kupewa bodaboda hizo za mkopo, wameoa na sasa wanahudumia familia zao, kwa kweli ni faraja kwetu’’, anasema.



Mkuu huyo wa Wilaya anawataka vijana hao kufanya kazi kwa bidii na warejeshe mikopo kwa wakati, ili na vijana wengine wapatiwe mkopo huo kwa lengo la kujikomboa na umasikini.

Anasema kuwa, hiyo ni fursa kubwa kwa vijana katika kukuza uchumi wao, hivyo wanatakiwa wazalishe bodaboda nyingine kwa ajili ya kutoa fursa ya ajira kwa wengine au kuzalisha mradi mwengine wowote ambao utamsaidia katika maisha yake.

‘’Nawambia vijana kuwa hiyo ni fursa kwao, waitumie vizuri kwa ajili ya kuzalisha na sio kusababisha ajali ambazo zinaleta maafa kwa taifa letu na tusizitumie kwa kufanya uhalifu kwani lengo la Serikali ni kuwakwamua kiuchumi’’, anaeleza Mkuu huyo.

Kwa mujibu wa utafiti uliofanyika mwaka 2020/2021 Zanzibar, katika Bajeti ya Wizara ya Nchi Ofisi ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji imeeleza kuwa, vijana wenye uwezo wa kufanyakazi ni kati ya miaka 15 hadi 35, huku ukosefu wa ajira ukiongezeka.

Ukosefu wa ajira umeongezeka kutoka asilimia 24.6 ya mwaka 2014/2015 hadi kufikia asilimia 27.6 ya mwaka 2020/2021, ambapo wathirika wa kubwa ni vijana ambao ndio nguvu kazi ya Zanzibar.

Kipato cha nchi hakiwezi kutosheleza kuwaajiri vijana wote, hata hivyo kwa mujibu wa mpango wa maendeleo wa mwaka 2021-2026, wanatarajia ukosefu wa ajira  kupungua na kufikia asilimia 10 ifikapo mwaka 2026, kutokana na miradi mipya na inayoendelea.

Kila boda boda moja ina thamani ya shilingi milioni 3,700,000 ambapo vijana waliopata mkopo wa bodaboda hizo wanatakiwa kulipa kwa muda wa mwaka mmoja na nusu.

                                                 MWISHO 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch