Skip to main content

KAMISHNA POLISI ZANZIBAR AKEMEA WANAOJICHUKULIA SHERIA MIKONONI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KAMISHNA wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad, amesikitishwa na tabia ya watanzania, kuendelea kujichukulia sheria mikononi, jambo ambalo wakati mwengine husababisha vifo kwa watuhumiwa.

Alisema, tabia hiyo sio mwenendo mzuri kwa watanzania, kwani serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanania na ile ya Zanzibar, zimeanzisha vyombo maalum, vya kushughulikia jinai na madai.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa njia simu, alisema zipo mahakama mbali mbali, jeshi la Polisi, ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka na ofisi za wapelelezi, ambazo zimewekwa kazi hiyo.

Alieleza kuwa, sheria zinaelekeza wazi wazi mara baada ya jamii kumshutumu mtu kutenda kosa, liwe la jinai ama madai, ni kumlalamikia katika vyombo vya sheria, lakini sio kujichukulia sheria mikononi.

Kamishna huyo alisema, anakerwa mno na jamii kuendelea kuwaondoshea uhai watuhumiwa wa makosa mbali mbali, kwani kazi ya kutoa hukumu, imepewa mahakama.

‘’Utamaduni wa kila mtuhumiwa kuuawa sio wa watanzania, kwani zipo taratibu za kisheria, tena maarufu ambazo, mtuhumiwa hutakiwa kuripotiwa na sio kushambuliwa,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Kamishna huyo wa Jeshi la Polisi Zanzibar Hamad Khamis Hamad, alisema hata mtuhumiwa awe na kosa kubwa kiasi gani, ana haki zake kutokana na ubinaadamu wake.

‘’Kwa mfano kuna haki ya kuhojiwa, kusikilizwa, kupewa dhamana, kukata rufaa, kutumikia chuo cha mafunzo na hata kupata msamaha kwa baadhi ya mazingira,’’alieleza.


Aidha Kamishna huyo, ameikumbusha jamii kuendelea kuvitumia vituo vya Polisi, kuripoti matukio mbali mbali, licha ya changamoto ambazo hujitokeza.



Kwa upande wake, Jaji Mkuu wa Zanzibar Khamis Ramadhan Abdalla, amesema hakuna kinga kwa wanaowashambulia watuhumiwa, kwani kazi ya kutoa hukumu kisheria, ipo kwa mahakama.

Alieleza kuwa, jamii inapaswa kuzingatia sheria na kanuni za kijinai, ambazo zimeweka utaratibu wa kushughulikia kesi zote, hadi kufikia kutolewa uamuzi.

‘’Mifumo ya sheria imeweka utaratibu nzima wa kushughulikia haki jinai, na ukiangalia mwanzo hadi mwisho, hakuna eneo ambalo mwananchi ameruhusiwa kujichukulia sheria mikononi,’’alieleza.

Nae Mkurugenzi wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba ‘CHAPO’ Nassor Bilali Ali, alisema elimu wanayoitoa kwa jamii, hatarajii kuona mwananchi, anajichukulia sheria mikononi.

‘’CHAPO inaowasaidizi wa sheria katika shehia zote za wilaya ya Chake chake, wamekuwa wakitoa elimu juu ya utaratibu nzima wa kushughulikia haki jinai, lakini sio kujichukulia sheria mikononi,’’alifafanua.

Akizungumzia kuhusu madhara ya kujichukulia sheria mikononi, Mratibu wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Tazania ofisi ya Pemba, Suleiman Salim, alisema moja ni kuendeleza visasi.

‘’Jingine ni kupora mamlaka ya kisheria ya mahakama, ambayo ndio inayopaswa kutoa hukumu kwa mshitakiwa, lakini sio jamii husika,’’alifafanua.

Alisema jingine ni kupunguza nguvu kazi kwa wananchi, pamoja na kuiongezea gharama serikali kwa matibabu, iwapo mtuhumiwa atapata majeraha.

Mwanamke mmoja ambae muume wake aliuawa na wananchi wenye hasira mwaka 2019 eneo la Wawi wilaya ya Chake chake, alisema kama serikali haifanyi juhudi za kuwakamata waliosababisha vifo, utamaduni huo, utakuwa endelevu.

Hassan Juma Hassan wa Msingini Chake chake, alisema wananchi wamekuwa wakijichukulia sheria mikononi, kutokana na mifumo ya haki jinai, kuchelewesha utoaji wa hukumu.



‘’Inawezekana wananchi wamemkamata mtuhumiwa na kumfikisha mbele ya vyombo vya sheria na ushahidi kamili, lakini baada ya muda unaskia hana kesi ya kujibu, hapo hasira huibuka,’’analeza.

Daktari wa saikolojia ya mwanadamu Ali Yussuf wa Chake chake, alisema moja ya sababu inayowaskuma wananchi kujichukulia sheria mikononi, ni kukosa imani na vyombo vya ulinzi na usalama.

‘’Kama wamempeleka mtuhumiwa mmoja kaachia, na kisha anarejea tena kufanya makosa bila ya hatia, akili huwashawishi kujichukulia sheria mikononi,’’alifafanua.

Aliyekuwa Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema elimu ya sheria bado iko chini, kwa jamii ndio maana wanajichukulia sheria mikononi.

Ripoti ya uhalifu ya Jeshi la Polisi Tanzania ya mwaka 2020, inaonesha kuwa, wapo wananchi 124 wameshauawa, kutokana na watu kujichukulia sheria mikononi Zanzibar.

Uchunguzu umebainika, hao ni wa kipindi cha miaka 10, kati ya mwaka 2011 hadi mwaka 2020, kwa mikao mitano pekee ya Zanzibar.

Kwa idadi ya wananchi hao waliouawa, kwa tuhma za kufanya uhalifu, ni sawa na kila mwaka, wastani wa watu 13 kuuawa visiwani humo katika kipindi hicho.

Watu wao waliouawa kwa Zanzibar, Mkoa wa mjini Mgharibi Unguja, uliongozwa kwa miaka yote hiyo, na takwimu hizo haijwahi kushuka.

Imebainika kuwa, mwaka 2011, Zanzibar kuliripotiwa matukio manne (4), mkoa wa Mjini mgharibi pekee, uliripoti matukio matatu (3).

Mwaka 2015 ilikusanya matukio manane (8), mkoa wa Mjini mgharibi ukaripoti matukio matatu, ingawa mwaka 2016 kati ya matukio 21, mkoa huo uliripoti matukio 16.

Hali hiyo, ipanda juu zaidi mwaka 2017, kwa wananchi 26 kuuawa, ambapo kati yao, 18 walikuwa wa mkoa wa Mjini magharibi.

Kwa mwaka huo mikoa mingine ya iliyoripoti matukio mengi zaidi, ni mkoa wa kusini Unguja, matano (5), kusini Pemba matatu (3), na mikoa mengine kukiwa hakuna vifo vilivyoripotiwa.

Mwaka 2019, ulibeba matukio 17, ambapo matukio 12 yalikuwa mkoa wa Mjini magharibi pekee, kusini Pemba matukio mawili (2) na mikoa mengine kukiwa na idadi sawa na tukio moja moja.

Hata mwaka 2020, mkoa wa Mjini magharibi, ulikusanya matukio 10, ya mauwaji kwa wananchi kujichukulia sheria mikononi, kati ya matukio yote 15 yaliyoripotiwa.

                       Mwisho

 







Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch