Skip to main content

MBINU ZA KUWAOKOA WATOTO WANAOBAKWA PEMBA HIZI HAPA

 



NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

Serikali imetakiwa kuweka mazingira mazuri ili kuwalinda wasichana wadogo dhidi ya vitendo vya ubakaji kisiwani Pemba.

Kati ya hayo, ikiwemo kutoa elimu ya kutosha, kuwafanya wasichana wajue haki zao, kuweka ulinzi dhidi ya wanaotaka kutoa taarifa na msaada wa kisaikolojia kwa walioathirika, imeelezwa.

Mapendekezo haya yamekuja kufuatia ripoti ya uchunguzi ya gazeti hili, iliyoonyesha kwamba kesi nyingi zinazohusu kubakwa kwa mabinti wenye umri chini ya miaka 18 zinaishia njiani kwa wahusika kutochukuliwa hatua yoyote.

Pamoja na hoja hizo zinazosemwa katika jamii, bado mtoto chini ya miaka 18 ni mtoto kutokana na sheria ya Zanzibar nambari 6 ya mwaka 2011 ilivyoeleza

Jambo la kwanza ambalo wadau waliozungumza ni hili wamesisitiza ni umuhimu wa Serikali kuendelea kusisitiza kwamba kwa mujibu wa Sheria za nchi, mtoto wa kike maana yake ni mtu mwanamke mwenye umri wa chini ya miaka 18.

Mkaazi wa Shehia ya Kiungoni, Ali Haji Omar alimwambia mwandishi kwamba la muhimu ni kila mtu kujua kwamba mtu mwenye umri wa chini ya miaka 18 awe mwanamke au mwanamume, ni mtoto na elimu zaidi ya kujitambua na kujithamini inatakiwa.

Namna ya kuwasaidia watoto

Omar aliliambia gazeti hili kwamba ili kuhakikisha watoto wanaoathiriwa na vitendo hivyo wanatoa ushahidi mahakamani, wanahitaji wapewe elimu zaidi kwa sababu kwa mujibu wa Sheria za Zanzibar, mwenye umri chini ya miaka 18 bado ni mtoto.

‘’Wapewe elimu ya umuhimu wa kutoa ushahidi na athari zinazoweza kujitokeza iwapo watakataa kutoa ushahidi katika Mahakama, kwa sababu Hakimu na Mwendesha Mashitaka hawakuwepo kwenye eneo la tukio’’, anasema mwananchi huyo.

Kwa upande wake, Saade Hamad Khlfan, mkaazi wa Shehia ya Piki yeye amependekeza kuwepo utaratibu wa kushughulika na kesi hizo mara tu baada ya muathirika kuwa tayari kutoa ushahidi, kwani kuchelewa ndiko huwafanya watoto na familia kubadili mawazo.

‘’Kwa mfano unasikia leo Hakimu hayupo, kesho Mwendesha Mashitaka ana kikao, kwa hiyo katika haya tubadilike na kubwa zaidi ni kuondoa dharura ikiwa mashahidi wapo na hasa shahidi nambari moja ambae ni mtoto mwenyewe’’, anaeleza.

Mwananchi kutoka Shehia ya Piki, Fatma Kassim Issa, anaeleza kuwa Mahakama zingetengeneza mazingira mazuri hasa ya ushahidi na si kuwapeleka mashahidi nusunusu, kwani hapo ndiyo huwa mwanzo wa watoto hao kugeuka.

‘’Kwa sababu unamkuta leo mtoto amesema vizuri lakini siku zikipita anaanza kujifikiria kusema kuwa hajanifanyia huyu, kanifanyia mtu mwengine na wala siwezi kumsema, lakini ikiwa Mahakama zina mazingira mazuri upelelezi unapokamilika tu hakuna haja ya kuzikosesha haki kwa mtoto’’, anasema.

Anasema kuwa, walio wengi wamekuwa wakigeuka baada ya kukaa siku nyingi bila ushahidi kusikilizwa na ndio wengine huchukua fedha kutokana na kukaa siku nyingi, hivyo wanakosa haki zao.

Rashid Ali Khamis mkaazi wa Mzambarau Takao, anasema jambo lingine linaloweza kufanyika ni kupunguza umri wa mtoto anayelindwa kisheria, kwani inawezekana pia kwamba wale ambao umri wao umevuka miaka 15 huwa wanajielewa na kujua wanachofanya.

Kwa upande wake, mkaazi wa Shehia ya Minungwini Maryam Faki Ali anapendekeza kuwepo kwa nyumba maalumu ya kuwatunza mabinti wadogo wanaotakiwa kutoa ushahidi mahakamani, ili wahifadhiwe na wasishawishiwe kuharibu ushahidi.

‘’Wengi wao wanashawishiwa, kutishwa au kuahidiwa ndoa na ndio maana wanakuwa wanabadilisha ushahidi au hawafiki mahakamani, lakini wakihifadhiwa sehemu maalumu itakuwa ni vigumu kubadilika’’, anaeleza.



Mratibu wa TAMWA Pemba Fat-hiya Mussa Said anaeleza kuwa, waathirika wa vitendo vya ubakaji wanahitaji kupewa msaada wa kisaikolojia na kuelezwa kuwa matendo hayo waliyofanyiwa yanawaathiri kisaikolijia na wabakaji wakiachwa wataendelea kuwabaka watu wengine.

‘’Pia tuwaeleze athari zinazoweza kuwapata wao wenyewe iwapo watakataa kutoa ushahidi na vipi watakaposhindwa kutoa ushahidi itachangia watoto wengine kuendelea kudhalilishwa’’, anaeleza.

Anaeleza kuwa, watoto wenye umri huo bado hawajajielewa na ndio maana wakifikishwa mahakamani wanawalinda watuhumiwa kwa kusema kuwa ni wapenzi wao, hivyo wanahitaji elimu ya kujitambua ili wajijue wao ni nani.



‘’Na ndio maana wanashindwa kutoa ushahidi mahakamani kwa sababu watuhumia wanawaambia kuwa asipotoa ushahidi ataenda kumuoa’’, anafafanua Mratibu huyo.

Mwananchi wa shehia ya Mtambwe Kaskazini, Husna Salum Bakar, anasema elimu itasaidia kuwajenga watoto hao waweze kuwa na misimamo thabiti ya kuweza kutoa ushahidi.

Akizungumza na mwandishi, Hakimu wa Mahakama Maalumu ya Kushughulikia Kesi za Udhalilishaji Mkoa iliyopo Wete, Ali Abdulrahman Ali, anasema watoto hao wanatakiwa kuwa na elimu hasa ya kujua athari zitakazotokea endapo atajiingiza katika mapenzi ya mapema.

‘’Zipo athari nyingi zinaweza kuwatokezea watoto hao iwapo watajiingiza katika ngono za mapema, kwa hivyo wapewe elimu ya kutosha na waambiwe kuwa unapofanya hivi kuna moja, mbili, tatu litakutokea hii itawasaidia kuachana na masuala hayo’’, anaeleza.

Anataja kesi za kubaka ambazo zimefikishwa mahakamani kuanzia mwaka 2020 hadi 2021 ni 49 huku za watoto kati ya umri wa miaka 15-17 zikiwa 19, ambapo nne washtakiwa wamefungwa, mbili wametozwa faini na kesi 13 zimeondolewa (kufungwa).

Hakimu huyo anafafanua kuwa, mwaka 2021 kesi za kubaka zilizofikishwa mahakamani ni 25, miongoni mwa hizo kesi za watoto wenye miaka 15-17 ni 16, ambapo kesi 11 zimeondolewa, kesi tatu washtakiwa wamefungwa na kesi mbili washtakiwa wametozwa faini kutokana na kuwa wapo chini ya miaka 18.

“Kesi za ubakaji zilizofikishwa mahakamani mwaka 2020 ni tisa (9), kati ya hizo watoto wenye miaka 15-17 ni kesi tatu, ingawa moja tu ndio iliyopata hatia na mbili ziliondoshwa”, anafafanua.

Mratibu kutoka Jumuiya ya Wanawake wa Kiislamu Wilaya ya Wete, Asya Ibrahim, anaeleza kuwa wanawasaidia watoto hao kwa kuwapa ushauri nasaha na kuwaeleza ili wazungumze ukweli, jambo hilo litasaidia kuondosha maasi ikiwa ni pamoja na huo udhalilishaji.

‘’Kwa sababu yule ambaye atakwenda kumtolea ushahidi (mtuhumiwa) atahukumiwa na jamii itajifunza kwamba kufanya hivyo ni kosa na utakapokwenda mahakamani utachukuliwa hatua za kisheria’’, anasema.

Rashid Hassan Mshamata ambaye ni Mwenyekiti wa Mtandao wa Kupambana na Udhalilishaji anaeleza kuwa, msaada mkubwa kwa watoto hao ni kuongezwa kupewa elimu ya kujua namna gani watafanya iwapo limetokea tukio hilo.




‘’Kwa sababu ikiwa hawakupewa elimu maisha yao ya baadaye, yote yataharibika na watashindwa kutimiza malengo yao waliyojiwekea,’’ anafahamisha Mshamata.

Khadija Mohamed mkaazi wa Mzambarau Takao anasema, watoto wapewe mafunzo mbali mbali ili wajue nini wafanye na kitu gani hawapaswi kufanya kutokana na umri wao, hiyo itasaidia kwa kiasi kikubwa kuondosha vitendo hivyo katika jamii.

Kwa mujibu wa takwimu za jeshi la Polisi Wilaya Wete za mwaka 2020 zinaonyesha kesi takribani 85 za udhalilishaji i ziliripotiwa, huku kesi 30 zikiwa ni kesi za ubakaji zinazohusisha watoto kati ya mika 15-17.

Kati ya hizo kesi 30 zilizoripotiwa, ni kesi nne (4) tu ambazo zilitolewa hukumu huku 17 zikfutwa katika kituo cha Polisi, kesi saba (7) zilifutwa mahakamani na kesi mbili (2) zikiwa katika upelelezi.

Wakati mwaka 2021 kesi zilizoripotiwa zilikuwa 44, kesi 28 zikiwa za watoto wenye umri wa miaka 15-17 ambapo ni kesi nne (4) tu zilizotolewa hukumu kama mwaka 2020, huku kesi 12 zikifutwa Polisi na saba (7) mahakamani na kesi tano (5) upelelezi wake bado unaendelea.

                                                 MWISHO.    

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch