Skip to main content

KATIBU MKUU HABARI, AWAONESHA NJIA YA MAFANIKIO WAKUU WA WIZARA PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KATIBU Mkuu wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Fatma Hamad Rajab, amewakumbusha wakuu wa vitengo vya wizara hiyo Pemba, kuendelea kufanyakazi kwa pamoja, kwani huo ndio msingi wa mafanikio.

Alisema, changamoto ya udogo wa bajeti ya kutosha, uhaba wa watendaji katika vitengo vyao, pamoja na kikwazo cha usafiri, vinaweza kupata ufumbuzi, ikiwa wataendelea kufanyakazi kwa ushirikiano.

Katibu Mkuu huyo, aliyasema hayo Gombani Chake chake, wakati akisalimiana na wakuu wa vitendo vya wziara hiyo, alipokuwa kisiwani Pemba, kwa mapunziko ya sikukuu.

Alieleza kuwa, umoja na mshikamano ndio suluhisho la changamoto kadhaa zinazowakabili, na kinyume chake, wanaweza kuyumba kiutendaji.

Alifahamisha kuwa, kama viongozi wakuu wa wizara hiyo wanashirikiana kwa karibu, ni vyema mwenendo huo wakauiga, kwani unaweza kuwapandisha juu kiutendaji.

‘’Niwalazimishe watendaji wenzangu, kuwa mkitaka kufanikiwa pamoja na changamoto kadhaa, jambo la msingi na la lazima ni kuwa wamoja,’’alishauri.

Akizungumzia ufanisi wa wizara hiyo katika kutoa huduma kwa wananchi, alisema karibuni wanaopata maudhui kupitia ving’amuzi vya Z-MUX, watapata hata tv za nchi jirani.

‘’Wizara umeshajipanga kuimarisha upatikanaji wa maudhui kupitia ving’amuzi vyetu, na naamini kama mpango wetu utafanikiwa, tutaongeza idadi ya wateja,’’alifafanua.

Katika hatua nyingine, Katibu Mkuu huyo wa wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo Zanzibar Fatma Hamad Rajab, aliwasisitiza watendaji hao, kuzingatia stahiki za wafanyakazi wao.

Alieleza kuwa, suala la maslahi ya wafanyakazi liwekipaumbele cha kwanza katika utendaji wao, kwani ndio wanaoweza kuinyanyua wizara kiutendaji.

‘’Sitoridhishwa hata kidogo, kuona watendaji wa chini wanapelekewa mbele malipo ya stahiki zao, lakini waratibu wanajilipa mwanzo, lazima tuwe waungwana,’’alifafanua.

Hata hivyo, amepongeza wakuu hao wa maidara kwa kuonesha mshikamano wao katika utendaji wa kazi za kila siku, jambo ambalo linampa moyo kwenye nafasi zao.

Mapema Kaimu Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba, Khamis Massoud Khamis  alisema, wamekuwa wakishirikiana vyema na watendaji hao katika utendaji wao wa kila siku.

Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Habari Melezo Pemba Jamila Abdalla Salim, alisema udogo wa bajeti walionao, ni miongoni mwa changamoto zao.

‘’Gari yetu kwa sasa inahitaji matengenezo ya haraka, na hasa kwa vile mwezi ujao kuna shughuli ya kitaifa ya mbio za mwenge wa uhuru, lakini hata vifaa vyetu vya sauti vimechoka,’’alilalamika.

Nae Mkuu wa Idara ya Uchapaji Pemba, Kassim Hamad Nassor, alisema utamaduni huo wa Katibu Mkuu wa kukutana na wakuu wa Idara, unazidisha uhai wao katika kufanikisha majukumu yao ya kila siku.

Katibu mkuu huyo wa wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Fatma Hamad Rajab, amekusudia kuendeleza utamaduni wa kuwa na vikao kila baada ya muda na wakuu wa Idara, ili kusikiliza mafanikio na changamaoto zao.

                                           Mwisho         

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch