Skip to main content

GORA AWAAMSHA WATUNZA SIRI, MAKATIB MHUTASI WA SERIKALI PEMBA

 

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

NAIBU Katibu mkuu wizara ya Nchi, Afisi ya Rais, Katiba, Sheria, Utumishi na Utawala Bora Zanzibar, Omar Haji Gora amewakumbusha watunza kumbu kumbu wa tasisi za serikali, kuwa, roho ya wizara ya ni sehemu za masjali.

Naibu Katibu mkuu huyo, aliyasema hayo, kwa nyakati tofauti wakati akiyafungua mafunzo ya siku mbili, kwa makatibu muhutasi na watunza kumbu kumbu za serikali, kisiwani Pemba.

Akizungumza na watunza kumbu kumbu hao, kwenye mafunzo yaliyofanyika ukumbi wa wizara ya Fedh Gombani, alisema masjali ndio eneo nyeti pekee, katika kila wizara.

Alieleza kuwa, ofisi hiyo ndiyo inayotegemewa na wafanyakazi wote, kwa kuhifadhi kumbu kumbu zao mbali mbali, kama vile barua za ajira.

Naibu Katibu mkuu huyo, alisema masjali sio sehemu ya kuwekwa ovyo ovyo, na inatakiwa kuangaliwa kwa macho zaidi ya mawili, kwani ni eneo la kutunzia haki za wafanyakazi.

‘’Msipokuwa makini kwenye masjali, mnaweza kumsababishia mfanyakazi, ugonjwa, maradhi na hatimae kifo, ikiwa mtaipoteza moja ya kumbu kumbu zake muhimu,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Naibu Katibu Mkuu huyo, alisema ni kosa kisheria kwa mtumishi wa eneo la masjala, kutoa siri ya mtumishi mwenzake.

‘’Kwa mfano kuna barua za uteuzi, kusimamishwa kazi, kuhamishiwa eneo jingine, kuzuiliwa kwa ruhusa au kuomba mkopo, hapa wapo wanaotoa nje siri hizi,’’alieleza.

Akizungumza kwenye mafunzo kama hayo, yaliofanyika ukumbi wa Baraza la mji Chake chake kwa Makatibu muhtasi, Naibu Katibu mkuu huyo, aliwataka kuwa na lugha mzuri.

Alieleza kuwa, moja ya jambo kubwa ambao waliowengi wanashindwa kulifaulu ni matumizi ya lugha sahihi, kivazi na utunzaji siri.

‘’Mafunzo haya na mengine yanayosimamiwa na Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ ni sehemu ya kukumbushana majukumu yetu sisi watumishi wa umma,’’alieleza.

Mapema Afisa Mdhamini wa wizara hiyo Pemba, Halima Khamis Ali, alisema anatarajia kuona mabadiliko kwa watunza kumbu kumbu na makatibu muhtasi serikalini.



Alisema kumekuwa na kilio kikubwa, kuanzia kwa watumishi wa umma na wananchi wanaofuata huduma, juu ya kutopokelewa vizuri na watumishi wa kada hizo.

‘’Baada ya mafunzo haya na mengine, tutakuwa tunafuatilia kuona ikiwa kuna mabadiliko, maana haiwezekani kwa mtumishi wa umma, kuwa na kiburi,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Afisa Mdhamini huyo, aliwataka watunza kumbu kumbu hao, kuwaeleze wakuu wao wa tasisi, juu ya mafunzo hayo, katika eneo la mabadiliko ya kiutendaji.

Kaimu Mkurugenzi wa Chuo cha Utawala wa Umma Zanzibar ‘IPA’ Bakari Khamis Muhidini, alisema chuo kitaendelea kuwanao watumishi wa kada zote.

Alieleza kuwa, mafunzo haya sio ya mwanzo, kwani wapo watumishi wengine wakiwemo waalimu, wameshapewa kwa mujibu wa majukumu yao.

‘’IPA imekusudia kuyafanyiakazi, maono ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, la kuwataka wafanyakazi wa serikali kutofanyakazi kwa mazoea,’’alieleza.

Akiwasilisha mada ya maadili kwa watunza kumbu kumbu, afisa kutoka ‘IPA’ Hassan Juma Issa, alisema kanuni ya Utumishi wa umma ya mwaka 2014, inakataza kutoa siri za serikali.

Alieleza kuwa, masjala ndio roho ya taasisi, hivyo mtendaji wa eneo hilo, hutakiwa kuwa kioo kwa watumishi wenzake na jamii kwa ujumla.

Nae mtoa mada kutoka ‘IPA’ Mzee Juma Haji, alisema mfumo salama wa upangaji majalada, ndio njia sahihi ya upatikanaji wa taarifa kwa haraka za mtumishi.

‘’Mtendaji wa masjala kama asipokuwa makini na kutozingatia utaratibu unaotakiwa, anaweza kuwa msumbufu wakati wa uhitaji wa taarifa husika,’’alifafanua.

Baadhi ya washiriki wa mafunzo hayo, wamesema hawana shida ya kutunza kumbu kumbu kama inavyotakiwa, ingawa shida ni baadhi ya wakuu wa tasisi huwalazimisha kupinda sheria.

                           Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch