Skip to main content

MHADHIRI SUZA: WANAWAKE WENYE DHAMIRA YA KUGOMBEA ANZENI MATARISHO SASA




NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAWAKE wenye dhamira ya kugombea uongozi wa nafasi mbali mbali katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2025, wameshauriwa kuanza sasa kutengeneza mazingira, ikiwa ni pamoja na kufanyakazi kwa karibu na jamii husika.

Kauli hiyo imetolewa na Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ Salim Ali ofisi ya Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar ofisi ya Pemba, kwenye mafunzo ya siku tatu ya kuwajengea uwezo, wanawake wenye dhamira ya kugombea.

Alisema, maandalizi ya kuelekea kugombea, hutakiwa kuanza mapema, ili kujua mipango, mikakati, njia za kupita, namna ya kuwafikia wapiga kura na wasaidizi wake.

Alieleza kuwa, haiwezekani mwanamke anaetaka kugombea kwa nafasi yoyote, ile kujiacha na kutojishirikisha vyema ndani ya chama chake, na kugonjea miezi miwili, kabla ya uchaguzi mkuu ndio ajitokeze.

‘’Maandalizi ya kuingia kwenye uchaguzi wa kiushindani, hutakiwa kuanza mikakati ya kimnya kimnya mapema, ikiwa ni pamoja na kutambua udhaifu wa wagombea wengine,’’alieleza.



Katika hatua nyingine, Mhadhiri huyo kutoka SUZA, alisema suala la kujua ilani ya chama husika, sheria na kanuni za nchi japo kwa kiwango kidogo ni wajibu, ili iwe rahisi kuelezea mikakati husika.

Hata hivyo alisema rushwa na ngono au pesa ndio jambo moja wapo la kulikwepa kwa mgombea mwanamke, kwani humshushia heshima yake, kuanzia kwenye chama na jamii kwa ujumla.

Akifungua mafunzo hayo, Mratibu wa TAMWA-Pemba Fat-hya Mussa Said, alisema wakati umefika sasa kwa wanawake, kufanya uamuzi wa kuingua majimbo kuafuta uongozi.



Aidha Mratibu huyo wa TAMWA- alisema, hakuna jimbo ambalo linahati miliki kwa wanaume, bali kila jimbo la uchaguzi ni halali kwa makundi yote.

‘’Yapo maneno yanasemwa kuwa, jimbo fulani ni jimbo dume, kwamba kwa tafsiri ya juu juu, mwanamke ni marufuku, sasa dhana hii ndio mnatayarishwa ili mkaiondowe,’’alieleza.

Katika hatua nyingine Mratibu huyo, alisema majungu, fitna, kutiliana maneno na kufanya mambo kinyume na sheria, sio njia mwafaka ya kutafupta uongozi.

Mkurugenzi wa PEGAO, Hafid Abdi Said, aliwataka waweka dhamira hao, wasisite kutoa mifano kwa wanawake wenzao waliofanikiwa, kwenye nafasi mbali mbali za uongozi.



Alieleza kuwa, kufanya hivyo kutawavuta wengine kuona wanawake wanaweza wanapopata nafasi mbali mbali za uongozi.

‘’Wapo wanawake waliofanikiwa vyema kwenye nafasi za uongozi, sasa hawa tuwachukuweni kama kigezo chetu, ili tunapokutana na wapiga kura, wasione wanawake hawawezi,’’alifafanua.

Mapema Mratibu wa mradi huo wa SWIL kutoka TAMWA-Zanzibar Maryam Ame, amesema wanawake kama watajipanga vizuri, wanaweza kuibuka na ushindi katika kila chaguzi.

Alisema, wanawake ndio wengi kuanzia chamani, kwenye kampeni na hata siku ya kupiga kura, hivyo atasimama mwanamke mwenye sifa na kujitangaaza vizuri, anaweza kushika uongozi.





Baadhi ya washiriki hao, walisema wamekuwa wakishiriki kwenye chaguzi mbali mbali, ingawa changamoto kubwa ni ndani ya vyama vyao hawajaaminiwa.

Maryam Mussa Sharifu, Zainabu Mussa Bakari, Nadhira Suleiman Said pamoja na Asha Mbarouk Matano, walisema mafunzo hayo, yamewasaidia kuona mbali zaidi.

Mradi wa Kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia 'SWIL' ambao ulizinduliwa mwaka 2020, ukitarajiwa kumalizika mwaka 2023, unatekelezwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, Jumuiya ya Utetezi wa Kijinsia na Mazingira Pemba ‘PEGAO’ na Chama cha wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA.

                          mwisho 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch