Skip to main content

''KIMBILIENI ZAECA WANAWAKE MNAOGOMBEA MKIOMBWA RUSHWA YA NGONO''

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

MAMLAKA ya Kuzuia Rushwa na Uhujumu wa Uchumi Zanzibar kisiwani Pemba, imewataka wanawake wanaogombea nafasi mbali mbali za uongozi, wasisite kuwaripoti wanaowanyemelea kwa rushwa ya ngono.

Afisa kutoka ZAECA Kassim Yussuf Ali, aliyasema hayo Machi leo 29, 2023 kwenye mafunzo ya siku tatu, ya kuwajengea uwezo, wanawake wenye dhamira ya kugombea katika uchaguzi mkuu ujao.

Alisema, kama wanaona suala la rushwa ya ngono kwao limekuwa changamoto kuelekea katika kila chaguzi, wahakikishe wanaandaa mazingira ya kuwaripoti wanaotaka kuwachafua.

Alieleza kuwa, ZAECA imeanzishwa kisheria kwa kushughulikia changamoto kadhaa ikiwemo viongozi wanaotumia madaraka na uwezo wao vibaya.

Alifafanua kuwa, ZAECA imekuwa ikishughulikia migogoro ya ina hiyo, inayowakumbuka watu wa makundi mbali mbali, hivyo na wao wasisite kuwafikisha wale wanaowakwaza, katika kutafuta haki ya uongozi.

‘’Wanawake mmekuwa woga kuwaripotia wale wanaowakwaza katika kutafuta uongozi, na mkiendelea kukaa kimnya, haki yenu ya kuwa viongozi itakaliwa,’’alieleza.



Katika hatua nyingine Afisa huyo, alisema kwa uchaguzi mkuu uliomalizika, wapo wanawake wagombea kadhaa waliofikishwa ZAECA, wakitumia rushwa katika kampeni zao.

Akiwasilisha sheria ya Tume ya Uchaguzi pamoja na sera ya jinsia, Afisa Uchaguzi Msaidizi wilaya ya Chake chake Shikha Kitwana Sururu, alisema jambo la kuzingatia kwa wagombea wanawake, ni ujazaji wa fomu.

Aidha alieleza kuwa, kasoro nyingine ni vyama kuwateua wanaume wengi zaidi kuliko wanawake, jambo ambalo Tume haiwezi kuliingilia.

‘’Ni kweli wanawake hawaonekani kwa wingi majimboni, lakini hili lina pande mbili moja, inaonekana hawagombei kwa wingi, lakini pili ni vyama kutowapa kipaumbele,’’alieleza.



Hata hivyo alisema, jambo jingine linalowaangusha wanawake, ni kutokuwa makini katika ujazaji wa fomu, kutumia majina zaidi ya mawili na kutozikagua fomu kabla ya kuziwasilisha Tume.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa PEGAO, Hafid Abdi Said, aliwataka waweka dhamira hao, wasisite kutoa mifano kwa wanawake wenzao waliofanikiwa, kwenye nafasi mbali mbali za uongozi.

Alieleza kuwa, kufanya hivyo kutawavuta wengine kuona wanawake wanaweza wanapopata nafasi kadhaa iwe za kisiasa au maeneo mengine.

‘’Wapo wanawake waliofanikiwa vyema kwenye nafasi za uongozi, sasa hawa tuwachukuweni kama kigezo chetu, ili tunapokutana na wapiga kura, wasione wanawake hawawezi,’’alifafanua.

Wakichangia kwenye mafunzo hayo, akiwemo Maryam Saleh Juma kutoka Chama cha ukombozi wa Umma, alisema bado anaona kunachangamoto ndani ya Tume za uchaguzi.

Nae Amina Omar Msellem kutoka CCM, alieleza kuwa, wakati umefika kwa Tume za uchaguzi, kutoa elimu ya mpiga kura, hata kabla ya uchaguzi mkuu.

Kwa upande wake Iptisam Hamad Abdalla kutoka CHADEMA, Maryam Mussa Shaif kutoka ACT-Wazalendo na Asha Mbarouk Matano kutoka CUF, walisema mafunzo hayo yamewasaidia kujua kasoro.

Mapema Mhadhiri wa Chuo Kikuu cha taifa cha Zanzibar ‘SUZA’ Salim Ali, alisema moja ya jambo linalowaangusha wagombe wanawake, ni kukosa kuchagua timu nzuri ya kampeni.




‘’Inawezekana huangalii sifa za meneje wako kampeni, pengine ni mtu tamaa, anaependa fedha, wasiotosheka na hawajui ajenda yako, hawa wanaweza kukuangusha,’’ alieleza.

Akifunga mafunzo hayo, Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, Dk. Mzuri Issa Ali, aliwataka watia nia hao kuzisoma sera, sheria na ilani za vyama vyao.

Alieleza kuwa, haiwezekani mgombea hajui ilani ya chama chake, hajui mipaka ya jimbo lake, na hajui wananchi wanataka nini kama akipata nafasi hiyo.

‘’Lakini tusikubali kupewa taarifa za kusikia sikia, bali sisi wagombeA ndio tuwe watafutaji, wahariri na wasambaazaji wa taarifa za vyama vyetu na majimboni,’’alieleza.

 Wakati huo huo, Mratibu wa mradi wa SWIL kutoka TAMWA-Zanzibar Maryam Ame, amesema wanawake wana haki ya kuongoza na kushika nafasi mbali mbali, katika maeneo kadhaa.

‘’Ndio maana, TAMWA kwa kushirikiana na PEGAO na ZAFELA ikaandaa mradi huu, lengo ni kuwawezesha ili muweze kudai haki zenu za kisiasa, demokrasia na uongozi,’’alieleza.

 Mradi wa Kuwawezesha wanawake kudai haki zao za uongozi, siasa na demokrasia 'SWIL' ambao ulizinduliwa mwaka 2020, ukitarajiwa kumalizika mwaka 2023, unatekelezwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, Jumuiya ya Utetezi wa Kijinsia na Mazingira Pemba ‘PEGAO’ na Chama cha wanasheria wanawake Zanzibar ZAFELA.

                          mwisho 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch