Skip to main content

KAMPENI YA RAIS SAMIA YA 'MSAADA WA KISHERIA' YATAMBULISHW KWA WADAU PEMBA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

AFISA Mdhamini wizara ya nchi, afisi ya rais, Katiba, Sheria, Utumishi wa Utawala bora Pemba, Halima Khamis Ali, amesema kampeni ya kitaifa ya Rais ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan ya msaada wa kisheria, inalenga kutoa ulinzi na upatikanaji haki, kwa wanawake, watoto na wale wa makundi maalum.

Afisa Mdhamini huyo aliyasema hayo Machi 28, 2023, ukumbi wa wizara hiyo Gombani Chake chake Pemba, kwenye mkutano maalum wa kuutambulisha mkakati wa kampeni hiyo, kwa wadau wa haki jinai wakiwemo wasaidizi wa sheria kisiwani humo.

Alisema, kampeni hiyo iliyopewa jina la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kutokana na maono yake ya kwa makundi hayo na mengine, ya upatikanaji wa msaada wa kisheria, kampeni hiyo inakuja kuondoa changamoto hizo.

Alieleza kuwa, kampeni hiyo inagusa kila taasisi katika utekelezaji wake, ikiwemo wasaidizi wa sheria, Jeshi la Polisi, Tume ya haki za bindamu, vyombo vya sheria, Ofisi za ustawi, wizara husika ya katiba na sheria, vyombo vya sheria pamoja na jamii kwa ujumla.



‘’Kampeni hii inataka kuona, zile changamoto za upatikanaji wa msaada wa kisheria na kisha haki kwa wahusika, zinapatikana na hasa kwa wanawake, watoto na wale wenzetu wa makundi maalum,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Afisa Mdhamini huyo alisema eneo jingine katika kampeni hiyo, ni upatikanaji wa wasaidizi wa sheria wapya 5,000 kutoa elimu ya kisheria, kuzisomesha sera na sheria za upatikanaji wa msaada wa kisheria.

Aidha alisema, kila mdau kama ataitekeleza ipasavyo kampeni hiyo, majibu ya maono ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mama Samia Suluhu Hassan, yatafikiwa.

Kwa upande wake Afisa Sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar Ali Haji Hassan, alisema ujio wa kampeni hiyo, ni sehemu ya utekelezaji wa mpango mkakati, wa utoaji wa msaada wa kisheria Tanzania.

Alieleza kuwa, kampeni ambayo ni kwa ajili ya Tanzania bara na Zanzibar, imekuja ili kuimarisha upatikanaji wa msaada wa kisheria, kwa wananchi hasa wasiokuwa na uwezo.




‘’Tunaelewa kuwa zipo sheria kama ile ya Msaada wa Kisheria Tanzania bara, nambari 1 ya Mwaka 2017, Kanuni zake za mwaka 2018 na sheria nambari 13 ya mwaka 2018 pamoja na Kanuni zake za mwaka 2019 kwa upande wa Zanzibar, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na ile ya Zanzibar ya mwaka 1984, ambazo ndio msingi mkuu wa utoaji wa msaada wa kisheria,’’alieleza. 

Akiwasilisha mpango wa mkakati wa kampeni hiyo, Afisa Sheria kutoka Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar Yussfa Abdalla Said, alisema kila mmoja kwa nafasi yake ni mtekelezaji wa kampeni hiyo.

Alifahamisha kuwa, utekelezaji wa kampeni hiyo unatarajia kuongeza uelewa wa kisheria na haki za binadamu kwa jamii, hususan haki za wanawake na watoto.




Alieleza kuwa jengine ni kuimarisha huduma ya ushauri wa kisheria na unasihi kwa waathirika na manusura wa ukatili wa kijinsia pamoja na kuweka mazingira wezeshi ya upatikanaji wa huduma za kisheria.

‘’Kuongeza uelewa kwa wananchi kuhusu elimu ya sheria kwa umma, masuala ya haki na wajibu na misingi ya utawala bora, na kuwa na huduma endelevu za msaada wa kisheria katika ngazi zote za kijamii,’’alifafanua Afisa huyo.

Wakichangia, baada ya uwasilishwaji wa kampeni hiyo, washiriki akiwemo, Mkurugenzi wa Jumuiya ya Wasaidizi wa sheria wilaya ya Mkoani Nassor Hakim Haji, alisema kampeni hiyo, inaweza kufungua ufahamu kwa Jeshi la Polisi.

‘’Hadi leo bado baadhi ya vituo vya Jeshi la Polisi, wanawazuia watuhumiwa zaidi ya muda wa kisheria, inakuwa kila siku uende kuuliza sababu hizo, sasa kampeni hii itawazindua,’’alieleza.

Nae mjumbe kutoka Jumuiya ya Maimamu Zanzibar ‘JUMAZA’ Nassor Abdalla Mauli, alisema kampeni hiyo ni nzuri, ikiwa jamii na wadau, wataweka kando siasa zao.

Msadizi wa sheria Jimbo la Chake chake Mashavu Juma Mabrouk na Mratibu Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora Pemba, Suleiman Salim walisema kazi iliyobakia ni wananchi, kuelimishwa juu ya mpango huo.

Wakati huo huo Afisa sheria wa Idara hiyo Pemba, Bakar Omar Ali, alisema wanasiasa ni sehemu ya utekelezaji wa mpango huo, ingawa hakuwashirikisha moja kwa moja.

‘’Ni kweli wanasiasa ni jukwaa muhimu katika kampeni hii, lakini wanaweza kushiriki, ingawa sio moja kwa moja, kama walivyo wadau wengine,’’alifafanua.

Kampeni hiyo ya kitaifa ya msaada wa kisheria ya rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan, ilizinduliwa Machi 1, mwaka huu na ikitarajiwa kumalizika Machi 2026.

Kampeni ya Huduma ya Msaada wa Kisheria ya Mama Samia inalenga kulinda na kukuza haki ya upatikanaji haki kupitia huduma za msaada wa kisheria nchini.

Kampeni hii inatarajia kuboresha upatikanaji wa haki kwa watu wasiojiweza, hususani wanawake, watoto na makundi mengine yaliyo katika mazingira magumu.

 Vilevile, itachangia kuimarisha amani na utulivu, kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na kuleta utengamano wa kitaifa.

Utekelezaji wa kampeni hii, unatarajia kuongeza uelewa wa kisheria na haki za binadamu kwa jamii hususan haki za wanawake na watoto.





Aidha kampeni hii inatarajiwa kuimarisha huduma ya ushauri wa kisheria na unasihi kwa waathirika na manusura wa ukatili wa kijinsia.

Jengine ni kuwa, maono ya mabadiliko ya huduma ya msaada wa kisheria umetokana na azma ya Dk. Samia Suluhu Hassan Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya kuimarisha mfumo wa kutatua changamoto zinazowakumba wananchi bila kusubiria wananchi kuwasilisha changamoto zao wakati wa ziara za viongozi wa kitaifa.

Ambapo kampeni hiyo ya msaada wa kisheria itaongozwa na kauli mbiu isemayo Msaada wa kisheria kwa haki, usawa, amani na maendeleo

                 Mwisho

Comments

Post a Comment

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch