Skip to main content

MILELE ZANZIBAR FOUNDATION, OFISI YA DC: CHAKE CHAKE WAENDESHA ZOEZI LA UCHUNGUUZI KWA WANAFUNZI

 

 



 NA HAJI NASSOR, PEMBA::

WANAFUNZI wa skuli Pondeani na Michakaini wilaya ya Chake chake, wameanza kufanyiwa vipimo vya aina tofauti, ikiwa ni pamoja na usikivu, zoezi linaloendeshwa na Milele Zanzibar Foundation kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa wilaya hiyo, kupitia Ofisi ya watu wenye ulemavu wilayani humo.

Akizungumza kwenye zoezi hilo skuli ya Michakaini msingi wilaya ya Chake chake, Afisa miradi Idara ya afya kutoka taasisi hiyo Mohamed Abdalla Rashid, alisema Milele imekuwa ikijali mno afya za jamii.

Alisema, lengo la zeozi hilo ni kuangalia afya za watoto walioko skulini, ili kuwagundua mapema, hasa katika eneo la uoni, usikivu na kisha kupatiwa matibabu.

Alieleza kuwa, katika zoezi hilo limewashirikisha wataalamu wa koo, maskio na macho, kwa lengo la kuwafanyia uchunguuzi kwa kina na kisha kufikishwa hospitali kwa huduma zaidi.

Afisa huyo alieleza kuwa, zoezi hilo linaumuhimu mkubwa kwa mustkbali wa ukuaji wa watoto, kwani wakati mwengine wanaweza kugundua tatizo mapema, na kulitibu.


‘’Milele kwa kushirikiana na Idara ya watu wenye ulemavu, tuliona tuwafanyie wanafunzi hili, ili kuwapa uhakika wa kushirikishwa kikamilifu wakati wa masomo yao darasani,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, alisema afya ni jambo la msingi na muhimu kwa mtoto anayesoma, na kama akiachiwa bila ya kufanyiwa uchunguuzi, unaweza kukaathiri maendeleo yake.



Hata hivyo amewakumbusha wazazi na walezi, kutopuuza mazoezi kama hayo, kwani huwasaidia watoto wao katika malezi na makuzi.

Mratibu wa Baraza la Taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba Mashavu Juma Mabrouk, ameishukuru tasisi ya Milele Zanzibar Foundation, kwa kubali kufanikisha zoezi hilo.

Alisema Milele inatekeleza kwa vitendo, juu ya haki za makundi mbali mbali wakiwemo watu wenye ulemavu, kwani nao wana haki sawa na wengine.

Alieleza kuwa, zoezi hilo linaweza kwagundua mapema watoto wenye mahitaji maalum, na kama watapata ushauri na matibabu husika, wanaweza kuondokana na ulemavu unaozuilika.

‘’Kwa hakika zoezi hili linaumuhimu mkubwa, maana kwanza unaweza kumjua mapema mtoto anakabiliwa na changamoto gani, katika malezi na makuzi yake,’’alieleza.

Hata hivyo aliiomba Milele Zanzibar Foundation kulifanya endelevu zoezi hilo, na hasa kuelekeza nguvu katika maeneo ya nje ya miji.



Wazazi Hassan Khamis Ali na Mwamke Mtumwa Omar wa Machomane Chake chake, walisema zoezi hilo limesaidia kuwagunuda watoto wao, aina ya changtamoto walionayo kiafya.

Mzazi Tamima Mohamed Rajab, alisema amegundua kuwa mtoto wake anakabiliwa na changamoto ya uoni hafifu, baada ya zoezi hilo kukamilika.

‘’Kama ningekaa naye nyumbani nisingejua kuwa, mtoto wangu anakabiliwa na tatizo la macho ya uasho, lakini baada ya zoezi madaktari wameniambia na kupata dawa bila ya malipo,’’alieleza.

Mtaalamu kutoka kitengo cha macho hospitali ya Chake chake Dk. Shadya Mohamed Salum, amesema baada ya zoezi hilo, wamegundua kuwa wapo wanafunzi wanakabiliwa na changamoto ya uoni, bila yao wenyewe kujijua.

‘’Kwenye tatizo hilo, wapo wasioona mbali, wengine karibu na wengine wanahitajia matibabu ya haraka, kabla ya kupata athari zaidi,’’alieleza.

Mapema mwalimu wa upimaji wa usikivu kisiwani Pemba Omar Massoud Saleh, alisema wanafunzi wengi wamegundulika kuwa na nta ‘wax’ na wengine kutokwa na taka masikioni mwao.

Alieleza kuwa, kuwa upande wa taka, husababishwa na mafua ambayo hayatoki kwenye pua, na kisha hukaa na kwenda kwenye mishipa ya sikio.




‘’Kwa kawaida mafua hutokea kwa njia ya mirija ya pua, lakini haya baada ya kukosa njia, hukaa kwenye miraja ya sikio na kisha kugeuka taka, baada ya kupevuka,’’alifafanua.

Alieleza kuwa, masikio yote ya binadamu kwa kwaida huzalisha nta ‘wax’ na kisha kujisafisha wenyewe kwa kutoa maji maji mithili ya jasho na kisha kuganda.

‘Nta ‘wax’ ndio kinga na sikio na kama ataingia mdudu mdogo, anaweza kuganda na akijaribu kula, hupata uchungu ambao ndio sumu husika,’’alieleza.   

Wanafunzi 560 wa skuli za msingi za Michakaini A, B na Pondenia wilaya ya Chake chake, wanaosoma darasa la kwanza, wamefikiwa na wataalamu wa macho, miwani, usikivu na saikolojia, ili kuwafanyia uchunguuzi wa awali ikiwa wanakabiliwa na changamoto za kiafya.   

Milele Zanzibar Foundation inashughulika zaidi na uungaji mkono wa maono ya serikali kuu, katika maeneo ya afya, elimu na maisha ya jamii kwa ujumla hasa huduma za kibinadamu.

                       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch