Skip to main content

''WANANCHI 108,860 ZANZIBAR WASHINDA KESI ZAO BAADA YA MSAADA WA KISHERIA'' MKURUGENZI ZLSC

 




NA HAJI NASSOR, UNGUJA:::

WANANCHI laki 118,760 wakiwemo wanawake 60,203, wanaume 39,641 na watoto 18, 232 wamenufaika na elimu, msaada na ushauri wa kisheria kwa muda wa miaka 30 na kati  ya hao, laki 108, 860 wameshinda kesi na kupata haki zao mbali mbali.

Aidha kati ya hao 11, 8760 ni wananchi 9, 216 pekee ndio ambao licha ya kupata elimu na msaada huo wa kisheria, walishindwa katika kesi zao.

Akizungumza kwenye kongamano la maadhimisho ya siku ya haki za binaadamu duniani, leo Disemba 10, 2022 lililofanyika Kijangwani mjini Unguja, na kuandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar 'ZLSC' kwa kushirikiana na Tume ya Haki za Binaadamu 'CHRAGG' kwa ufadhili wa Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Haki za Binaadamu 'UN-OHCHR' Mkurugenzi Mtendaji wa Kituo hicho Harusi Miraji Mpatani, amesema wastan kwa mwaka waliopatiwa msaada ni wananchi 3, 936.





Ameeleza pia Kituo kiliwasaidia watoto na masuala ya kisheria 18,232, ambapo pia kwa upande mwengine, Kituo hicho kiliwapa elimu wananchi katika mikutano ya wazi, makongamano na semina wapatao 574, 808.



Amesema, licha ya changamoto ambazo kituo kimepitia wanajivunia kuona wapo wananchi, waliopata msaada wa kisheria na wengi wao kupata haki zao hivyo.

Hivyo Mkurugenzi huyo, ameitaka jamii kuendelea kukiunga mkono kituo hicho, ili kutimiza malengo yake, hasa ya kuwapatia elimu, ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo.

‘’Ni jambo la kujivuania kwetu na wananchi, kuona kituo kimeaminiwa na wananchi wastani wa laki 6 kuja kupata ushauri na msaada wa kisheria,’’alieleza.

Akizungumzia kuhusu kilele cha siku ya kimataifa ya haki za binaadamu, alisema kila mmoja akiheshimu haki za mwenzake, haki ya binaadamu wote kuwa ni sawa, italeta maana.


Kwa upande Mkurugenzi wa Kituo hicho Zanzibar, ameipongeza na kuishuru kwa dhati Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Haki za Binaadamu 'UN-OHCHR' kwa ufadhili wao ambao umefanikisha shughuli hii.

''Waliotupa uwezo wa hali na mali ni wezntu wa Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Haki za Binaadamu 'UN-OHCHR' na ndio maana shughuli yetu imeng'ara na inapendeza, kwa hili hongereni UN-OHCHR na ahasanteni,''alisema. 

Akifungua kongamano la maadhimisho hayo, Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibar Mgeni Jailan Jecha, alisema Zanzibar, ilikuwa ya mwanzo kuziweka kwenye katiba yake ya mwaka 1984.

‘’Ipo sura nzima ambayo lengo ni kuja kuzilinda haki hizo, hivyo ni wajibu wa wananchi, kuona kila mmoja anailinda haki ya mwenzake,’alieleza.

Aidha Mkurugenzi huyo alisema haki ya kuishi ndio hasa msingi mkuu wa haki za binaadamu, hivyo ni wajibu wa jamii na vyombo vya ulinzi na usalama, kulitilia maanani hilo.




Katika hatua nyingine, aliupongeza uongozi wa ZLSC kwa kufikisha miaka 30 ya utendaji wao wa kazi, na kuahidi kuendelea kushirikiana nao.

Mapema Mwenyekiti wa Bodi wa ‘ZLSC’ Jaji wa mahakama kuu Zanzibar Mshibe Ali Bakari, alisema suala la haki za binadamu ni jambo pana.



‘’Hakuna anayeweza kutoa tafsiri halisi ya maana ya haki za binadamu, hivyo maneno yaliomo kwenye katiba, kuwa binaadamu wote ni sawa, inatosha,’’aliafanua.

Katika hatu nyingine Mwenyekiti huyo wa ZLSC amesifu juhudi za ufadhili wa kufanikisha shughuli zote za siku mbili kupitia Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Haki za Binaadamu 'UN-OHCHR' na kuwaomba waendelee kushirikiana.

''Kwa niaba ya wajumbe wa Bodi wa ZLSC tunawashukuru sana wenzetu wa UN-OHCHR kwa ufadhili wao  mkubwa na dio uliofanikisha shughuli hiii, kwa hili hingereni sana,''alifafanua Jaji Mshibe. 

Kwa upande wake, Katibu wa Tume ya Kurekebisha sheria Zanzibar Mussa Kombo, alisema lazima suala la haki za binaadamu liangaliwe na utamaduni wa nchi husika.

‘’Kwa mfano Tanzania hatukubaliani na uwepo wa mapenzi ya za jinsia moja, hata kama ziko nchi zinakubaliana na kuona ni sehemu ya haki za binaadamu,’’alisema Katibu huyo.

Awali Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema changamoto walizokumbana nazo walizigeuza na kua fursa ya kusonga mbele.

Akiwasilisha mada ya hali halisi ya haki za binadamu Zanzibar na upatikanaji wake, Naibu Katibu wa Tume ya Haki za binadamu na Utawala Bora Zanzibar, Juma Msafiri Karibona, alisema serikali imekuwa mlinzi mkuu wa haki hizo.



Alieleza kuwa, zipo mamlaka zimekuwa ndizo zilizopewa jukumu ikiwa ni pamoja na Jeshi la Polisi, tume ya haki za binadamu, katiba na sheria mbali mbali.

‘’Kila mmoja akitimiza wajibu wake kwa kutii na kuheshimu haki ya mwengine, sio rahisi kusikia kuwa, kuna mmoja amevunjiwa haki zake,’’alieleza.

Afisa sheria kutoka vyuo vya Mafunzo Zanzibar Seif Maabad Makungu, alisema kwa sasa haki za binaadamu, kwa wanafunzi wa vyuo vya mafunzo, iko vizuri, ikiwemo kupata uhuru wa kuabudu.

Alieleza kuwa, hata mwaka huu 2022 wanafunzi watatu wameruhusiwa kufanya mitihani yao ya taifa, sambamba na kuwepo kwa milo mitatu, kupata habari kupitia tv na usomaji wa magazeti.

 Baadhi ya washiriki wa kongamano hilo, wamesema elimu bado inahitajika kwa jamii, ili kujua thamani na hadhi ya haki za binadamu.




Walisema, Jeshi la Polisi sio wa mwanzo kulinda haki hizo, bali kila mmoja na kwa nafasi yake, ananojukumu hilo.

Haya ni maadhimisho ya 12 ya haki za binadamu ulimwenguni kufanywa na Kituo cha Huduma za sheria Zanzibar ‘ZLSC’, ili kuwaleta pamoja wadau wa haki za binadamu, kujadili changamoto za uvunjifu wa amani, ambapo kwa mwaka huu yamefadhiliwa na Umoja wa Mataifa, Ofisi ya Haki za Binaadamu 'UN-OHCHR' 

                   Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch