Skip to main content

AFUNGWA MIAKA 7 PEMBA KWA KUMBAKA MTOTO WAKE WA KUMLEA

 





NA HAJI NASSOR, PEMBA::

MSHTAKIWA Said Abdalla Issa (40) wa Chanjamjawiri na Kengeja, ameanza maisha mapya chuo cha mafunzo, kwa muda wa miaka saba (7), baada ya mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, kukumuta na hatia ya kumbaka mtoto wake wa kulea mwenye miaka 14.


Pamoja na kutumikia adhabu hiyo, aidha hakimu wa mahakama hiyo Muumini Ali Juma, alimtaka mshitakiwa huyo kumlipa fidia ya shilingi milioni 1 muathirika huyo, haraka iwezekanavyo.

 

Mshitakiwa huyo ambae alimbaka mtoto wake huyo kumlea mwanzoni mwa mwaka 2019, kisha kesi hiyo kwa mara ya kwanza, ilifunguliwa mahakamani hapo, Mei 23, mwaka huo huo na upande wa mashataka, ukaanza kuwasikiliza mashahidi.

 

Akisoma hukumu ya kesi hiyo, hakimu Muumini alisema, ushahidi uliotolewa mahakamani hapo, ambao haukucha chembe ya shaka, ulitosha kumtia hatiani mshatakiwa huyo.

 

Alisema, mtu pekee anaeweza kuthibitisha kuwa ameingiliwa ni muathirika, na upande wa mashataka uliweza kumuongoza vyema mtoto huyo, na kukiri kuingiliwa kwake.

 

‘’Mtoto kwanza alimfahamu mshitakiwa (baba yake wa kufikia), na kisha aliieleza vyema mahakama, namna alivyobakwa kutoka hatua moja hadi nyingine,’’alisema.

 

Aidha hakimu alisema, mtoto huyo (aliyebakwa), alimtambua bila ya shaka yoyote mshitakiwa huyo, alipokuwa mahakamani, na hatua zilizochukuliwa na mama yake wa kulea, baada ya kubakwa.

 

‘’Lakini hata maelezo ya askari mpelelezi, nayo yaliunga mkono vyema maelezo ya mtoto, aliyoyatoa wakati akihojiwa kituo cha Polisi wilaya ya Chake chake, na kuzidi kuunga nguvu ushahidi huo,’’alisema Hakimu.

 

Katika hatua nyingine Hakimu huyo, alisema upande wa mashataka, ulithibitisha bila ya shaka umri wa mtoto kuwa ni miaka 14, ambapo kisheria hana ridhaa kwenye makosa ya ukatili na udhalilishaji.

 

Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, upande wa mashtaka ukioongozwa na wakili wa serikali Ali Amour Makame, uliiomba mahakama hiyo, kutoa adhabu kali kwa mshitakiwa.

 

‘’Vitendo vya ukatili na udhalilishaji vimekuwa vikiwaandama watoto, na wakati mwengine wamekuwa wakifanyiwa na watu wao karibu kama kaka au baba, sasa ni wakati wa mahakama kutoa adhabu, ambayo itakuwa fundisho kwa wengine,’’alisema.

 

Hata hivyo, upande wa utetezi ukiongozwa na wakili wake Abeid Mussa Omar, aliiomba mahakama hiyo, kumpunguzia adhabu mteja wake.

 

Alisema kuwa, bado ni nguvu kazi ya taifa, samba mba na kuwa na familia kubwa inayomtegemea, hivyo kama akipewa adhabu kali, anaweza kusababisha athari.

 

‘’Mteja wangu anafamilia kubwa inayomtegemea kwa kila kitu, sasa ni vyema kwa upande wa mahakama, ikalizingatia hilo, ili kuweko kwake ndani, isiwaumize wengine,’’aliomba.

 

Baada ya maombi ya pande zote mbuli, hakimu alisema ameyazingatia, na kuamua kumpeleka chuo cha mafunzo kwa muda wa miaka saba (7), na kumlipa fidia muathirika ya shilingi milioni 1.

 

Shahidi wa mwisho katika kesi hiyo, alikuwa ni mke wa mshtakiwa huyo, Shemsa Hakim Khamis wa Chanjamjawiri wilaya ya Chake chake, ambae awali alidai kuwa, mume wake hakumbaka mtoto wao wa kumlea, bali ni uongo alioutengeneza mtoto huyo.

 

Hata hivyo ushahidi huo, haukusaidia kumnasua mume wake kwa kosa la ubakaji kwa mtoto huyo, na hatimae juzi Novemba 29, mwaka 2022, kuhukumiwa miaka 7 na kulipa fidia ya shilingi milioni 1, ingawa haki ya rufaa imetolewa.

 

Mshtakiwa Said Abdalla Issa mkaazi wa Kengeja na Chanjamjawiri wilaya ya Chake chake, alimbaka mtoto wake wa kulea, tokea mwaka 2019.

 

Kufanya hivyo ni kinyume, na kifungu 108 (1), (2) (e) na kifungu cha 109 (1) cha sheria ya Adhabu nambari 6 ya mwaka 2018, sheria ya Zanzibar.

 

                Mwisho     

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch