Skip to main content

MAMA ZAINAB AKUMBUSHIA ADA SKULI 'BETTER CHANGE ACADEMY' KWA WAZAZI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:: 

MKE wa Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar, Zainab Kombo Shaib, amewakumbusha wazazi na walezi wenye watoto wao skuli ya maandalizi na msingi ya ‘Better Change Academy’ ya Gombani Chake chake Pemba, kulipa ada zao kwa wakati, ili kufanikisha azma ya waalimu kuwapatia elimu bora watoto wao.

 

Alisema kama wapo waliookeza kwenye elimu kwa kuanzisha kituo cha elimu ya maandalizi na msingi, ni wajibu kwa watakaopeleka watoto wao hapo, kulipa kipaumbele suala la ada.

 

Mke huyo Makamu wa Makamu wa Kwanza, ameeleza hayo ukumbi wa Samail Gombani Chake chake Pemba, kwenye mahafali ya pili ya skuli hiyo, yalioambatana na siku ya wazazi.

 

Alisema, mazuri yalioonekana kwenye sherehe hizo, msingi wake mkuu ni wazazi na walezi, kukubali kulipa ada zao kwa wakati.

 

Alieleza kuwa, elimu ni jambo pekee la thamani na ndio urithi pekee kwa mtoto, hivyo ni wajibu kwa mzazi ama mlezi huiska, kulitia maanani, jambo hilo.

 



"Niwakumbushe wazazi na walezi wenzangu, tuhakikishe tunajipanga vyema, ili kuona kuwa uhai wa skuli hii ambayo ni ada, zinalipwa kwa wakati,"alieleza.

 

Katika hatuna nyingine, Mke huyo wa Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar, Zainab Kombo Shaib amewataka wazazi wa kike kuacha utamaduni wa kuwapa watoto wao simu, kama sehemu ya ulezi.

 

Alieleza kuwa, siku hizi watoto wamekuwa wakilelewa na picha za katuni, milio ya simu ili mzazi ama mlezi apate wasaa wa kufanyashughuli zake nyingine, akijua mtoto wake yuko salama.

 


"Sasa simu ndio mlezi wetu nambari moja, sisi baada ya kuzaa mlezi wa watoto wetu ni milio ya simu na katuni na bila ya kujua kuwa, hicho ni moja ya chanzo cha ubakaji,"alifafanua.

 

Alisema kuwa sasa wale wanawake waliokuwa walezi ndio wanaoishia kwenye kumbi za starehe, harusi na huo wakati mdogo unaopatikana, watoto baada kunyonyeshwa wanapolia, huachiawa simu kama mlezi wao.

 

Akizungumza kuhusu skuli hiyo, Mke huyo wa Makamu wa Kwanza wa rais Zanzibar, mama Zainab Kombo Shaib, aliupongeza uongozi wa skuli hiyo, kwa juhudi zao kubwa.

 

"Skuli ndio kwanza ina miaka miwili, lakini matunda yake kama vile inamiaka 10, kwa kweli waalimu wanapiga kazi,"alifafanua.

 

Hata hivyo ameiomba wizara ya elimu na mafunzo ya amali, kuwa karibu mno na skuli hiyo ili kufanikisha azma yao, ya kutoa elimu yenye kiwango.

 

Kwa upande wake Mwenyekiti wa kamati ya wazazi skulini hapo, Khalfan Amour Mohamed alisema, licha ya changamoto wanazokabiiana nazo, lakini juhudi za walimu zinaonekana kwa vitendo.

 

Alieleza kuwa, skuli hiyo ambayo bado ni changa kwenye ramani ya mji wa Chake chake, lakini wamekusudia kuleta mabadiliko makubwa ya kielimu kwa haraka.

 

"Changamoto ya uhaba wa vyumba vya kuosomea na idadi ya waalimu saba ni ndogo, ingawa tunaendelea kujipanga, kufikia ndoto,"alieleza.

 

Akizungumzia umuhimu wa elimu, sheikh Said Abdalla Nassor alisema, hilo ndio jambo pekee ambalo mzazi anatakiwa kuhakikisha, anampa mtoto wake.

 


Akisoma risala Maaidizi Mwalim mkuu wa skuli hiyo, Issa Kingawaya, alisema moja ya changamoto wanazokabiliana nazo, ni ukosefu wa huduma ya maji safi na salama skulini hapo.

 

Aidha alieleza, kuwa jambo jengine ambalo ni kero kwao ni uchakavu wa barabara, iliyoingia skulini kwao kutoka barabara kuu ya Chake chake.

 





Katika mahafali hayo, yalioambatana na siku ya wazazi michezo kadhaa iliyopamba jukwaa, ilikuwepo ikiwa ni pamoja na utenzi, igizo, wimbo na masuala ya ibada kama dua sira hadithi kur-an tafsiri.

 

                                              MWISHO

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch