Skip to main content

MWENYEKITI BODI ZLSC AWAONYESHA NJIA POLISI KUMALIZA UHALIFU



NA HAJI NASSOR, UNGUJA:::

MWENYEKITI wa Bodi ya Wadhamini wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Jaji wa Mahakama kuu Zanzibar, Mshibe Ali Bakari, amesema lazima jamii na walinzi waamke, kutokana na wahalifu kutumia mbinu mbadala za kihalifu.


Alisema, hata wale wanaowadhalilisha wanawake na watoto wamekuwa wakitumia mbinu za ziada, kabla na baada ya kufanya matendo hayo, ambapo sio rahisi hata wataalamu wa kiulizi kubaini.


Mwenyekiti huyo wa Bodi, ameyasema hayo ukumbi wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzbar ‘ZLSC’ Kijangwani mjini Unguja, wakati akifungua kongamano la siku mbili, la kuelekea siku 16 za kupinga ukatili.

 


Alisema, lazima jamii na jeshi la Polisi liongeza nguvu za zaiada katika utendaji wake wa kazi, ili kukabiliana vyema na uhalifu na udhalilishaji uliopo.

                                                                                  

Alieleza kuwa, urahisi wa usafiri, wa vyombo vya maringi mawili, boti, ndege na meli zinazoingia Zanzibar, lazima walinzi na jamii washirkiane, ili kukabiliana na uhalifu.

 

‘’Kwa mfano uwepo wa boda boda baadhi yao sio waaminifu, na sasa ukipanda kwa mtu usiyemjua unakuwa na hofu kama safari yako hujafika,’’alieleza.

 

Katika hatua nyingine, Jaji huyo mstaafu  alisema, sio fahari watu wengi kufungwa, kuweko rumande, kesi kuongezeka na matendo, bali fahari ni kutokuwepo kwake.

 

‘’Jamii na wahalifu hawaogopi suala la kufungwa miaka mingi, bali lazima kutafutwe njia mbadala ya kupunguza matendo hayo, ili kila mmoja aishi kwa amani,’’alieleza.

 

Aidha Jaji huyo ambae pia ni Mwenyekiti wa Bodi wa ‘ZLSC’ aliwataka washiriki wa kongamano hilo, kutoa michango ambayo itasaidia katika mapambano hayo.

 

Mapema Afisa Mipango wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ Jamila Massoud, alisema kituo kimekuwa karibu mno na jamii, katika kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo.

 

‘’Tukiwa ndani ya siku 16 za kupinga ukatili, tumekuwa tukishirikiana katika kuona, jamii inapata uwelewe wa haki zao kupitia wasaidizi wa sheria,’’alieleza.


 


Akiwasilisha mada ya ukatili na udhalilishaji, Mratibu wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ tawi la Pemba, Safia Saleh Sultan, alisema hali hiaridhishi katika jamii, hasa kutokana na udhalilishaji wa watoto, sasa kufanywa na watu wa karibu.

 


Alisema, kwa mfano katika utafiti wa kihabari uliofanywa na TAMWA kati ya mwezi Oktoba 2021 hadi Juni 2022, wapo baba wazazi 13, kwa Pemba wanne na tisa Unguja, wamegundulika kuwabaka watoto wao.

 

Aidha alisema, utafiti huo pia umegundua kuwa, wapo waganga wa kienyeji 10 wakiwa wanne Pemba, na Unguja sita nao waliwabaka wateja wao, huku waalimu wa madrassa 20 nao wamegundulika kuwadhalilisha wanafunzi wao.

 

‘’Lakini hata kwa upande wa Pemba, sasa imegundulika kuwa wastani wa malalamiko 23 ya kuomba talaka, yamekuwa yakipokelewa mahakama ya kadhi,’’alifafanua.

 


Aidha mtoa mada huyo, alisema zipo athari kadhaa za ukatili na udhalilishaji kwa watoto, ikiwa ni pamoja na kukosa elimu, kupata athari ya kiakili na afya.

 

Naibu Mrajisi wa mahakama kuu Zanzibar Salum Hassan Bakar, alisema serikali imeanzisha mahakama maalum ya kupambana na udhalilishaji, na sasa hali inaridhisha.

 

‘’Kwa mfano mahakama maalum ya mkoa wa kusini Pemba, kwa mwaka huum imebakisha kesi tatu na mkoa wa kaskazini Pemba kesi 10, ambapo haya ni mafanikio makubwa,’’alisema.

 

Afisa dawati la wanawake na watoto kutoka jeshi la Polisi makao makuu Zanzibar Rahma Ali Salim, alisema bado jamii, inahamu ya kuzimaliza kesi hizo nje ya mahakama.

 

Hakimu wa mahakama maalum ya kupambana na makosa ya udhalilishaji mkoa wa kusini Pemba, Muumini Ali Juma, alisema adhabu kubwa haisaidii kupunguza makosa hayo.

 

Aidha alisema, bado kesi zinazaowahusu watoto wenye umri wa miaka 14 hadi 17 ndio zenye mashaka mahakamani, kwa kule kutoa ushahidi wa uongo.

 

Mwakilishi kutoka Jumuiya ya wanawake wenye ulemavu Zanzibar JUWAUZA, Salma Saadati, alishauri kuwa ofisi ya Mtakwimu mkuu iweke takwimu maalum za watu wenye ulemavu waliodhalilishwa.

 

Alisema, takwimu lazima ziwe jumuishi, zisiwe jumla jumla kama ilivyo sasa, ambapo hukosa mchanganuo halisi na kukosekana kuchukuliwa hatua stahiki.

 

 Wakichangia mada kwenye kongamano hilo, washiriki hao walisema elimu zaidi inahitajika kwa jamii, ili kuona waliowengi wanafika mahakamani kutoa ushahidi.

 

Mmoja kati ya washiriki hao, Kamisha wa msaidizi wa Polisi kutoka ofisi ya Naibu Mkurugenzi wa makosa ya jinai Zanzbar Haji Abdalla Haji, sasa kasi ielekee kwenye kuzuia matendo haya, na sio kutumia nguvu katika sheria kali.

 

‘’Nakishauri Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar sasa tuanzishe utamaduni wa elimu ya kuzuia matendo haya na zaidi ilengwe vijijini,’’alishauri.

 

Kongamano hilo la siku mbili ni sehemu ya maadhimisho ya siku 16 za kupinga ukatili, ambapo Disemba 10 Kituo hicho kitaadhimisha siku ya kimataifa ya haki za binadamu.

                   

                               mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch