Skip to main content

ZLSC: 'TATUWENI MIGOGORO KWA NJIA MBADALA ZA AMANI NA HAKI '

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

KITUO cha Huduma za Sheria Zanzibar, ZLSC kimewashauri wananchi wa shehia ya Wingwi Njuguni wilaya ya Micheweni Pemba, kikitumia kituo hicho wanapokuwa na migogoro mbali mbali, ili kupata sulhu kwa njia ya amani na haki.

Kauli hiyo imetolewa na Mratibu wa Kituo hicho Pemba, Safia Saleh Sultan, wakati akizungumza na wananchi hao, kwenye mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala za amani na haki, uliotanguliwa na igizo.

Alisema, ZLSC imekuwa ikibuni njia kila siku, kuhakikisha wananchi wanajengewe uwezo wa kujua sheria na kanuni,  na kisha weweze kutatua migogoro kwa njia ya amani, hasa kwa kesi za madai.

Alieleza kuwa, migogoro ya kesi za madai kama vile ya ardhi, ndoa, matunzo ya watoto, madeni baina yao ni vyema wakavitumia vikao vya familia, kuyamaliza.

‘’Kesi kama hizi mnapokimbilia mahakamani, kuna athari kadhaa moja wapo ni kupoteza muda, fedha na kuchelewa kupatikana sulhu, ambayo itakuwa endelevu,’’alifafanua.

Akizungumzia mradi utatuzi wa migogoro kwa njia ya mbadala za amani na haki, wanaouendesha kwa mwezi mmoja, chini ya the foundation for civil society, alisema wanatajia kuona wananchi, wanatumia vikao kutatua migogoro ya.

Kwa upande wake Wakili wa watoto wanaokinzana na sheria kutoka kituo hicho kisiwani Pemba, Siti Habib Mohamed, alisema njia ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya vikao vya familia, inafaa zaidi.



Alieleza kuwa, huwajenga wanajamii kuendelea kuelewana, kutowekeana visasi pamoja kutokurejea tena kwa mgogoro uliotatuliwa kwa njia mbadala za amani.

Katika hatua nyingine Wakili huyo, amewakumbusha wananchi hao wa Wingwi Njuguni, kuwatumia wasaidizi wa sheria, wanapokumbana na changamoto za kisheria.

‘’Kila jimbo na sasa karibu kila shehia wapo wasaidizi wa sheria, ambapo moja ya majukumu yao ni kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria bila ya malipo, sasa hao watumieni,’’alishauri.



Mapema Afisa Ufuatiliaji na tathmini kutoka ‘ZLSC’ Zanzibar Khamis Harouon Hamad, aliwataka wanananchi na hasa wanawake, kufuatilia haki zao kwa upana.

‘’Wanawake mnapokumbwa na changamoto za kisheria msikate tamaa mapema, fuatilieni hatua kwa hatua, na bahati nzuri sisi ZLSC, ni moja ya jukumu letu kuwasaidia tena bure,’’alieleza.

Akifungua mkutano huo sheha wa shehia ya Wingwi Njuguni Ali Hamad Said, alikipongeza Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kwa uamuzi wake, wa kuwapa elimu hiyo.

Alieleza kuwa, zipo shehia kadhaa wilaya ya Micheweni, ingawa Njuguni, imekuwa na bahati, na kuwaomba kufika mara kwa mara kutoa elimu kama hiyo.



Baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo, walisema suala la kutunza amani ni jambo moja kubwa, kwani inapochafuka, kuirejesha kwake, huwa vigumu.

Hamad Ali Suleyum, alisema amani ni tunda muhimu na ndio msingi na chachu ya kufikia maendeleo ya kweli, kwenye taifa lolote ulimwenguni.

Nae Mwaliche Haji aliwataka wanawake wenzake, kuwa na subra wakati wanapokumbana na changamoto kama za  migogoro ya ndoa.

‘’Suala la kufanya sulhu kwa njia ya amani na haki ndio chachu ya kuendeleza ndoa na familia kwa ujumla, na kwa hakika igizo tuliloliona kama tukilifuata hakuna sababu ya kuzuka migogoro,’’alisema.

Nae kiongozi wa dini sheikh Mohamed Ali Rubea, alisema kwa sasa, njia wanazotumia kijijini hapo kutatua migogoro, ni vikao vya kamati ya mskiti na vile vya familia.








‘’Wakati mwengine, ili kuzinusuru ndoa, huwataka mmoja kati ya wanandoa, kupuuza ama kujisahaulisha unapotokezea mgogoro, na njia hii hufanikiwa mno tena kwa amani,’’alieleza.

Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kwa sasa kinaendesha mradi wa utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala za amani na haki, unaofadhiliwa na the foundation for civil society.

                 Mwisho  

  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch