Skip to main content

WANAWAKE WAJASIRIAMALI KWENYE MASOKO, MADIKO WAKOGA MATUNDA YA UCHUMI WA BULUU PEMBA

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA

‘KABLA ya kuongezeka kwa wavuvi na wachuuzi hapa soko  la samaki Mkoani, nilikuwa mauzo yangu ya uji na maandazi ni shilingi 35,000 kwa siku, lakini sasa yamezidi mara mbili,’’anasema Aisha Hemed Khalifa.

Anasema, kwanza hakujua nini sababu ya kuongezeka kwa wavuvi na wachuuzi kwenye soko hilo, na alijikuta akiishiwa na biashara yake kabla ya saa 5:00 asubuhi muda aliouzoea tokea zamani.

Kwa kwaida, alishazoea anapoanza biashara yake hiyo, humaliza kati ya saa 5:00 hadi 5:30, ingawa kuanzia mwezi Januari mwaka huu hali imebadilika.

Biashara yake hiyo aliyoianza miaka mitano sasa, anasema ilikuwa ya kusua sua, kutokana na kuwa na idadi ndogo ya wavuvi na wachuuzi (wateja) kwenye soko hilo.

Awali aliacha biashara ya duka la vyakula, na kujiingiza kwenye uuzaji wa uji na maandazi, sokoni hapo Mkoani, ili kuongeza pato lake.

Akiwa kwenye soko hilo anasema biashara ilikuwa ya kudoro dora kiasi, ingawa pato lake lilikuwa tofauti, ikilinganishwa na biashara ya duka aliyokuwa nayo.

“Biashara hii ya uji na maandazi makavu kwangu, inalipa zaidi kuliko ile ya duka, maana kwanza hapa huwa naifanya kulingana na hali ya wavuvi na wachuuzi wanapokuja na sio kila wakati,’’anasema.

Mjasiriamali huyo aliyeachika miaka mitatu sasa akiwa anawahudumia watoto sita, kwa kwaida ikifika saa 5:30 mchana huwa ameshamaliza biashara na kurudi nyumbani kuendelea na shughuli za kilimo.

SERA YA UCHUMI WA BULUU ULIVYOKUZA BIASHARA

Anasema, kuanzia mwezi Januari mwaka huu 2022, sasa biashara yake imekuwa ikipanda siku hadi siku, akisema sera ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, imeongeza idadi ya wavuvi na wachuuzi.

Anasema, sio wavuvi lakini hata vijana wameamua kufunga susu nyuma ya baiskeli, kuamua kuchuuza samaki, wakiamini kuwa sekta hiyo, sasa imepata mkombozi.

“Sina takwimu halisi lakini sasa wavuvi wapya ninaowajua mimi tu wanafika 20, sambamba na wawachuuzi 30 wapya waliongezeka, wakifurahia uchumi wa buluu,’’anasema.

Mjasiriamali huyo anasema ahadi ya Dk. Mwinyi ya kuitumia bahari kwa ajili ya kukuza pato la wananchi, kwake limeanza hata kabla ya kuvua rasilimali yoyote baharini.

Sera ya uchumi wa buluu anaifahamu kuwa, ni kuinua pato la serikali na hata la mtu mmoja mmoja, likisababishwa na uwepo wa bahari.

“Hata mimi sasa kuongeza pato langu la biashara kutoka kilo nne za zamani za unga wa mtama hadi sasa kufikia kilo sita sio jambo dogo,’’anaeleza.

Anasema hata kwenye maandazi, alikuwa kabla ya ujio wa sera ya uchumi wa buluu, akitumia unga wa nganu kilo mbili kwa ajili ya maandazi, lakini sas analazimika kutumia kilo nne.

“Mimi amaandazi yangu sio kwa ajili ya wateja wa uji tu, lakini hata wengine wanaokuja sokoni, lakini ukweli kuanzia mwezi Januari hadi Machi mwaka huu mauzo yangu yamepaa,’’anasema.

Huyu ni mmoja tu, lakini wapo wapishi wa uji na maandazi na wengine chai wanaouza kwenye madiko (masoko ya samaki) 22 walielezea kupata manufaa.

Halima Omar Haji, aliyepo soko la samaki Wete, anasema sera ya uchumi wa buluu, kwake umeshapanda chati, baada ya kujikuta akiongeza mauzo ya biashara zake.

“Mimi nauza maandazi ya mafuta, ya kupambia na chai lakini sasa nimeshahama mauzo ya shilingi 35,000 kwa siku na sasa nahesabu kwenye shilingi 50,000 kwa siku,’’anasema.

Nilipotaka kujua sababu za kuongeza mauzo, akajikuwa kuwa anachokishuhudia ni kuongeza kwa wavuvi hata wale ambao walishatangaaza kustaafu.

Sababu nyingine ni kuongeza kwa wachuuzi vijana, jambo ambalo wapo waliopata mshangao na walipoulizwa wamesema wamejenga matumaini kwa ahadi ya rais Dk. Mwinyi.

Hata mjasiriamali wa juisi, vileja, uji na chai aliyepo bandari ya Tumbe wilaya ya Micheweni Tumu Haidari, anasema ameanza biashara hiyo kwa miaka sita sasa.

Kwa miaka yote hiyo, anasema hakuwahi kushuhudia mauzo ya shilingi 65, 000 kwa siku, ambapo hayo ameyashuhudia ndani ya mwaka huu.

“Mimi ilikuwa biadhaa zangu zote nikishauza najikuta nna shilingi 40,000 tu, lakini sasa dhana ya chumi wa buluu na kuongeza kwa wavuvi na wachuuzi, kwangu ni neema,’’anasema.

Hivyo hivyo, nae muuza mihogo ya kukaanga, chai na samaki soko la samaki Micheweni, Mwache Haji Hija anasema kwa sikukuu hii ijayo, anahakika ya watoto wake kuwanunua nguo kwa uhakika.

Anasema awali alikuwa akiifanya biashara hiyo kama eneo lake la mapunziko tu, lakini anataka kutanua mafya kwa sasa na kujenga kibanda cha kudumu.

“Lazima nimpongeze rais wangu wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kwa kuamua kuinua kipato chetu kwa mtazamo wa bahari, hii kwangu ndio yajayo ni neema tupu,’’anasema.

Mjasiriamali huyo anasema, kwa vile amekuwa akiingia kwa zamu na mwenzake sokoni hapo, ndio hasa pato lake huwa la uhakika zaidi.

Anasema, kwa miaka iliyopita kwa vile hakukua na idadi kubwa ya wachuuzi wala wavuvi na walaji, inaweza ikapita siku tatu bila ya kushuka sokoni.

“Sera ya uchumi wa buluu na ukweli wa vitendo wa rais Dk. Mwinyi, naamini ndio iliyoongeza idadi ya wanunuzi wa samaki, wachuuzi na wavuvi na wao baada ya kuuza na kununua hujipatia kinywaji kibandani kwangu,’’anasema.

MALENGO YA WAJASIRIAMALI HAO NI YEPI?

Wanasema, sasa wanajipanga kwenda Idara ya Uwezeshaji, ili kuomba mikopo, kwa ajili ya kuendeleza biashara zao na ikiwezekana waajiri wenzao.

Halima Juma Khamis wa aliyepo sokoni Wesha Chake chake, anasema aliwahi kuchukua mkopo wa shilingi 200,000 mwaka 2013, ingawa ulimshinda kurejesha.

“Kwa hatua ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi kuimarisha uvuvi na wengine wanaotegemea rasilimali za bahari, sasa najiamini kuchukua mkopo hadi shilingi 500,000,’’anasema.

Nae Halima Omar Haji, anaiomba Idara ya Uwezeshaji kupunguza masharti, ili sasa na wao waingie kwenye sekta ya mikopo, kama walivyo wenzao,’’anasema

WAVUVI NA WACHUUZI WANASEMAJE

Msaidizi mkuu wa diko la Wesha Chake chake Mohamed Haji, anakiri kuongezeka kwa wavuvi kwenye diko hilo, ambao baadhi yao walishataka kustaafu.

Anaema, sio wavuvi tu lakini hata kuna ongezeko kubwa la wachuuzi, na wengi wao kutoka nje ya mji wa Chakechake.

“Hivi sasa wapo wachuzui wanaotumia gari ndogo aina ya ‘carry’ kutoka miji ya Mkoani na Wete wakifuata samaki hapa, hivyo hawa wengi wao baada ya kufika hupata vinywaji,’’anafafanua.

Kwake anasema, dhana ya uchumi wa buluu ambao hata ndani ya soko hilo matunda yake yameshaonekana, ndio miongoni mwa sababu za kuongezeka kwao.

Mkuu wa wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja, anasema azma ya serikali, sasa kuwa ndio mkombozi wa kuinua kipato cha taifa na hata mtu mmoja mmoja.

Mvuvi Haji Kheir Haji wa Mwambe mwenye ngalawa jina la ‘joka pevu’ anakiri kuwa, ongezeko la wavuvi ni manufaa kwa wafanyabiashara hasa walioko kwenye madiko.

Pandu Mjanaheri Ussi ambae ni mchuuzi mpya, anasema kilichomvuta kufanya shughuli hiyo, ni kutokana na kauli ya rais wa sasa wa Zanzibar, wa kuiimarisha sekta ya uvuvi.

“Ni kweli, nimeona kundi la vijana wenzagu wakiwa wamefunga masusu na kuchuuza, lakini tukifika kwenye diko, kwanza hupata kifungua mdogo kwa wale mama zetu,’’anasema.

AHADI YA DK. MWINYI KUINUA PATO KWA UCHUMI W A BULUU

Wakati akinadi sera za chama chake cha Mapinduzi CCM kwenye kampeni, kuelekea chaguzi mkuu, aliwaahidi wananchi kuinua pato kupitia bahari.

Akisema kuwa, bado bahari ya Zanzibar haijaguswa kiuvuvi, na pindi akipata ridhaa, atakahakikisha anaongeza pato la taifa na la mtu mmoja mmoja kupitia shughuli zilizoko baharini.

Uchumi unaotokana na rasilimali za bahari kama vile samaki, chaza, majongoo na mwani (uchumi wa buluu) utaweza kuongeza pato la taifa.



Dk. Mwinyi aliwaambia wananchi wa Zanzibar kuwa, hali hiyo inaweza kuongeza makusanyo la mapato ya ndani kutoka shilingi bilioni 428. 511 kwa mwaka 2015 hadi kufikia shilingi bilioni 748.9

Lakini dhana ya uchumi wa buluu, ikitumika vilivyo inaweza kupunguza utegemezi wa bajeti na kufikia asilimia 5.7 na kuvuuka lengo lililoanishwa kwenye Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, na kufikia asilimia 7 hapo mwakani.

Dk. Mwinyi anaamini kuwa, kwa vile uchumi wa buluu hauwalengi, wavuvi, wachuuzi, wakulima wa mwani, majongoo, wavuvi wa mishipi, nyavu na madema pekee, anaona hata wanaofanya shughuli za juu watanufaika.

Hapa, alilenga sekta binafasi ambapo serikali inaazimia kushuka kwa riba ya mikopo, kutoka wastani wa asilimia 18 ya mwaka 2015 hadi asilimia 14 ya mwaka 2020.

Jambo moja ambapo wavuvi na wengine wanaotegemea bahari wanatarajia kulipata kama alivyoahidi Dk. Mwinyi wakati wa kampeni, ni kukamilisha utayarishaji wa sera mpya ya uvuvi na kufanya mapitio ya sheria ya uvuvi nambari 7 ya mwaka 2010.

Kwenye Ilani hiyo ya CCM, ambayo imeahidi pia kuongeza uzalishaji wa samaki, aina ya Jodari katika bahari kuu na ufugaji maalum wa kutumia vizimba ‘cage farming’ kutoka tani 36,728 hadi tani 44, 450.

Kubwa zaidi, ambalo nalo litafanywa ni kujenga miundombinu kwa ajili ya kuimarisha utendaji wa kampuni ya uvuvi ya Zanzibar ‘ZAFICO’ ikiwemo vyumba baridi vya kuhifadhia samaki.

Hapa Mkurugenzi mkuu wa Shirika la Uvuvi Zanzibar ‘ZAFICO’ Zahoro Kassim, anasema alichokiahidi Dk. Mwinyi sio ndoto bali yanaukweli, na hasa kwa vile hata ununuzi wa boti za uvuvi kwa ajili ya bahari kuu zinakuja. 



Matumaini pia kwa wananchi na hasa wavuvi na wachuuzi wa samaki ni pale, Dk. Mwinyi alipowaahidi wizara husika ya Uchumi wa Buluu, kuzalisha na kusambaaza vifaranga milioni 10 vya samaki, kaa na majongoo kila mwaka.

Haya sasa yakifanyika kwa pamoja, wale mama mtilie ambao wanaendesha biashara zao kando kando ya madiko na masoko ya samaki, wanaweza kuongeza pato lao mara dufu.

                               Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch