Skip to main content

SAADA KHAMIS: MWALIMU WA MADRASSA MWENYE ULEMAVU ANAYEFUNDISHA KWENYE MAZINGIRA MAGUMU


NA FATMA HAMAD, PEMBA

‘’KIPINDI cha mvua  wanafunzi hulazimika niwafungie  wasije madrasani mpaka  zitakapo malizika,’’ hayo ni maneno ya Sada  Khamis  Hamad  mwenye ulemavu wa viungo  ni  mwalimu wa madrssa.

Kwake anasema ulemavu alionao  haukua mzigo kuwa  asitimize ndota zake za kuwa mwalimu wa madrassa.

Hii ni baada ya kuukosa uwalimu wa skuli kutokana na changamoto za hapa na pale, ingawa hakukata tamaa.

‘’Nilikuwa natamani siku moja niwe darasani nafundisha   ila sikubahatika, kusoma skuli hata darasa moja, kwani ilikuwa iko maeneo ya mbali na siwezi kutembea,’’anakumbuka.

 Ukosefu wa kiti mwendo kwa wakati huo, na hasa kutokana na ukata wa fedha waliokuwa nao wazazi wake, ulimkosesha elimu ya skuli.

Yote hayo ni masikitiko ya Mwalimu wa Madrasa ya Qur-aan  Sada Khamis Hamad mwenye ulemavu wa viungo anaeishi katika kijiji cha Shumba Vyamboni Wilaya ya Micheweni Pemba.

Maalim Sada Khamis Hamad ambae ni mtoto wa sita  katika familia yao, anasema suala la kukata tamaa na yeye lilikuwa mbali mno.

Bada ya miaka kadhaa, alishindwa hakuweza tena kwenda madrasa kutokana na hali yake na kwa vile hana usaidizi wa kigari ambacho chengemuwezesha kumsaidia.

Baada  ya  kuona  anakosa  kusoma,  ndipo  akamua  anzishe  madrasa  yake  mwenyewe  baada ya kuhitimu kusoma Qur-aan  ili  aweze  kuiendeleza  elimu yake.

 ‘’Nilisema  ijapo kuwa  sikuweza  tena kwenda  kusoma, lakini   isiwe  sababu  ya  kukaa  tu nyumbani, ndipo  nikamua  nianzishe  madrasa  yangu, ili kuwafundisha watoto,’’anaeleza.

Huu ni mwaka wa nne tangu kuanzisha madrasa  hiyo, ambapo alianza  na  wanafunzi  wanne (4)  wawili wa kike na  wawili  wanaume  na  sasa  ana  wanafunzi 52.

ANA CHANGAMOTO GANI?

 Moja anayoiona na kumkosesha usingizi ni ukosefu wa  sehemu  salama  ya  kusomeshea wanafunzi kutokana na mazingira yake.

 Kwake mazingira hayo, hayako sio rafiki,  kwani  kwa sasa anatumia kibaraza cha  nyumba  yao kuwafundishia  wanafunzi  wake.



‘’Nasumbuka  sana  hususan kipindi  cha  mvua barazani panakuwa  hapasomeki  inabidi  wanafunzi  wasije  madarasa mpaka  mvua  zikate,’’ anasema.

Wanafunzi wamekuwa wakikimbia na kwenda madrssa nyengine kwa vile kuna  sehemu  salama  za kufundishia.

Akasema ni wakati kwa wale wanaouguswa na haki ya watoto juu ya elimu, kuona wanamtembelea na kumpiga tafu, ili kumjengea madrassa ya kisasa.

‘’Si vyema nguvu zote zikaelekezwa kwenye ujenzi wa miskiti pekee, bali msingi wa dini ya kiislamu, ni uwepo wa madrassa za kisasa na sio kusomea barazani,’’anafafanua.

WANAFUNZI WAKE

 Asha Khamis na Ali Juma wanafunzi wanaosoma  katika  madrsa hiyo, wanasema hawaridhishwi  na  kitendo cha kusoma  barazani.

‘’Kwakweli  hatupendi kusoma mazingira haya, kwani  pakiwa na jua hapakaliki, na kukiwa na mvua tunafungiwa kabisa,’’wanasema.

 Wanasema kama kweli kuna nia ya kweli kwa wadau wa haki za watu wenye ulemavu na watoto kusaka elimu, hakuna budi kujenga madrassa ya kisasa.

MAMA MZAZI

Hadia Salim Ameir, anasema  mungu  amemjaalia  kuzaa  watoto  wanne  wote  wenye  ulemavu  wa viungo  ambapo  mmoja  alifariki.

Anasema mwanzo akiwazaa wanakua ni wazima  wanatembea wenyewe, lakini  kila  wakiwa wakubwa  ndio wanapata ulemavu.

 ‘’Nilikua nawazaa ni wazima lakini mwisho wake wanakua walemavu, na sikuwapeleka Hospital nikajua ni sababu gani ilopelekea  hivyo’’,anasema mama huyo.

 

Aidha alieleza kuwa anaishi katika mazingira magumu  yeye na watoto wake  kwani  hata nyumba yao wanayoishi imeshakua mbovu na haina hata  huduma rafiki  za  vyoo  kwa  ajili  yao.

 

“Baba yao ameshafariki  huduma  zote   wananitegemea   mimi na sina msaidizi, sina  hata  kazi ya uhakika ya kufanya  maisha  yangu  ni  magumu  nahitaji  msaada”, alieleza.

Kwa bahati mbaya wako viongozi wa majimbo kama vile Mbunge au Mwakilishi hajawahi kupita katika familia yetu ili kuangalia changamoto zilizopo kwenye familia hii.

Mratibu  wa Baraza  la  Taifa  la  Watu wenye  ulemavu  Pemba  Mashavu   Juma  Mabrouk, anasema  wamekua  wakiwasaidia  watu  wenye  ulemavu, ambao  wanajishuhulisha  na  harakati  mbali mbali.

 Anasema  wamekua  wakifurahika  wanapoona  watu  wenye ulemavu   wakijishuhulisha   na  shughuli  mbali  mbali, hivyo  amewataka  wahisani  na  wasamaria  wema  kuelekeza   macho yao kwao.

 Hata hivyo amewashauri wazazi wa wanafunzi wanaosoma katika madrassa hiyo, kuonesha mfano kwa  kuanza kuchangishana fedha kwa ajili ya kuanzisha ujenzi wa madrassa ya kisasa.



” Sisi Baraza hatuna mfuko maalumu wa kumsaidia mtu mmoja moja kama huyo, kwani anayoyafanya ni mambo ya kijamii ispokuwa tunawaomba wanajamii kuchangia, ili aweze kujenga madrassa”, alishauri.

UONGOZI WA SHEHIA

Sheha wa shehiya  ya Shumba vyamboni Time  Said   Omar, ameleza kuwa  mwalimu  huyo anapata shida kwani  anasomeshea  wanafunzi wake  katika baraza  ya  nyumba  yao  na  wakati  mwengine  hukaa kwenye  Muembe.

Amesema  ameshachukua  jitihada  mbali  mbali  kuhakikisha  anapatiwa msaada  wa kujengewa madrassa  japo  chumba kimoja,  lakini  bado  hajafanikiwa.

‘’Nimeshawapeleka viongozi wengi ili waweze kumsaidia lakini bado hatujafanikiwa na   hivi saivi nimejipanga niende   kwenye jumuia ya Milele Foundation ili waweze kumsaidia’’, alieleza sheha .

Licha ya ulemavu wake lakini mungu amemjalia kipaji cha elimu  ameshafika  Dar-es-salamu  kushiriki mashindano ya qur ana, hivyo anahitaji  kuungwa mkono   kwa hali na mali  ili aweze kuendeleza  kipaji chake hicho.

UONGOZI WA WILAYA

Mkuu  wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatib Yahya, anasema anelewa changamoto ya mwalimu, huyo ingawa wanaangalia namna ya kumsaidia.

‘’Hakuna fungu maalum kwa ajili ya kumsaidia  mtu  mmoja  mmoja  kwa  ajili  ya  kujengea  nyumba  ama  Madrassa,  lakini kama wakitokezea wahisani tutampekelekea,’’anasema.



OFISI YA MUFTI

Msaidizi Katibu ofisi ya Mufti Sheikh Said Ahmad Mohamed, kwa vile ofisi hiyo ndi msimamizi mkuu wa madrasa zote za Qur-an, ameahidi kuonana naye.

‘’Nimevutiwa mno kuona kuna mwanamke tena mwenye ulemavu wa viungo ameanzisha mpango wa kuihuisha dini ya kiislamu, na sisi tutaangalia namna ya kumasaidia,’’anasema.

KATIBA YA ZANZIBAR YA MWAKA 1984

Kifungu cha 10 (g) kinafafanua ‘kwamba serikali itawekea mazingira rafiki kwa makundi ya wagonjwa, waliojiajiri, wazee, watoto na watu wenye ulemavu’.

Lakini hata kifungu cha 12 (1) kimefafanua kuwa, ‘watu wote ni sawa mbele ya sheria, na wanayo haki, bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki sawa mbele ya sheria’.’

SHERIA YA WATU WENYE ULEMAVU NO 9/2006

Kifungu cha 9, kinaelezea haki ya kupata elimu kwa watu wote wenye ulemavu na mafunzo mengine kama ilivyo kwa raia wengine.

                              MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch