Skip to main content

FCS YAAHIDI KUENDELEA KUFANYAKAZI NA ZLSC

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA:: 

email: hajipembatoday@gmail.com


TAASISI ya Foundation for Civil Society ‘FCS’ ya Tanzania bara, imesema itaendelea kufanyakazi kwa karibu na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’, ili kuhakikisha jamii inajengewa uwezo, wa kutatua migogoro kwa njia mbadala za amani na haki.

Hayo yalieleza na Afiss programu kutoka tasisi hiyo Eveline Mchau, wakati akiwasalimia wananchi wa Kibubunzi shehia ya Shumba Mihogoni, wilaya ya Micheweni, kwenye mkutano wa wazi wa kutoa elimu ya utatuzi wa migogoro, kwanjia mbadala.

Alisema ‘ZLSC’ imekuwa ikifanya vyema kwenye kutoa elimu, ushauri na msaada wa kisheria kwa wananchi bila ya malipo, jambo ambalo wao limewavutia.

Alieleza kuwa, kinachofanywa na ‘ZLSC’ cha kuwaelekeza wananachi namna bora ya utatuzi wa migogoro, hasa kwa kesi za madai, ni jambo jema, na tasisi yao inapendezewa mno.

‘’Wananchi, wakati umefika kutozitumia sana mahakama hasa kwa migogoro ya madai, na badala yake tuitumie elimu tunayopewa na wenzetu, kama hawa ‘ZLSC’ ambao tunafanya nao kazi,’’alishauri.





Mapema baadhi ya wananchi wa kijiji hicho cha Kibubunzi shehia ya Shumba Mihogoni, walisema utaratibu wa ‘ZLSC’ kuwafuata wananchi, uwe endelevu ili kupata uwelewa zaidi.

Mwananchi Ali Abdalla Ameir, alisema mpango huo wa kufika kijijini kwao, ni vyema na wananchi wengine kufikiwa na kufaidika na elimu hiyo.

‘’Elimu ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala za amani na haki ni nzuri, lakini sasa ‘ZLSC’ isiishie kwetu na vijiji vyengine mfike, ili ienee,’’alipendekeza.

Nao wananchi Khalfan Khamis na Hussein Faki, walisema changamoto mbali mbali zitajitokeza, pindi migogoro ya kesi za madai zitapelekewa mahakamani.



Akifungua mkutano huo, sheha wa shehia hiyo Salim Said Salim, alisema nafasi hiyo ni adhimu kwao, na aliwataka wananchi kuitumia, kwa kuuliza maswali.

‘’Kwa niaba ya wananchi wa kijiji hichi cha Kibubunzi, niwapongeze watendaji wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ na wafadhili wenu ‘FCS’ kwa hatua ya kutufika,’’alieleza.

Akieleza namna ya utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala za amani na haki, Mratibu wa ‘ZLSC’ tawi la Pemba Safia Saleh Sultan, alisema njia moja ni kuwatumia viongozi, dini na wazee kutatua migogoro hiyo.



Njia nyingine alisema, ni vikao vya familia, wasaidizi wa sheria na hata kuwatumia watu maarufu wanapokuwa na migogoro yenye mfumo wa madai.

Wakili wa watoto wanaokinzana na sheria kutoka ‘ZLSC’ tawi la Pemba Siti Habib Mohamed, alisema ni kosa kuzifanyia sulhu kesi za jinai, kama vile ubakaji, ulawiti, wizi na kuua.

‘’Kesi ambazo jamii inapaswa kuzikalia kitako na kutafuta sulhu ni zile za madai kama madeni, migogoro ya ardhi, ndoa na matunzo ya watoto na nyingine zinazofanana na hizo,’’alifafanua.

Aidha wakili huyo, alisema kwa kesi za madai wananchi wanapozitumia mahakama, hukumbana na changamoto kadhaa kama vile gharama, kupoteza muda na wakati mwengine kuwekeana visasi baada ya hukumu.






Kwa upande wake Afisa Ufuatiliaji na Tathmini kutoka ‘ZLSC’ Zanzibar Khamis Haroun Hamad, aliwataka wanananchi kushirikiana katika utatuzi wa kesi za madai, zinapotokezea katika maeneo yao.

 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ‘ZLSC’ kwa sasa kinaendesha mradi wa utatuzi wa migogoro kwa njia mbadala za amani na haki, unaofadhiliwa na the foundation for civil society kwa muda wa mwezi mmoja.

                 Mwisho  

  

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...