Skip to main content

WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA WATUNUKIWA VYETI, KISHA WAPEWA NENO

 

NA MWANDISHI WETU, PEMBA::____------

JANA Mei 26, 2022, wasaidizi wa sheria kutoka majimbo 18 ya uchaguzi kisiwani Pemba, wamemaliza na kisha kutunukiwa vyeti vyao, baada ya kumaliza mafunzo ya siku 15 ya wasaidizi wa sheria.

Aliyekabidhi vyeti hivyo, kwenye hafla iliyofanyika Gombani Chake chake, alikuwa Afisa Mdhamini Afiri ya Rais, Katiba, Sheria, Utamishi na Utawala Bora Pemba, Hali Ali Khamis.

Kwenye hutuba yake, aliwataka wasaidizi hao wa sheria, kwenda kuisadiai jamii, ili kupunguza majanga kama ya udhalilishaji, dawa za kulevya, migogoro ya ardhi na ndoa.

Hata hivyo aliwataka wasibweteke na elimu ya awali ya sheria walioipata, na badala yake, wabuni mbinu za kujiendeleza ili kupanua wigo, wa utoaji msaada wa kisheria.

Aidha aliipongeza Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar, kwa kuendelea kuijengea uwezo wa kisheria jamii ya Zanzibar.

Mkurugenzi wa Idara hiyo Zanzibar Hanifa Ramadhan Said, alisema pamoja na kumalizika kwa mafunzo hayo ya awali, Idara itaendelea kuwajengea uwezo, wasaidizi hao wa sheria.



Alisema, waliharakisha kuwapa elimu wasaidizi hao wa sheria wapya, ili wende vijijini kuisaidia jamii, na kisha mafunzo mengine yatafuata.

Hata hivyo, aliipongeza tasisi ya LFS, kwa kuendelea kuwaunga mkono katika mradi wa Kuimarisha upatikanaji haki Zanzibar, ambapo mafunzo, hayo ni sehemu ya utelezaji wa mradi huo.

Kwa upande Afisa sheria wa Idara ya Sheria Zanzibar Ali Haji Hassan, alisema wasaidizi hao wa sheria, walikuwa jasiri na anaamini, wamepata elimu waliyopewa.

Hata hivyo aliwataka kutojamini kipita kiasi wanapokwenda kwa jamii, na badala yake wajisomee zaidi, ili wanapowahudumia wawe na uhakika wa jambo husika.



‘’Jamii inawasubiri kwenda kuwapa elimu ya kisheria, ushauri na hata msaada wa kisheria, lakini silaha pekee ni kujisomea zaidi,’’alisema.

Naibu Mkuu skuli ya sheria Zanzibar -Utawala Khamis Juma Mwalimu, alisema wataendelea kushirikiana na Idara ya Katiba na Massada wa Kisheria Zanzibar, katika kutoa utaalamu.

Mapema wakisoma risala yao, wahitimu hao waliiomba Idara kuharakisha kupatiwa mafunzo nyongeza, ili kuongeza uwelewa wao wa siku 15.



Walisema, ni vyema kukaandaliwa kwa sheria nyingine kama ZSSF, mabaraza ya miji na hifadhi ya wazee, ili kuzifahamu kwa kina, wakati wanapotoa msaada wa kisheria.

Hata hivyo, aliiomba kutengenezewa vitambulisho maaluma, na kuandaliwa zira za kimafunzo, kisiwani Unguja ili kbadilishana uzoefu na wenzao.



Mahafali hayo ya wasaidizi wa sheria ni ya kwanza, yakisimamiwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria Zanzibar.

Mradi wa wasaidizi wa sheria, ulianzishwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ZLSC, mwaka 2007, ambapo kwa sasa wapo wasaidizi wa sheria zaidi ya 290 kwa Unguja na Pemba.

                                       Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...