Skip to main content

ANAYEDAIWA KUMPA UJAUZITO MWANAFUNZI KENGEJA AENDELEA KUSAKWA

 

 

NA HAJI NASSOR, PEMBA

JESHI la Polisi Mkoa wa kusini Pemba, linaendelea kumtafuta, Khamis Ali Khamis ‘Diri’ wa kijiji cha Ukunda shehia ya Kengeja wilaya ya Mkoani Pemba, aliedaiwa kumpa ujauzito mwanafunzi wa skuli ya Kengeja wilayani humo.

Jeshi hilo limesema, mtuhumiwa huyo aende atakako na ajifiche kwenye msitu mkubwa kiasia kigani, lakini mwisho wa siku, atatiwa mikononi na kufikishwa mbele ya vyombo vya sheria, kujibu tuhuma hizo.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Kamada wa Polisi mkoani humo Richard Tadei Mchomvu, alisema baada ya kutokea tukio hilo, mwaka juzi, alituma askari wake kumtafuta kisiwani Unguja, alikokimbilia bila ya mafanikio.

Alisema kwa vile mtuhumiwa huyo alijua kuwa ameshafanya jinai, kwa kumpa ujauzito mwanafunzi huyo miaka 16, aliamua kukimbia, ingawa kwa sasa wanashirikiana kwa karibu mno na Jeshi la Polisi la mikoa yote ya Unguja, kwa ajili ya kumtafua.

Alieleza kuwa, kwa sasa mitego imeshawekwa kila kona, na taarifa za mtuhumiwa huyo zimeshasambaa, ili kuhakikisha anakamtwa.

“Taarifa za tukio la kijana ‘Diri’ kumpa ujauzito mtoto huyo tunazo, na awali tulituma askari Unguja kwenda kumtafuta, ingawa hatukufanikiwa,”alieleza.

Akizungumza hatua nyengine iliokwisha chukuliwa na Jeshi hilo la Polisi, alifahamisha kuwa, ni pamoja na kufungua jalada la kesi la ubakaji la kumpa ujauzito mwanafunzi huyo.

Awali wazazi wa mwanafunzi huyo, walisema baada ya kutokea kwa tukio hilo mwaka juzi, mtoto wao walidhani anaumwa na ndipo aliposafirishwa hadi Unguja, kwa ajili ya matibabu zaidi.

Mama mzazi huyo alisema, baada ya kufikishwa Unguja na kufanyiwa vipimo, iligundulika kuwa ana ujauzito wa miezi sita, ingawa yeye kwa hatua za awali hakuelezwa kwa vile mume wake alikuwa mgonjwa.

“Mimi waliniambia tu kwamba anauma, na sasa ameshapata ahuweni, ingawa baadae nilianza kusikia kwa ajirani na kisha ndio nikapewa taarifa rasmi,”alieleza.

Mtoto huyo ambae mwaka jana alifanya mtihani wa taifa wa darasa la sita, alisema mtuhumiwa alimuendea usiku ndani nyumba yao, na kabla ya kufanya tendo hilo, alimtaka asitowe taarifa kwa mama yake.

“Baada ya kufika chumbani wakati taa nimeizima, alivua nguo zake na kuniweka goti kifuani na kuniziba mdogo na alinitaka nisije mueleza mama, na nikifanya hivyo atanijeruhi,”alieleza mtoto huyo.



Kwa sasa tayari mtoto huyo ambae mwaka huu alitarajiwa kuendelea na masomo yake ya darasa la tisa, ameshajifungua, na anasema kama akiruhusika baadae ataendelea na masomo yake ya sekondari.

Majirani wa mtoto huyo, walisema familia yao imekuwa ikikumbwa na mitihani ya kubakwa, maana hata dada yake kabla ya kuolewa na mume huyo aliembaka yeye, nae alibakwa.

Kwa upande wake Afisa wa ustawi wa Jamii wilaya ya Mkoani Aisha, alisema taarifa hizo wanazo ingawa, bado hawajalifuatilia kujua nini kinaendelea.

Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 11, kinaeleza kuwa, binadamu wote huzaliwa wakiwa huru, na wote sawa, wanastahiki heshima ya kutambuliwa na kuthaminiwa utu wake.

Azimio la ulimwengu juu ya haki za binadamu toleo maalum la miaka 60, kifungu cha 7, kinaweka wazi kuwa, mbele ya sheria watu wote ni sawa, na wanastahiki haki sawa za  kulindwa.

Sheria mpya ya Adhabu no 6, ya mwaka 2018 ya Zanzibar, kwenye kifungu chake cha 109, kimetamka kuwa, mtu yeyote ataketiwa hatiani kwa kosa la ubakaji, atatumikia kifungo cha maisha, ingawa katika mazingira mengine ya ubakaji, adhabu yake ni kifungo kisichopungua miaka 30.

Sheria ya Mtoto ya Zanzibar nambari 6 ya mwaka 2011 imetamka wazi juu ya jukumu la wazazi, walezi au mwengine anayekaa na mtoto kuhusu kumtunza na kumlinda na janga lolote lile likiwemo ubakaji na ulawiti.

 

Sheria ya elimu ya Zanzibar ya mwaka 1982 kifungu cha 20 (1) kinaelezea jukumu la wazazi au walezi kuhakikisha watoto wanasoma na kumaliza elimu ya lazima.

 

Lakini sheria ya kuwalinda wari na watoto wa mzazi mmoja, ya mwaka 2005, baada ya marekebisho, imeweka wazi iwapo, mwanafunzi atapata mimba, baada ya kujifungua anaweza kurejea masomoni.

 

Utafiti wa kitaifa uliofanywa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mwaka 2009, juu ya sababu za udhalilishaji, uligundua, watoto sita wa kike, na wa kiume kila tisa (9) wameshafanyiwa udhalilishaji kwa kila watoto 20.

 

Aidha utafiti ukagundua kuwa, watoto wa kike 62 na wakiume 71 walikuwa wamefanyiwa udhalilishaji wa kingono kabla ya kufikia miaka 18.

 

                     Mwisho

 

 

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch