Skip to main content

MSEMO AWAONESHA CHOCHORO WASAIDIZI WA SHERIA PEMBA KUFIKA MBALI

                                                                          


NA HAJI NASSOR, PEMBA


NAIBU Mkuu wa skuli ya sheria Zanzibar ‘Zanzibar school of law’ kitengo cha taaluma, Msemo Mavare amewataka wasaidizi wa sheria kisiwani Pemba, kujiendeleza na kuwa wanasheria kamili, mara watakapomaliza mafunzo yao ya awali.

Alisema, bahati ya kuingia kwenye usaidizi wa sheria ni mwanzo, hivyo ili isiwe mwisho, lazima wajiewekee mpango wa kujisomea sheria zaidi hapo baadae.

Naibu huyo aliyasema hayo Gombani Chake chake Pemba, wakati akizungumza na wasaidizi wa sheria tarajali, kwenye mafunzo ya siku 15 yanayoendelea, ambayo yameandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar.

Alisema, wapo wanasheria na mawakili hapa Zanzibar, ambao mwanzo wao, walianzia kuwa wasaidizi wa sheria, na wamepanua wigo wa kutoa huduma zaidi kwa jamii.

Alieleza kuwa, kada ya sheria, imekuwa tegemeo kubwa jamii ya watu maskini na wale wasiokuwa na uwelewa wa kujua misingi ya haki zao kisheria.

‘’Nyinyi wasaidizi wa sheria, mhakikishe mnajiendeleza kielimu hapo baada ya kumaliza mafunzo haya, maana elimu na hasa ya sheria ina uwanja mpana,’’alieleza.

Katika hatua nyingine, Naibu huyo mkuu wa skuli ya sheria Zanzibar kada ya taaluma, alisema jambo jengine muhimu la kuzingatia, ni kuwahudumia wananchi bila ya ubaguzi.

Hata hivyo, amewataka wasaidizi hao wa sheria tarajali, kuthamini nafasi hizo, kwani walioomba kwa Pemba pekee, walikuwa zaidi ya 200 na kupatika 18 kutoka kila jimbo la uchaguzi.

Kwa upande wake Afisa sheria kutoka Idara ya Katiba na msaada wa sheria Zanzibar, kisiwani Pemba, Bakari Omar Ali, alisema kazi ambayo iko mbele yao, wasaidizi hao wa sheria, ni kujitolea zaidi.



‘’Muelewe kuwa, mnakwenda kuisaidia jamii, ambayo wakati mwengine imeshakata tamaa, hivyo hakuna malipo ambayo unaruhusika kumdai, hata kama atapa mabilioni ya fedha,’’alieleza.

Akiwasilisha mada ya sheria nambari 7 ya mwaka 2018 ya Mwenendo wa Makosa ya Madai Zanzibar, wakili wa kujitegemea, Zahran Mohamed Yussuf, alisema huo ndio msingi mkuu wa kesi za madai.

Alieleza kuwa, msingi mkuu wa kudai haki kupitia hati ya madai, inajumuisha, jina kamili la mdai ‘Plaintiff’, anuwani kamili, kinacholalamikiwa.

‘’Lakini hata kwa anayedaiwa ‘defendant’ nae baada ya kupokea wito, atakakiwa kujibu kipengele kimoja baada ya chengine kwa nambari, na kisha atatakiwa kuwasilisha mashahidi,’’alieleza.

Nae wakili wa sherikali kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa mashtaka Juma Ali Juma, aliwataka wasaidizi hao wa sheria, kuwa makini kwenye mafunzo hayo.

Baadhi ya wasaidizi hao tarajali, walisema mafunzo hayo watayafanyia kazi ipasavyo, ili kuona jamii iliyowazunguruka inanufaika na mafunzo hayo kwa kina.



Juma Seif Juma wa jimbo la Chonga, Abdalla Saleh Issa Mkoani, Omar Abdalla Nassor wa jimbo la Pandani na Habib Chapa Hamad wa Jimbo la Micheweni walisema, bado jamii inahitajia elimu juu ya kujua haki zao za kisheria.

Mafunzo hayo ya siku 15 yalioanza Mei 12, mwaka huu yameandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa kisheria Zanzibar, yalifadhiliwa na LSF na mada kadhaa zilijadiliwa ikiwa ni pamoja na mirathi, jinai, sheria za ardhi, dhana ya wasaidizi wa sheria na maadili.

                                           Mwisho        

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch