NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@
Maafisa ufuatiliaji na tathmini wa wizara mbali mbali Pemba wameshiriki katika mafunzo ya kujengewa uwezo juu ya ufuatiliaji na
tathmini za miradi, ili kufanya kazi zao kwa ufanisi.
Akizungumza na washiriki wa mafunzo
hayo katika ukumbi wa makonyo Wawi
chake chake Pemba mgeni rasmi kwa niaba
ya Kaimu
Katibu mtendaji Tume ya mipango
Zanzibar, Kamishna idara ya Uchumi Ameir
Haji Sheha alisema, mafunzo hayo ni muhimu kwa maafisa hao katika utekelezaji
wa majukumu yao ya kikazi.
Alisema mafunzo hayo yatasaidia
kujenga utamaduni wa kufuatilia na kutathmini ili kupata takwimu sahihi za utekelezaji miradi na shughuli za maendeleo ,
ambazo mara nyingi hutumika katika utaarishaji wa mpango wa maendeleo ya Zanzibar.
Alisema ufuatiliaji na tathmini
husaidia watekelezaji wa miradi kujua mwelekeo wa utekelezaji wa kazi zao, ili kuhakikisha utimilifu wa
malengo ya mda mrefu waliojiwekea kulingana na muda sahihi.
" Ufuatiliaji wa miradi na
tathmini husaidia kujua mwelekeo wa utekelezaji wa kazi kwa kuhakikisha malengo ya mda mrefu yaliowekwa
yanafikiwa kulingana na muda husika, ndio maana tumeandaa mafunzo haya, "
alieleza.
Aidha aliwapongeza watendaji wa tume
ya mipango kwa kuandaa mafunzo hayo kutokana na umuhimu wake katika kuwaongezea
uwezo maafisa hao ili watimize majukumu yao kwa ufaninisi zaidi.
Nae
Afisa mdhamini tume ya mipango Pemba Khamis Issa Mohamed aliwataka washiriki wa mafunzo hayo kutumia
taaluma watakayo ipata katika utekelezaji kazi zao ili kuendana na kasi ya utendaji kazi wa rais
katika kuleta maendeleo kwa jamii.
Alisema maafisa ufuatiliaji na
tathmini wanakazi ya kupanga na kufuatilia miradi mbali mbali ya kimaendeleo,
hivyo mafunzo hayo ni hatua muhimu katika utekelezaji majukumu yao.
"Nyinyi ndio wenye kazi ya kupanga
na kufuatilia miradi ya maendeleo, hivyo mafunzo haya ni hatia muhimu katika
utekelezaji majukumu yenu ya kikazi", alieleza.
Aliongeza kua kwa mara ya kwanza maafisa hao watapatiwa
mafunzo ufuatiliaji katika miradi ya kiuhandisi ambayo ni mara ya kwanza kufanyika kwa Zanzibar.
Mmoja wa washiriki wa mafunzo hayo Nachia Hamad Suleiman kutoka wizara ya fedha na mipango Pemba alisema, mafunzo hayo yatawasaidia kujua ufuatiliaji wa miradi kwa usahihi ili kupata matokeo chanya kama inavyokusudiwa.
Mafunzo hayo yalioandaliwa na Tume ya
mipango yameanza leo tarehe
1Disemba yamehusisha maafisa ufuatiliaji
na tathmini kutoka wizara 18 za serikali
na yanatarajiwa kufanyika kwa muda wa siku nne.
MWISHO

Comments
Post a Comment