Skip to main content

LEO SIKU YA WATU WENYE ULEMAVU DUNIANI, MATAMU YAO HAYA HAPA KWA ZANZIBAR

 

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

SIKU ya kimataifa ya watu wenye ulemavu duniani, ilianza kuadhimishwa mwaka 1992 na Umoja wa Mataifa.

Tangu kuanzishwa kwa siku hii, kumekuwa na mafanikio mbalimbali duniani, ambapo kwa Zanzibar pekee, ni kuwepo wa sheria nambari 8 ya mwaka 2022.

Malengo ya siku hii, ni kuongeza uelewa juu ya mambo yanayohusu watu wenye ulemavu, pamoja na kutoa elimu juu ya haki na fursa zao.

Taarifa za mitandao zinafafanua kuwa, siku hii hutazamiwa kuongeza uelewa kwa watu wenye ulemavu, katika masuala kadhaa, likiwemo la uchumi wao.

Malengo endelevu ya dunia Sustainable Development Goals ‘SDGs’ ni mkusanyiko wa malengo 17 yalopangiliwa kwa faida ya watu wote ulimwenguni, wakiwemo wao.

Maana, malengo haya yalianzishwa mwaka 2015 na Baraza kuu la umoja wa mataifa, yalikiwa na malengo ya kufikiwa mwaka 2030, kama sehemu za ajenda za mwaka huo.

Kwani inafahamika kuwa, miongoni mwa malengo hayo endelevu ni pamoja na kutokomeza umaskini, kukomesha njaa, afya njema na ustawi, elimu bora, usawa wa kijinsia na maji salama.



Wakati leo dunia ikiadhimisha siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu, watu wenye ulemavu Pemba, wanasema ipo hatua iliyochukuliwa dhidi yao.

 MATAMU DHIDI YAO

Mashavu Juma Mabrouk ambae ni Mratibu wa Baraza la taifa la watu wenye ulemavu Zanzibar ofisi ya Pemba, anasema kuwepo kwa sheria mpya ni jambo jema kwao.

‘’Leo tukiadhimisha siku ya kimataifa ya watu wenye ulemavu, lazima tujivunie walau kuwa na sheria hiyo mpya na sera yake,’’anasema.

Suleiman Manour kutoka Jumuiya ya wasioona ZANAB, anasema awakiadhimisha siku ya watu wenye ulemavu, yapo mazuri kwao.

‘’Hata kuwa na wizara inayoshughulikia watu wenye ulemavu ni jambo jema, maana zamani ilikuwa sisi tukihangaika huku na kule tu,’’anakumbuka.



Hidaya Mjaka Ali kutoka Umoja wa watu wenye ulenmavu ‘UWZ’, anasema zipo asasi zaidi 10 za watu wenye ulemavu na hukutana na kujadiliana.

‘’Kwa mfano tulianza na ‘UWZ’ sasa zipo kama ZANAB, ZAPDD, CHAVIZA, JUWALAZA zote hizi na nyingine ni ishara kwamba tunatambulika kisheria,’’anaeleza.

Katija Mbarouk mjumbe wa baraza la watu wenye ulemavu wilaya ya Wete Pemba, anasema sasa wanashirikishwa, kwenye mambo kadhaa ya kiinchi kama uongozi.


‘’Kwa mfano hivi karibuni tulikuwa na Tume za uchaguzi ile ya Zanzibar ‘ZEC’ na ile ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ‘INEC’, katika ushauri wa kuelekea uchaguzi mkuu,’’anakumbuka.

Omar Haji Nassib wa Mchanga mdogo, anakiri kuwa wakati wakiadhimisha siku ya watu wenye ulemavu, kwa kiasi kikubwa, heshima yao ipo kwa jamii.

‘’Kwa mfano hata ukitaka kupanda meli, ndege au gari watu wanakupata nafasi na wakati mwingine unapewa heshima kubwa,’’alieleza.

HAYA YALIKUJAJE?

Aliyekuwa Waziri katika ofisi ya Makamu wa Kwanza Harusi Said Suleiman, anasema serikali inaendelea kuthmani kwa vitendo, haki za watu wenye ulemavu.

‘’Kwa mfano hata ujio wa sheria mpya ya watu wenye ulemavu nambari 8 ya mwaka 2022, ni ishara kwa serikali kuwathamini,’’anasema.

Afisa Mdhamini wa Afisi hiyo Pemba Ahmed Abubakar, anasema eneo jingine ambalo serikali, inathamini watu wenye ulemavu kwa vitendo, ni kuanzishwa kwa baraza la taifa la watu wenye ulemavu.

Anakumbuka kuwa, kwenye hiyo sheria yao mpya, vifungu vinalazimishwa kuanzishwa kwa baraza hilo kwa ajali yao, na sasa lipo na ni msaada mkubwa.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, akilihutubia baraza la wawakilishi, aliahidi kuendelea kuzitekeleza haki za watu wenye ulemavu.

MITANDAO INARIPOTI NINI?

Kwa mujibu taarifa kutoka kwa Tume ya Haki za Binaadamu na Utawala Bora ‘THBUB’ wakati wa maadhimisho ya siku kama hii, mwaka 2021, ilisisitiza haja ya kuzitunza haki za kundi hilo.

 Kwenye taarifa yake, ikisisitiza kuwa, siku hii ni matokeo ya Azimio nambari 47/3, la mwaka 1992 la Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, lililopitisha Disemba 3 ya kila mwaka, kuwa ni siku ya kimtifa.

Juni 13, mwaka 2021, BBC Swahili iliripoti, kuwa watu wenye ulemavu na hasa wale wa ngozi, hupitia changamoto kadhaa, katika maisha yao, na kukosa furaha.

Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA-Zanzibar, kinaendesha mradi maalum, ambao unawajengea uwezo waandishi wa habari, ili kuyaibua wanayofanywa na wawtu wenye ulemavu.

Mkurugenzi wao Dk. Mzuri Issa Ali, anasema vyombo vya habari, havikuwa na weledi wa kuandika taarifa za watu wenye ulemavu, jambo lililowaficha na kuzidi kupata msongo wa mawazo.



''Loe tukiwa ndani ya siku ya kimataifa kwa ajili yao, walau unaona mazuri yanayofanywa na watu wenye ulemavu katika vyombo vya habari,''anasema.

             Mwisho  

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...