Skip to main content

MDHAMINI MAKAMU WA KWANZA, AELEZEA UBORA MATUMIZI YA GESI

 



NA SAIDA ALI, PEMBA@@@@


AFISA Mdhamini Afisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Ahmed Abuubakar Mohamed, amesema mazingira mazuri ni kuunga mkono kwa kutumia nishati salama ya gesi, ikiwa ni njia moja wapo ya kulinda mazingira yao, ili kuweka mabadiliko yanayotokezea kutokuwa na hali nzuri ya kimazingira.


Ameyasema hayo alipokuwa akizungumza wafanyabiasha ya ‘Oryx gas’ juu ya matumizi salama ya nishati safi ya kupikia, ukumbi wa Tibirinzi Chake chake Pemba.


Alisema kuwa utumiaji mzuri wa gesi na uhamasishaji, wanaweza kulinda hali ya mazingira, ukataji wa miti ovyo na uchimbaji wa nchanga na uharibifu wa viunbe hai ambavyo vinaweza kuwa mazingira mazuri.

" Uwepo wenu kutasaidia wananchi kutumia nishati safi na salama ya kupikia, pamoja na kuacha kukata miti na mbadala wake, kutumia gesi, ili kuhakikisha hali ya mazingira inakuwa salama," alifafanua.  

 
Meneja Mkuu wa taasisi ya Oryx gas Zanzibar Shuwekha Khamis Omar, alisema kuwa, wanadhamira ya kuhakikisha upatikanaji wa gesi, unakuwa wa uhakikika na kuimarisha huduma zao kwa ufanisi.


Alisema kuwa, ufanisi huo umekuwa hasa katika kipindi hichi cha miaka mitano, wameweza kuimrisha huduma zao kwa kuweka bohari kubwa la kupokelea gesi na kuhifadhi eneo la Mangapwani Unguja.


Alieleza kuwa, bohari hiyo imeweza kupokea Meli za Gesi Zanzibar, na uhifadhi mkubwa wa karibu tani 1,300  na  inauwezo wa  kutumiwa na wananchi wa Unguja na Pemba.


"Tumekuwa tukiimarisga huduma na ufanisi mkubwa katika tasisi yetu, na ufanisi huo umekuwa hasa katika kipindi hichi cha miaka mitano kwa kuweka bohari kubwa ya kupokelea na kuhifadhi,’’ alieleza.


Mkurugenzi wa Oryx gas Zanzibar Fuad Alinabhany alisema, nishati pekee yenye kuaminika ni utumiaji wa oryx gas pamoja uuzaji wa mitungi hiyo.


Kwa upande wake mfanyabiashara Juma Mussa Said wa Chanjaani Chake chake, aliahidi kuyachukua vyema mafunzo hayo na kuwa mabalozi mzuri, kwa wauzaji wao.


Alisema kuwa jambo jema walilolipata hapo kwenda kuwahamasisha watumiaji wa gesi, kueka sehemu salama pamoja na kuinasihisha jamii, kutumia nishati mbadala.

MWISHO.

 

Comments