Skip to main content

KIDUTANI WAPITISHA KANUNI KUSIMAMIA MALEZI YA VIJANA WAO

 


 NA MOZA SHAABAN, PEMBA @@@@

KAMATI ya maadili na taaluma ya kijiji cha Kidutani shehia ya Chumbageni Wilaya ya Mkoani Pemba, imepitisha kanuni 19 zitakazowaongoza katika kusimamia malezi ya watoto na vijana.

Akizungumza kijijini hapo  katika kikao cha kupitisha kanuni hizo kilichoandaliwa na  kamati hiyo Mwakilishi wa sheha ambae pia ni Mratibu wa kamati ya maadili ya shehia hiyo Abrahman Mohamed Khamis alisema, Ofisi ya sheha ipo tayari kushirikiana na wanakijiji  katika kusimamia kanuni hizo.

Alisema ni vyema wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa kamati hiyo, ili lengo liweze kufanikiwa, huku akiwataka wanakamati hao iwapo patakua na kikwazo chochote katika utekelezaji majukumu yao, kupeleka changamoto zao kwa sheha.

"Ofisi ya sheha ipo tayari kushirikiana na nyinyi katika hili, naomba na wananchi mutoe ushirikiano wa kutosha ili kufanikisha jambo hili, na iwapo patatokezea kikwazo  katika utendaji kazi wenu musisite kuripoti kwa sheha", alieleza.

Nae Mjumbe wa Sheha wa Shehia ya Chumbageni Juma Shaaban Jabir alisema, hatua iliyochukuliwa na wanakikijiji hao, ni nzuri kwani itasaidia kutatua changamoto za kimaadili katika shehia yao, huku akisisitiza kamati hiyo kua endelevu.

Aliongeza kua huenda kijiji hicho kikawa mfano nzuri na wakuigwa ndani ya shehia hiyo na hata shehia nyingine, huku akitoa wito kwa kamati hiyo kuweka pembeni itikadi zao za kisiasa na badala yake wafanye kazi kwa maslahi ya kijiji hicho.

Akizungumza katika kikao hicho  Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la polisi  Abdallah Mohamed Abdallah alisema, iwapo mtu yeyote atapingana na kanuni hizo kwa makusudi, ni vyema kamati kumripoti kwa kwao, kwa lengo la kuchukuliwa hatua zaidi, huku akiitaka jamii kutoa mashirikiano ya kutosha kwa jeshi hilo.


Nae Mwenyekiti wa kamati hiyo Machano Ali Makame, alipongeza ushirikiano wanaoupata kutoka kwa jamii na uongozi wa shehia, ambapo alifafanua kua tokea kuanza kamati hiyo wanafunzi 25 wameanza kusoma, baada ya kupewa vitabu vya aina tofauti vikiwemo vya kumjua Muumba wao kutoka katika kamati hiyo.

Akisoma kanuni 19 zilizopitishwa katika kikao hicho Mshauri Eelekezi wa kamati hiyo Haji Nassor Mohamed alisema, kanuni hizo ni pamoja na marufuku ya kutembea usiku zaidi ya saa nne kwa asiekua na dharura, marufuku ya ukataji nywele usio zingatia maadili pamoja na uvaaji nguo za mbano.





Huku kanuni nyengine zikiwa ni marufuku ya uvutaji sigara, unywaji  pombe na madawa ya kulevya, upigaji ngoma ovyo pamoja na kanuni inayotaka futarisho kwa wanakijiji kila mwaka mara moja kwa lengo la kuwaunganisha.

Kamati ya maadili na taatuma ya kijiji cha Kidutani shehia ya Chumbageni,  ilioanzishwa mienzi minne iliopita, ikiwa na wajumbe 12 wakiwemo wanaume na wanawake, na imepitisha kanuni 19 itakazozisimamia katika utendaji kazi wake, ambazo zitasainiwa na sheha wa shehia hiyo, Kamanda wa polisi wa Wilaya ya Mkoani pamoja na Mkuu wa wilaya hiyo.

                                                                MWISHO

 

 

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...