Skip to main content

MWANAIDI HAMAD: MGOMBEA 'AFP' ANAEPAMBANIA KUTATUA KERO KOJANI


 


IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ 

 

MWAKA 2025 ni mwaka ambao wanawake wengi wamejitupa jimboni kuwania nafasi mbali mbali za uongozi.

 

Hii inaoneshea dhahir kwamba, sasa jamii imepata uwelewa juu ya masuala ya uongozi kwa wanawake na ndio maana wakachaguliwa kwenye kura za maoni, ili kusudi waingie katika mchakato wa kugombea.

 

Imeonekana kuwa, wanawake wapo imara na waaminifu katika kutekeleza yale wanayoyaahidi kwa wananchi kwa lengo la kuipatia maendeleo jamii iliyowazunguka.

 

Tayari wamefikia hatua ya kuingia jimboni kugombea, lililobaki ni kusubiri siku ya uchaguzi ili wachaguliwe kuingia kwenye vyombo vya maamuzi, kwa ajili ya kuwasilisha kero za wananchi na kupatiwa ufumbuzi unaofaa.

 

Mwanaidi Hamad Rashid mwenye umri wa miaka 39 mkaazi wa Kitambuu Wilaya ya Wete, ni mmoja kati ya wanawake waliojitupa majimboni kuwania nafasi za uongozi kwa lengo la kuleta mafanikio kwenye maeneo yake.

 

Ni mgombea uwakilishi Jimbo la Kojani kupitia chama cha Wakulima (AFP) ambae ni mara ya kwanza kugombea na kufanikiwa kuingia katika mchakato wa uchaguzi.

 

Mgombea huyo hakuwa na ndoto za kuwa kiongozi hapo awali, ingawa alipoona sasa jamii inamkubali mwanamke kuwa kiongozi, ndipo alipoona kuna haja kugombea ili aweze kutatua kero zilizomo kwenye Jimbo lao.

 

"Kuna changamoto mbali mbali zinazotaka ufumbuzi, hasa zinazotukwanza wanawake na watoto wetu, lakini sikuwa na njia ya kuzisemea, ndio nikaona ili nipate sehemu ya kuziwasilisha ni vyema nigombee uwakilishi," anaeleza.

 

Mwanaidi ana imani kwamba wananchi wa Jimbo lake watamchagua kwenye kuwawakilisha katika chombo cha kutoa maamuzi, kwani wameona wameshapata mtetezi.

 

Anasema, wananchi wa Jimbo lake wanampa pongezi nyingi kwa hatua aliyoichukua kwani ameoneshwa uthubutu wa kutaka kuwaletea maendeleo katika Jimbo lao.

 

"Wananchi sasa wanataka maendeleo, hivyo wanachagua mtu ambae atawaletea maendeleo, ndio maana nikaamua kuingia kwenye mchakato ili niwatimizie lengo lao" anafahamisha.

 

Mgombea huyo anaeleza, anafanya mikutano ya kampeni sambamba na kupiga kampeni za nyumba kwa nyumba ili kuhakikisha anapigiwa kura ya ndio ifikapo Oktoba 29 mwaka huu.

 

Anasema, atakapofanikiwa kushika nafasi hiyo ya uwakilishi, atazidisha ushirikiano na wananchi kwani itakuwa ameshabeba dhamana nzito, hivyo atahakikisha lile lengo la kutatua kero za jamii na kuleta maendeleo linakamilika kwa haraka.

 

Atazitumia pesa za mfuko wa Jimbo katika kuboresha na kuleta mabadiliko ya kimaendeleo kwenye Jimbo lao, ili wananchi wanufaike na fedha hizo ambazo zinaletwa makusudi kwa ajili ya kuendesha shughuli za huduma za kijamii.

 

"Nitakuwa tayari muda wote, nitatatua changamoto zinazowakabili wananchi wa Jimbo langu, hivyo naomba wanichague, kwani neema ipo njiani," anaeleza.


Mwanaidi anawaambia wananchi wa Jimbo hilo watarajie mazuri kwani wamepata kiongozi bora, anaejali maslahi ya jamii, hivyo atawathamini sana.

 

Atatekeleza vyema majukumu yake ya kazi bila kuathiri majukumu ya kifamilia, hiyo italeta thamani kubwa kwake na kuwa mfano kwa jamii iliyomzunguka hasa kwa wale wenye mawazo hasi kwamba mwanamke hawezi kuongoza.

 

Anafafanua kuwa, elimu ya uongozi hajawahi kupata sehemu yeyote, isipokuwa baada ya kupita kwenye kura za maoni, wagombea wote waliitwa na Tume ya Uchaguzi Zanzibar kupatiwa mafunzo, ambapo na yeye alipata nafasi hiyo.

 

"Lakini kupitia vyombo vya habari nilikuwa nilisikia kuhusu umuhimu wa mwanamke kuongoza na ndio maana nilipoona jamii sasa imebadilika kwa kupata uwelewa na mimi nisiwe nyuma kwenye hilo," anafafanua.

 

Anawaomba wananchi wazidishe ushirikiano kwake na wamchague ili apate nafasi ya kwenda kuwatetea kwenye chombo cha maamuzi.

 

Mwanaidi alikuwa mwanachama wa kawaida tangu alipojiunga na chama hicho mwaka 2001 akiwa kidato cha nne na hakuwahi kushika nafasi yeyote ya uongozi.

 

"Harakati za kusaka uongozi nimeanza mwaka huu wa 2025 na ndio nimebahatika kuingia kwenye mchakato, namshukuru sana Mungu kwa kunijaalia hii nafasi," anasema.

 

Mgombea huyo anaeleza, tangu ajiunge na chama hicho hajawahi kupata changamoto yeyote na hata hapo alipogombea pia, hiyo ni kuonyesha wazi kwamba sasa elimu ya uongozi kwa wanawake tayari imeshawaingia akilini wananchi.

 

Mtu wa karibu wa mgombea huyo, Farida Juma Khamis anasema mwanaidi ni mwanachama mwenzake wa muda mrefu ambae wanashirikiana kwa hali na mali katika kukijenga chama chao.

 

Anasema, mgombea huyo hajawahi kushika nafasi yeyote ya uongozi ingawa mwaka huu amepata mwamko wa kugombea na hasa kwa vile chama chao kinatoa fursa kwa wanachama wote.

 

"Naamini atakapofanikiwa kuwa mwakilishi atatekeleza vizuri majukumu yake katika Jimbo na kuhakikisha analiletea maendeleo, pia chama chetu kimesema kitasimama imara kuhakikisha atakaefanikiwa anatimiza ahadi alizoziweka kwa wananchi wakati wa kuomba kura, hivyo kupitia msukumo huu atafanya wajibu wake vizuri," anaelezea.

 

Farida amlisisitiza Mwanaidi kuwa, atakapofanikiwa kuwa mwakilishi basi zile siku ambazo vikao vya Baraza vitafungwa, arudi kwa wananchi kusikiliza kero zao, ili atakaporudi aziwasilishe, hiyo itamfanya aaminike zaidi na mara nyengine apite jimboni bila kupingwa.

 

 

Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Kaskazini Pemba Raya Juma Othman anasema, mgombea huyo yupo vizuri katika kutekeleza majukumu yake ya kazi, hivyo atakapofanikiwa kupata nafasi hiyo ahakikishe anatimiza ahadi alizoziweka kwenye kampeni.

 

"Mpango wa chama chetu ikiwa wagombea wote watakafanikiwa, watahakikisha wanaleta mafanikio kwenye majimbo yao, kwa sababu tutakuwa nao bega kwa bega na kumuelekeza, hivyo hatowasahau waliomchagua," anasema Mwenyekiti huyo.

 

Alimuomba mgombea huyo, akifanikiwa kuwa mwakilishi awe anaejali maslahi ya wananchi wake na ikiwa atakosa basi asivunjike moyo, kwani chama kipo pamoja nae na kitampa msukumo itakapofika uchaguzi mwengine wa mwaka 20230.

 

Mgombea huyo ameolewa na ana watoto watano, ambapo ana elimu ya kidato cha nne aliyosoma katika skuli ya Secondari ya Fidel Castro.

 

                            MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...