Skip to main content

KAMPENI ZA KISIASA MAJI MTUNGINI, WALIO NJE YA PEMBA HAWAAMINI MASIKIO YAO

 


NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

ACHA kufukua makaburi, kujua yaliopita kwa siasa za Pemba.

 

Maana chaguzi sita za vyama vingi, zilizokwishapita, ukiamua kufuakua makaburi, wapo watakolia, watakaofuta machozi na wingine kupoteza fahamu.

 

Acha kabisa, kuuliza, kufungua ripoti, kusaka takwimu, kuingia kwenye mitandao ya kijamii au kusililiza rikodi, za maovu yaliopita.

 

Wewe jua tu, kuwa taifa la Tanzania tokea pale lilipofanya uchaguzi wa kwanza mwaka 1995, sasa linaingia uchaguzi mkuu wa saba Oktoba 29, mwaka huu.

 Narejea tena, acha kabisa kutaka kujua siasa za Pemba, jinsi zilivyokuwa na nguvu hadi kupindukia mipaka, tena ndani miezi kama hii ya kmapeni.


SIASA ZA MWAKA HUU ZINATOFAUTI GANI?

Juzi nilishuhudia siasa za kiungwana, kistaarabu na za kisheria, kwa wafusia wa vyama vya CCM kubishana kwa hoja za sera, na wenzao wa ACT-Wazalendo.

 

‘’Huyu Dk. Mwinyi anafaa, maana kwanza ni daktari atawafanyia uchunguuzi na kisha kuwatibu nyote ACT-,’’ni maneno ya kisera kutoka kwa wanaccm wa Chambani Mkoani.

 

Ali Khamis Juma, aliwaamba wafuasia wa ACT-Wazalendo kuwa, wampe tu kura Dk. Mwinyi, maana ameshafanya mingi, ili pate kuyaendeleza.

 

Asha Said Khalfan nae wa CCM, aliwataka wafuasi wote wa vyama vyingine, kubakia na vyama vyao, lakini kura kumpa Dk. Mwinyi.

 



Utani huo, wa sera huku kila mmoja akiwa na picha za mgombea wake, ghafla wafuasi wa ACT-Wazalendo, nao walijibu kwa kumnadi mgombea, wao kiaina.

 

‘’Jamani kila kitu cha nchi hii, kinaendeshwa kwa mujibu wa sheria, sasa nyinyi CCM mnashindwaje kumpigia kura baba OMO,’’alihoji Hija Kombo Ali wa Mgagadu.

 

Yeye ni mfuasi wa ACT-Wazalendo, akawanadia sera wafuasi wa CCM, waliokuwa wakiwasubiri wenzao, kuelekea kwenye uzinduzi wa kampeni Jimbo la Kiwani.

 

‘’Si mnamuona kwenye picha alivyopendeza, na huyu ni mwanasheria nguli na dunia inamjua, mnashindwa nini kumpigia kura, ili tuongozwe kisheria,’’alihoji.

 

Mafunda Hamad Juma nae mfuasi wa ACT, alisema wagombea wote ni wazuri, ingawa anayetoka kwenye chama chao, ni mzuri zaidi na ana haiba ya kuwa raisi.

 

Hayo, yalikuwa madogo, eneo la Ukutini wafuasi wa ACT-Wazalendo wao walitangaaza sera za chama chao, kwa mtindo wa kunyanyua picha juu kwa pamoja.

 

Huku wanaccm nao, walitumia picha wagombea wao na kuonesha ishara ya mitano tena, kwa Dk. Mwinyi na kumtaja mama Samia, kuwa anatosha.

 

Kijana Said Juma Omar wa Ngwachani, anasema siasa za kushindanisha sera na uzuri wa picha za mgombea kwa Pemba, ni ishara nzuri.



 


‘’Maana tulishazoea ikifika mwezi mmoja kabla ya uchaguzi mkuu, kisiwa cha Pemba, huwa mshike mshike na kujaa na woga hata chumbani mwako,’’anasema.

 

Maryam Haji Mohamed wa Wawi, anasema kwa sasa hali ya Pemba, iko shuwari kama vile hakuna uchaguzi mkuu siku chache zijazo.

 

‘’Kinachonifurahisha ni kuona, mwaka huu uchaguzi huwenda ukawa mwepesi kiamani, na kila mmoja kuvaa sare ya chama chake, bila ya hofu,’’anasema.

 

Leila Hassan Hija wa Pujini, anasema sasa unifomu za vyama, hazionekani tena kama ni uadui, bali ni nguo kama zilivyo nyingine.

 

Adam Said Hamad wa Mchanga mdogo, anasema kwa sasa, hakuna tena maskani za vyama, ambazo zinapiga marufuku wafuasi wa vyama vingine, kupiga soga.

 

‘’Hapa kwetu tunaangalia tv katika banda lolote la vyama, na hata kama utavaa sare za CCM unaingia kwa ACT na yeye anaingia kwa CUF,’’anasema.

 







WENYE MAMLAKA

August 20, mwaka huu ndani ya ukumbi wa Manispaa Chake chake, Jeshi la Polisi Zanzibar lilikutana na waandishi wahabari, likiwataka kuhakikisha kalamu zao, hazizai chuki.

 

Kamishina wa Polisi Zanzibar ‘CP’ Kombo Khamis Kombo, akasema inawezekana kufanyika kwa kampeni na wafuasia kubaki na vyama na sera zao, bila uvunjifu wa amani.

 

‘’Katika kutunza amani hasa kipindi cha kabla, wakati na baada ya uchaguzi, kila mmoja ana nafasi ya kuondoa viasharia vya uvunjifu wa amani, mkiwemo waandishi wa habari,’’alisisitiza.

 

Waandishi wa habari wenyewe, Septamba 15, mwaka huu walishauriwa kutumia kalamu na vipaza sauti vyao vizuri, kutangaza habari, zinazohusiana na uchaguzi, kwa lengo la kulinda amani.


 



Aliyewapa kauli hii, alikuwa ni Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar Thabit Idarous Faina, wakati alipokuwa akitoa mafunzo kwao, kwa lengo la kuwajengea uwezo, juu ya usambazaji wa habari bora.

 Akasema, inawezekana mno, wagombea na wafuasi wa wakatuliza mkunkari wa kisasa, na kufanyika kwa kampeni za kiungwa na kistaarabu.

 

‘’Kalama za waandishi na hasa wanaotumia mitandao ya kijamii, zinaweza kuwa chanzo kikuzuri cha kutuliza jazba na wafuasi wakashindanisha sera,’’alisema.

 

Hata wanawake waliotia nia kutoka vyama vya siasa, kumbe nao walishauriwa kunadi sera za vyama vyao, sio matusi.


Maana Mkurugenzi wa mradi wa kuwawezesha wanawake katika masuala ya uongozi na demokrasi kutoka PEGAO, Hafidh Abdi Said, alisema machafuko na vurugu, sio utamaduni wa Zanzibar.




 


WAGOMBEA

Septemba13, mwaka huu mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya ACT -Wazalendo Othman Massoud Othman, kwenye uzinduzi wa kampeni Tibirinzi, alitaka kwanza amani itawale.

 

‘’Kwanza amani na kisha ndio chama, maana kinyume chake, hakutatawalika, hakutohesabika kura na wala hizi kampeni hazitofanyika,’’alisema.

 

Hata mgombea urais wa Zanzibar, kutoka ADA-TADEA Juma Ali Khatib, amesona sio busara kwa wafuasi wake, kujibu mashambulizi.

 

‘’Nyinyi msikubali kuchokozeka, na kuiacha Pemba hii kuwa na uvunjifu wa amani, maana athari yake huwapata wanawake na watoto,’’aliwakumbusha.

 

Jambo kama hili, liligusiwa na mgombea urais wa Chama cha ‘ADC’ Hamad Rashid Mohamed, kwa kuwataka wanachama wa vyama vya siasa, kuondokana fujo zinazopelekea madhara kwa sababu tu ya siasa.

 

Huwenda wananchi wa Pemba, kwa kukumbuka madhara ya kisasa ya chaguzi sita zilizopita, na ndio maana leo, tukiwa ndani ya siku zisizidi 25, Pemba ni shuwari.

 

Kwani wagombea kadiri wote, pamoja na kunadi sera, lakini jambo la kuomba amani na utulivu, kama vile ni lazima kulitaja na kulisisitiza.

 

Kwani hata mgombea urais Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha NRA, Khamis Faki Mgau, nae alishasema wazi kuwa, suala la amani ndio kipaumbele chake.

 

‘’Kwanza amani, pili amani, tatu amani kisha ndio chama changu, maana nimepanda ya juu ya jukwaa kwa amani iliyopo,’’anasisitiza.

 

Kwenye kampeni za CCM uwanja wa Gombani Chake chake, mgombea uraisi wa Zanzibar, Dk. Hussein Ali Mwinyi, akawatoa hofu wananchi juu ya amani.

 

‘’Nendeni mkakipigie kura CCM, Oktoba 29, mwaka huu na msiwe na hofu yoyote ya vunjifu wa amani, kwani ndio hazina yetu,’’anasema.

 

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassana, alilirejea neno la kutunza amani, akisema vikosi vipo kwa kazi hiyo.

 

 VIONGOZI WA DINI

Sheikh Said Ahmana Mohamed, kutoka Ofisi ya Mufti, akawakumbusha wagombea, kwamba wasikubali kuwa sehemu ya machafuko, watabeba dhima kwa Muumba.

 

‘’Tumia ulimi wako, maneno yako, mdomo wako na maarifa yako, kutowagombanisha watu, wala kuwaingiza kwenye madhara, likitokezea unabeba dhima,’’aliwakumbusha.

 

Mseminari kutoka Kanisa Katoliki ‘RC’ Barnabas, alisema kwenye kongamano la amani Mkoani, kuwa kanisa haliridhishwi na uwepo wa fujo.

 

‘’Fujo, uvinjifu wa amani, vita havina mwisho mzuri kwa wananchi, na ndio maana tunataka amani kwanza, kisha mingine,’’anasema.

 

NYARAKA

Katiba ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzani, Ibara yake ya 26, ikifafanua haki kwa wananchi wa kutii sheria za nchi, kama ilivyo ya Zanzibar ya mwaka 1984, kifungu cha 23, kikisitiza wajibu wa kulinda mali.

 

Ibara ya 29 ya Mkataba wa kimataifa wa haki za watu wenye ulemavu, inayataka mataifa kuhakikisha kuwa, watu wenye ulemavu wanashiriki kwa ukamilifu katika medani ya siasa kwa amani.

 

‘’Kulinda haki ya watu wenye ulemavu, kupiga kura kwa siri wakati wa uchaguzi na bila kudhalilishwa, kuchukua dhamana za uongozi na kutekeleza masuala yote ya umma, katika ngazi zote za  serikali,’’unafafanua mkataba huo.

 

Sheria ya Watu wenye Ulemavu nambari 8 ya mwaka 2022, kifungu cha 28 (1),(e), kikisisitiza haki kadhaa kwa watu hao, ikiwemo ya kisisasa bila ya kubaguliwa.

 

Ndio maana, sheria ya Uchaguzi nambari 4 ya mwaka 2018, kifungu cha 63 (3), kikabainisha kuwa, kampeni zitafanyika hata kwa njia ya misafara ya vyombo vya moto na mkutano, kwa amani.

 

Kanuni za maadili ya uchaguzi ya mwaka 2025, Ibara ya 16, (1), kimepiga marufuku kwa kiongozi wa chama, mwanachama, mshabiki, mfuasi wa chama kufanya fujo na vitendo, vya hujuma katika kampeni.

 

Kanuni hizi zinafafanua kua, ni kosa kuharibu mwenendo wa uchaguzi na kampeni za wagombea wengine, pamoja na kufanya vitendo vinavyopelekea kuibua chuki, vitisho, fujo, udhalilishaji wa makundi maalumu katika kutekeleza malengo ya kisiasa.

                        Mwisho   

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...