Skip to main content

ALIEPITWA KWA KURA MOJA 2020 AIBUKA MSHIDI 2025 KURA ZA MAONI

 

 


'Anasema mwaka huu ndio aliopangiwa na Mungu kuingia jimboni kugombea, ...awaomba wananchi kumchagua'

 

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

 

"Alienipita kwa kura moja 2020, nimempita kwa kura 62 kwenye kura za maoni mwaka huu 2025, hivyo nimeshinda kwa kishindo,"

 

Maneno hayo ya furaha yalimtoka mgombea uwakilishi Jimbo la Tumbe kupitia chama cha Mapinduzi CCM Salma Khamis Tumu wakati akizungumza na mwandishi wa makala hii huko kijiji kwao.

 

Salma mwenye umri wa miaka 53 mkaazi wa shehia ya Tumbe Magharibi anasema, ameamini kwamba riziki ya mtu haiendi kwa mwengine bali siku ikifika, itamfika tu mwenyewe.

 

Pamoja na kushindwa kwenye kura za maoni kwenye uchaguzi uliopita wa mwaka 2020, lakini hakukata tamaa bali ajijipanga kugombea tena 2025, ambapo alipitishwa kwa kura 134 huku mpinzani wake ambae ni mwanamme akijipatia kura 72.

 

Mgombea huyo anasema, hizo ni baraka za Mungu kumjaalia kupita kwenye nafasi hiyo, hivyo amewaomba wananchi wamchague ili awaletee maendeleo katika Jimbo lao.

 

"Nawashukuru sana wajumbe kwa kuona umuhimu wangu wa kunichagua, nawaahidi kushirikiana nao bega kwa bega kuhakikisha Jimbo letu linakuwa la mfano katika kulipatia maendeleo kwa haraka," anasema.

 

Anasema, mwaka 2015/2020 aliwahi kushika nafasi ya udiwani na kuwaletea maendeleo wananchi wa Jimbo lake kulingana na uwezo wake, hivyo basi atakapochaguliwa kuwa mwakilishi atahakikisha analeta maendeleo zaidi, kwani atazitumia vizuri pesa za mfuko wa Jimbo, kuwanufaisha wananchi.

 


Alipokuwa diwani, Salma alijenga mnara wa kuweka tangi la maji katika skuli ya msingi Tumbe pamoja na kusaidia fedha kwa ajili ya kuunga umeme, hivyo amekuwa akisaidia kutoa mchango wa hali na mali pale panapohitajika.

 

"Nilitoa fedha zangu mfukoni kutekeleza hayo, lakini pia nilikuwa naibua changamoto mbali mbali na kuzifikisha sehemu husika kwa ajili ya kutatuliwa, hivyo tulikuwa tunashirikiana na mbunge na mwakilishi kuzitatua," anaeleza mgombea huyo.

 

Anasema, juhudi alizokuwa akizichukuwa alipokuwa diwani katika kuwafikishia wananchi huduma bora, ndizo ambazo atazitumia wakati atakapopata nafasi ya uwakilishi, kwani amejipanga kutekeleza mambo mbali mbali kuhakikisha changamoto zote za Jimbo zinamaliza.

 

Amejipanga kujenga vyoo kwenye skuli mpya ya msingi ya Tumbe, ili watoto waanze kuitumia kujipatia elimu,  jambo ambalo litwapunguzia masafa makubwa ambayo ni kikwazo kwao hasa ukizingatia ni wadogo.

 

"Skuli hiyo ilianza kujengewa kwa nguvu za wananchi wakisaidiwa na viongozi wa majimbo pamoja na Serikali, lakini kwa sasa inahitaji vyoo ili ianze kutumika, hivyo nikichaguliwa nitajenga vyoo watoto wapate kusoma karibu, kwani skuli wanayosoma ni mbali," anasema.

 

Mgombea anafafanua, Ilani ya chama cha Mapinduzi CCM imeeleza, itajenga hospitali ya kisasa kwenye Jimbo lao, hivyo atakapokuwa kiongozi atalisimamia hilo kuona kwamba inajengwa kwa ajili ya kuwapatia huduma bora wananchi.

 

Atahakikisha pia kinajengwa kituo cha mafunzo ya Amali ili vijana wajiendeleze kielimu, hali itakayowasaidia kupata ajira, kwani kiwanja kipo kimeshapimwa kwa ajili ya ujenzi na Serikali imeahidi kukijenga kituo hicho.

 

"Sitowaacha nyuma wanawake katika kupata haki zao za msingi sambamba na kuwasimamia watoto wasitelekezwe, kwani ndio chanzo cha kudhalilishwa na kukosa huduma zao za msingi," anaeleza.

 


Salma amejipanga kuhakikisha vikindi vya ushirika vinapata mikopo ya kujiendeleza kiuchumi huku akikusudia kuwasimamia watu wenye ulemavu kupata haki zao stahiki na kupata huduma bora na rahisi popote wanapohitaji huduma za kijamii.

 

Vile vile anafafanua kuwa, Dk. Hussein Ali Mwinyi ametoa ahadi ya kuwanunulia boti wavuvi ili wajipatie kipato, hivyo atakapofanikiwa kuwa mwakilishi atalikumbushia suala hilo mara kwa mara kwa ajili ya kutekelezwa na wapate kuendeleza na shughuli zao za uvuvi bila kikwazo.

 

Anawataka wananchi wa Tumbe wazidishe imani kwake na wamchague, kwani amejipanga kuwatatulia changamoto zote zinazowakabili ikiwemo ukosefu maji safi na salama, ambayo bado ni tatizo kwa baadhi ya vijiji.

 

"Wananchi watarajie mazuri baada ya kunichagua kwani nitashirikiana na viongozi wangu wa Serikali katika kuhakikisha tunamalizia kero zote kwenye Jimbo letu," anasema.

 

Anawaomba wananchi kwenda kumpigia kura yeye pamoja na viongozi wengine wa chama chao ifikapo Oktoba 29, ili wapate kuongoza na kuwaletea maendeleo katika nchi.

 

Mgombea huyo anasema ameshawahi kushika nafasi mbali mbali za uongozi baada ya kujiunga na chama hicho mwaka 1992, ambapo alianza kuwa Katibu wa CCM tawi la Tumbe na pia kuwa Katibu wa UWT Jimbo la Tumbe.

 

"Pia nilipokuwa diwani nilikuwa Makamo Mwenyekiti Halmashauri ya Wilaya ya Micheweni kwenye Baraza la Madiwani na nafasi hizo niligombea na kufanikiwa," anaeleza.

 

Kupitia nafasi hizo alizozisimamia, mgombea huyo uwakilishi zimemjenga ujasiri na uthubutu wa kusimama na kuweza kuongea, hali iliyomfanya aendelee kugombea nafasi za juu za uongozi ili apate kuwatetea wananchi, kwa ajili ya kupata maendeleo katika maeneo yao wanayoishi.

 

Mume wa mgombea huyo, Ali Kombo Hindi anamuelezea mke wake kuwa ni mpambanaji na anatekeleza majukumu yake vizuri katika nyadhifa zote alizowahi kuzisimamia, hivyo anaamini na hiyo nafasi ya uwakilishi ataisimamia vizuri.

 

"Kwa kweli tangu aingie kwenye harakati za uongozi mke wangu anatekeleza wajibu wake vizuri na nina hakika akifanikiwa kuwa mwakilishi ataliletea maendeleo Jimbo letu," anaeleza.

 

Anasema kuwa, suala la uongozi kwa wanawake ni muhimu sana kwani wana huruma na waoga, hivyo wanajitahidi kutekeleza yale yanayoyakiwa katika kuhakikisha jamii inakuwa bora na yenye maendeleo.

 

"Katika familia tunampa ushirikiano mkubwa na ndio maana akapata ujasiri wa kusimama na kuingia jimboni kugombea, tutaendelea kumuunga mkono ili afanikiwe," anasema baba huyo.

 

Katibu wa CCM Jimbo la Tumbe Mohamed Mwewe Omar anamfahamu mgombea huyo kuwa ni mwanaharakati wa shughuli mbali mbali za kimaendeleo, kijamii na kisiasa na ameshashika nafasi mbali mbali za uongozi wa kuchaguliwa pamoja na kuteuliwa.

 

Mohamed anamuelezea Salma kuwa ni mwanamke anaejitolea, anaependa kushiriki na kushirikishwa, hivyo atakapopata nafasi hiyo ya uwakilishi itakuwa ni chachu ya maendeleo katika Jimbo lao na nchi kwa ujumla.

 

"Tumemuona katika nyadhifa alizosimamia mwanzo, alitekeleza ipasavyo majukumu yake na kusimamia kero kwa ajili ya kupatiwa ufumbuzi," anafahamisha Katibu huyo.

 

Katibu huyo anamtaka mgombea huyo, atakapopata dhima ya kulisimamia Jimbo baada ya kuchaguliwa kwenye uchaguzi mkuu, ajitahidi kutekeleza yale yote aliyowaahidi wananchi kipindi cha kampeni, kwani muungwana ni vitendo, hivyo inatakiwa vitendo vionekane.

 

"Pia akubali kushauriwa kwani ushauri ni njia muhimu ya kufikia mafanikio," anaeleza.

 

Salma ameolewa na ana watoto na wajukuu, ambapo harakati zake za kuongoza zilianzia mwaka 1992 mara tu baada ya kujiunga na chama.

 

Mgombea huyo ametekekeza haki yake ya kushiriki katika demokrasia na uongozi, kama Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1964 ilivyoeleza kwenye kifungu cha 21 (2) cha na kifungu cha 67 (1) cha Katiba hiyo kama ilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2010.

 

                       MWISHO.

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...