Skip to main content

CHUMU JUMA ABDALLAH: ANAYEINUA SAUTI YA WANAWAKE KATIKA UONGOZI

 



Na AMRAT KOMBO , ZANZIBAR @@@
Kwa miaka mingi, siasa imekuwa ikitazamwa kama uwanja wa wanaume. Lakini kwa Chumu Juma Abdallah, mwanamke mwenye umri wa miaka 40, mtazamo huo unabadilika taratibu, Kutoka kuwa kijana aliyekuwa na shaka ya uwezo wake.

 leo amekuwa kiongozi anayetazamwa kwa heshima, akigombea Uwakilishi wa Viti Maalum na nafasi ya Makamu Mwenyekiti Taifa wa Chama cha Alliance for African Federal Party (AAFP) kwa upande wa Zanzibar.

“Nilianza nikiwa ninaogopa, nikiamini siwezi, lakini viongozi wangu walinipa moyo. Waliniambia ninaweza, nami nikaamua kuthibitisha,” Amesema Chumu.

Safari ya Chumu kielimu ilianza mwaka 1990 katika Skuli ya Msingi Hurumzi, kisha akaendelea na Skuli ya Sekondari Hamamni mwaka 2000. Mwaka 2002, alijiunga na Chuo cha Muslimu Mazizini, hatua aliyosema ilimsaidia kujijenga katika maadili na kujiamini.

Akiwa mtoto wa nne kati ya watoto nane wa Mzee Abdallah, Chumu anakumbuka jinsi wazazi wake walivyokuwa na mashaka kuhusu azma yake ya kuingia kwenye siasa.

“Mwanzoni hawakuamini, lakini walipoona jinsi ninavyopambana kwa nidhamu na bidii, wakaanza kuniunga mkono,” Amesema Chumu.

Mwaka 2009, akiwa kijana wa miaka 24, ndipo maisha yake ya kisiasa yalipoanza kwa bahati. Alivutwa na hamasa ya wananchi na wanachama wa Alliance for African Federal Party (AAFP) waliovutiwa na ujasiri wake wa kuzungumza kwa hoja.

Chumu alianza kama mjumbe wa kawaida, kisha akapanda ngazi hadi Naibu Katibu Mkuu wa AAFP upande wa Zanzibar, baadaye Makamu wa Wajumbe wa Kina Mama wa chama hicho. Leo, anatafuta nafasi mbili kubwa zinazohitaji uzoefu, busara, na moyo wa utumishi , Uwakilishi wa Viti Maalum na Makamu Mwenyekiti Taifa wa chama kwa upande wa Zanzibar.

“Nafasi hizi mbili ni jukumu kubwa, lakini naamini ninaweza. Si kwa maneno, bali kwa matendo,”Amesema Chumu.

Mbali na siasa, Chumu amejitolea sana katika jamii, hasa katika kuinua wanawake na vijana. Kupitia mafunzo kutoka TAMWA–Zanzibar na semina za chama chake, amekuwa mstari wa mbele kuwajengea uwezo wanawake katika ujasiriamali na uongozi.

“Mafunzo yamenifundisha kuona thamani ya mwanamke na nguvu ya kijana. Kila mmoja ana mchango mkubwa katika kujenga taifa,” Amesema Chumu 

Kwa moyo huo wa kujitolea, aliunda kikundi cha kikoba cha vijana 25 wanawake na wanaume kwa lengo la kuweka akiba bila riba na kuanzisha biashara ndogo ndogo.

“Nilitaka vijana wajifunze kuweka na kuwekeza. Leo, wengi wao wana biashara zao, jambo linalonipa faraja kubwa,” Amasema Chumu.

Chumu hakufika alipo bila changamoto. Anakiri kukutana na upinzani, mitazamo hasi, na maneno ya kubezwa hasa kutokana na kuwa mwanamke ndani ya chama cha upinzani.




“Kuna waliokuwa wananiona kama msaliti kwa sababu chama changu si tawala. Lakini mimi naamini katika kushirikiana kwa maendeleo ya nchi,” Amesema Chumu.

Kwa mtazamo wake, siasa siyo vita, bali ni jukwaa la mijadala ya kimaendeleo. Ndiyo maana anaamini uongozi lazima ujengwe katika misingi ya uwazi, ushirikishwaji na uwajibikaji.

Kama atapata fursa ya kutumikia nafasi anazogombea, Chumu ana mipango thabiti ya kuimarisha ushiriki wa wanawake na vijana katika maendeleo ya nchi.
 
Anasema malengo yake ni Kuelimisha wanawake kuwa siasa si ya wanaume pekee. Kukuza programu za mafunzo ya uongozi na ujasiriamali kwa vijana na wanawake.

“ kuanzisha vikundi vya kijamii vyenye mikopo isiyo na riba , Kuimarisha uongozi wa uwajibikaji, pamoja na wanawake , vijana nao wajue kuwa kuongoza hakuhitaji umri mkubwa, bali moyo wa kuhudumia watu.” Amesema Chumu

Ali Hassan Mussa, Katibu Mwenenzi wa Alliance for African Federal Party (AAFP), amesema ni kiongozi mwenye maono na moyo wa kujituma.

“ Chumu ni kijana mchapakazi asiogopa changamoto yoyote, ameanza kushiriki kwenye siasa akiwa mdogo , tumemuamini sana kutokana na juhudi zake na anaweza kufika mbali akiendelea na mapambano yake bila ya kukataa tamaa.” Amesema Chumu



Khamis Ali, mkazi wa Fuoni, naye amesema anapendezwa na uongozi wa mgombea huyo kwani ni mchapakazi na mwenye kujitambua .

“ Chumu ni mfano wa mwanamke mwenye uthubutu, anayejituma bila kuchoka. Tumejifunza mengi kwake na anapenda kuona vijana tunajituma.” 

Naye Moza Said ambae ni mwanachama wa Alliance for African Federal Party (AAFP), amesema anapenda kuona mwanamke mwenziwe anashika nyazifa mbalimbali , kwani inamuhamasisha na yeye kushiriki katika nafasi za uongozi.

‘‘Napenda jinsi anavyojiamini na kujituma,anaonesha kuwa bora kwenye uongozi wake , hii inanifanya nami kupenda kushiriki katika nafasi za uongozi.” Amesema Moza

Licha ya majukumu mengi ya kisiasa, Chumu amesema amejifunza kuweka uwiano kati ya familia na kazi za chama.

“Ninatenga muda wa familia yangu, kwa sababu mafanikio ya kazi yanahitaji utulivu wa nyumbani,” Amesema Chumu.

Amesema anatamani kuwa kioo cha wanawake wenzake, akiwapa matumaini kuwa mafanikio yanaanza kwa kuamini ndani yako.

“Natamani siku moja wanawake waje kusema, nataka kuwa kama Chumu. Hapo nitajua juhudi zangu hazijapotea.”
              MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...