Skip to main content

IDADI YA WANAWAKE WATIA NIA NAFASI ZA UONGOZI UCHAGUZI 2025, YAWA TOFAUTI NA YA 2020

 



Na Amrat Kombo, Zanzibar @@@@

UPEPO wa mabadiliko unaendelea kuvuma katika siasa za Zanzibar, safari hii ukivumisha na sauti ya mwanamke. 
Kadri Uchaguzi Mkuu wa 2025 unavyokaribia, idadi ya wanawake wanaotia nia kugombea nafasi za udiwani, ubunge na uwakilishi imeongezeka kwa kiwango kikubwa ikilinganishwa na mwaka 2020.

Ni dalili ya ujasiri, elimu na hamasa ya kijinsia katika uongozi wa kitaifa ,ishara kwamba wanawake sasa wanajitokeza kwa kujiamini zaidi kushika hatua za maamuzi.

Mwelekeo huu si wa bahati, bali ni matokeo ya juhudi za muda mrefu za serikali, mashirika ya kiraia na jumuiya za kimataifa kuhimiza usawa wa kijinsia katika uongozi.

Kwa mujibu wa takwimu za uchaguzi wa mwaka 2020, Zanzibar ilirekodi idadi ndogo ya wanawake waliofanikiwa kushinda nafasi za uongozi. Kati ya wagombea wa ubunge walioteuliwa na vyama, wanaume walikuwa 257 na wanawake 81, ambapo wanawake walioweza kushinda walikuwa wanne pekee.

Lakini mwaka 2025 hali imebadilika. Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imekamilisha uteuzi wa wagombea kwa Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu, ambapo Wagombea wa Urais wa Zanzibar 11, wagombea wa Baraza la Wawakilishi 484 ,Wagombea wa Udiwani 341.

Takwimu hizi zinaonyesha ongezeko kubwa la wanawake walioteuliwa na vyama kugombea nafasi hizo, jambo linalothibitisha kuwa sauti ya mwanamke sasa inasikika kwa nguvu zaidi kwenye uwanja wa siasa.

Kwa upande wa vyama vya siasa navyo mambo yamebadilika kila chama kimeimarisha ongezeko la viongozi wanawake . 



Kaimu Katibu Mkuu wa chama cha National Reconstruction Allince  NRA, Ulimwengu Mkandama, amesema mwaka huu umeleta mafanikio makubwa kwa chama chake.

“Mwaka 2020 tulikuwa na wabunge tisa wanawake, lakini mwaka huu 2025 tumefikia 21, wakiwemo wawili wenye ulemavu. Tulikuwa na madiwani wanne, sasa tumekuwa saba, na tumepata wawakilishi watatu wa kike”.Amesema Mkandama 

Mikataba mbalimbali imekuwa nguzo muhimu katika kufanikisha mwamko huu ,Mkataba wa CEDAW (1979) , unazitaka nchi wanachama, ikiwemo Tanzania, kuhakikisha wanawake wanashiriki kikamilifu katika uongozi na maamuzi bila ubaguzi.



Azimio la Beijing (1995)  Linahimiza serikali kuondoa vikwazo vinavyowanyima wanawake fursa ya kushiriki kwenye maamuzi na kuweka mikakati ya kufikia uwiano wa kijinsia.

Kwa upande wa chama cha ACT Wazalendo, Msemaji wa Sekta ya Maendeleo ya Wanawake, Watoto na Makundi Maalum, Halima Ibrahim Mohmmed , amesema katika Chama chao hawakubaki kuwa nyuma wamendelea kuwahamasisha wanawake kushiriki kwenye uongozi na kuendelea kuitika mwaka huu.

“Mwaka 2020 tulikuwa na wagombea watano wa ubunge, mwaka huu wameongezeka hadi sita. Wawakilishi walikuwa wanne, sasa ni watano. Hii inaonyesha mwamko wa kweli wa wanawake katika chama chetu na ninaimani takwimu hii itaongezeka .” Amesema Halima 

Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs)  Hususan Lengo la 5, linasisitiza usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake katika ngazi zote za uongozi.

Mkataba wa Maputo (2003) Unazihimiza nchi za Afrika kuweka sera na sheria zinazowawezesha wanawake kushiriki katika nafasi za maamuzi ya kisiasa.



Chama cha NCCR-Mageuzi pia kimeonyesha mabadiliko , kwani mwaka 2020 hakukuwa na wagombea wanafasi mbalimbali ikiwemo uwakilishi, ubunge, urais, pamoja na udiwani lakini mwaka huu mambo yamebadilika.

“Mwaka 2020 hatukuwa na muamko wa kugombea nafasi za urais, uwakilishi, ubunge pamoja na  udiwani. Lakini mwaka huu tumepata nguvu mpya  tunagombea nafasi zote, ikiwemo urais, wawakilishi wanne, madiwani wanne na wabunge wanne.”Amesema Laila

Mashirika ya wanawake Zanzibar yamepongeza muamko huo ikiwemo TAMWA-Zanzibar imetambua mchango wa wanawake 13 wanaotegemewa kugombea nafasi ya urais na umakamu wa rais katika Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 2025 sawa na asilimia 36 ya wagombea wote 36 walioteuliwa na Tume ya Uchaguzi ya Taifa (INEC) kwa ngazi hizo mbili.

Kwa upande wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, wagombea wanawake ni watatu, Dk. Samia Suluhu Hassan Chama Cha Mapinduzi (CCM) Rais anayetetea kiti chake, Mwajuma Mirambo Chama cha Union For Multiparty Democracy (UMD), Swaumu Rashid Chama Cha United Democratic Party (UDP) .

Huku nafasi ya Mgombea Mwenza imevutia wanawake 10, akiwemo Chumu Juma Abdallah  Chama Cha Alliance For Africa Farners  Party (AAFP), Fatma Abdulhabib Fereji (ACT-Wazalendo), Devotha Minja (CHAUMA) na wengineo.



TAMWA imesema kati ya wagombea hao, tisa wametokea Zanzibar mmoja katika nafasi ya urais na nane kama wagombea wenza, jambo linaloashiria historia mpya ya ushiriki wa wanawake katika nafasi za juu za siasa.

“Takwimu hizi zinaonyesha wazi kuwa wanawake wa Zanzibar wanaendelea kuvunja vikwazo katika uongozi wa kisiasa, jambo linaloashiria historia mpya ya ushiriki wao katika nafasi za juu za maamuzi,” 
                            MWISHO

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...