Skip to main content

WANAFUNZI KIDATO CHA 6 KIWANI WASEMA TAYARI DK. MWINYI KESHAREJEA TENA IKULU

 

 

 HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

WANAFUNZI kidato cha sita, skuli ya sekondari ya Kiwani wilaya ya Mkoani Pemba, wamesema tayari Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi ‘CCM’ Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesharejea tena Ikulu, kufuatia utekelezaji mkubwa wa Ilani, sekta ya elimu.

Walisema, kujengwa skuli ya kisasa ya ghorofa na yenye vifaa vya kisasa vya sayansi, ni ishara ya kukubalika kwake, na tayari wanamuona ameshaingia ikulu kwa awamu ya pili.

Wakizungumza na waandishi wa habari wa Unguja, Tanzania bara na wenyeji Pemba jana Septemba1, 2025, kwenye ziara maalum ya kuangalia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, walisema kwenye sekta ya elimu Dk. Mwinyi, hana mpinzani.

Walieleza kuwa, ndani ya jimbo hilo la Kiwani pekee, zipo skuli zaidi ya tatu za ghorofa, ikiwemo yao, yenye vifaa vyote husika.

Mmoja kati ya wanafunzi hao, Saleh Muhisn Haidar, alisema Dk. Mwinyi ni kiongozi mwenye maono na anayefikiria mbali, katika sekta kadhaa, ingawa ya elimu amevunja rikodi.


Alifafanua kuwa, baada ya uwekezaji huo wa skuli yao, watahakikisha wanafanya vyema kwenye mitihani yao taifa, na kuwa matokeo ya mfano.

‘’Kwenye sekta kadhaa kama vile kilimo, afya Dk. Mwinyi amefanya makubwa, ingawa kwenye elimu niseme, amevunja rikodi na sisi tunamuahidi kumrejesha tena Ikulu,’’alieleza.

Kwa upande wake mwanafunzi Rauhiya Ahmed Juma, alisema kwa sasa, skuli yao imekuwa ikiwapa hamasa ya kusoma kwa bidii, kutokana na kupatiwa vifaa vya kisasa.

Katika hatua nyingine, alisema baada ya kumalizika kwa ujenzi wa skuli hiyo, sasa wameanzishiwa kidato cha tano na cha sita, pamoja kujengewa dakhalia.


Mapema Mwalimu Mkuu wa skuli hiyo Ali Simai Makame, alisema kwa hakika Dk. Mwinyi kwenye sekta ya elimu, hawana cha kumlipa, ila asubiri mazuri, kwenye kisanduku cha kura mwezi Oktoba mwaka huu.

Alieleza kuwa, alichokifanya Dk. Mwinyi kupitia Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025, haijawahi kutokezea, na kumfanya kila mdau wa elimu, kuridhia maendeleo hayo.



‘’Ukiangalia ndani ya kipindi cha miaka minne, amefanya makubwa, ikiwemo ujenzi wa skuli hiyo, jambo lililotupa hamasa ya kazi, sisi waalimu,’’alifafanua.

Skuli hiyo ambayo inavyumba vya kusomea 45, vinne vya waalimu, stoo tano, maabara mbili na kubeba wanafunzi 909, kutoka wanafunzi wa zamani 235, waalimu 13 na sasa kuwepo waalimu 26.

Wananchi wa Kiwani akiwemo Mohamed Juma Maalim, alisema kama kuna watu hawajaona matunda ya Dk. Mwinyi, kwa miaka minne, wafike kijijini kwao.

‘’Tuna skuli ya kisasa yenye vifaa kamili, na kwa kazi hii aliyotufanyia, yeye ameshaingia Ikulu asubiri kuapishwa tu,’’alisema.

Nae Aisha Haji Mohamed, alisema kwa sasa watoto wao wanapata haki yao ya elimu, wakiwa ndani ya skuli ya bora na ya kisasa, jambo ambalo hawakulitarajia.

‘’Mimi naona Dk. Mwinyi, hana haja ya kufanya kampeni, aanze tu kujipanga nini anataka kutufanyia kuanzia mwaka 2026,’’alifafanua.

 Mwezi Novemba mwaka 2024, Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, akiwa uwanja wa mpira Konde, alisema, ameshayatekeleza kwa vitendo, aliyowaahidi wananchi, kama ujenzi wa madarasa 2,773.

Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025 iliitaka serikali kujenga madarasa 1,500 ingawa ilishavuuka lengo hilo tokea mwaka 2024, kwa asilimia 184.


Dk. Mwinyi aliyasema hayo, mara baada ya kuifungua skuli ya skondari ya ghorofa tatu Konde, kwenye shereha za miaka minne ya uongozi wake.


Serikali ilipanga hadi kufikia mwaka 2025, iwe imeshajenga vyumba 2,000 vya madarasa katika skuli za Unguja na Pemba, ili kuondoa mikondo miwili.

Alisema kama kuna watu wanapiga porojo waangalie takwimu kutoka wizara ya elimu, zitadhihirisha ahadi zake.

Akizungumza mafanikio mingine, alisema ni kuongezeka kwa bajeti ya mikopo ya elimu ya juu, kutoka shilingi bilioni 11.5 hadi shilingi bilioni 33.4, jambo liliongeza wigo kwa wanafunzi.

Kuhusu ajira za waalimu, alisema wapo waliokwishaajira 3,384 na mwaka huu wa fedha wengine 1,239 wataajiriwa.

Alisema hayo yanafikishwa, kutokana na kuimarika kwa bajeti ya mendeleo ya wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, kwa kufikia shilingi bilioni 518 sawa na ongezeko la asilimia 552.

                      Mwisho

 

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...