Skip to main content

NYUMBA ZA MADAKTARI MKOANI ZAWAPA UHAKIKA WA HUDUMA WAGONJWA

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

DAKTARI dhamana hospital ya Abdullah Mzee Mkoani Pemba, Khamis Suleiman Khamis, amesema kupatikana kwa makaazi ya ya madaktari, wanaofanyakazi hospitalini hapo, kumewapa uhakika wa matibabu wagonjwa wale wa dharurua na wa nyakati za usiku.

Alisema, kazi iliyofanywa na Rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi ya kuwajengea nyumba hizo, imeongeza bidii ya kazi kwa madaktari na kuwahakikisha huduma saa 24 wagonjwa.

Daktari huyo dhamana aliyasema hayo leo Septemba 1, 2025, alipokuwa akizungumza na waandishi mbali mbali wa habari kutoka Zanzibar na Tanzania bara, katika ziara maalum ya kuangalia utekelezaji wa Ilani ya CCM ya mwaka 2020/2025.


Alisema nyumba hizo 74 zimenodoa shida ya madaktari hao, kuishi mbali na kituo chao cha kazi, jambo ambalo lilikuwa likiwawiya vigumu wananchi, wanaohitaji huduma hasa wakati wa usiku.

Alieleza kuwa, baada ya kumalizika ujenzi huo wa nyumba za kisasa, sasa, madaktari wameondokana na changamoto ya makaazi, ambayo ilikuwa ikiwaathiri pia wapewa huduma.

‘’Kuwepo kwa nyumba hizi 74 za kisasa zenye kila kitu mpaka mashine za kufulia nguo, kwanza lazima sisi madaktari tumshukuru Dk. Mwinyi, maana sasa kwanza huduma zimeimarika na madaktari wamepata utulivu wa kazi yao,’’alisema.

Katika hatua nyingine, alisema kwa sasa kumepunguza uwezekano wa utoro kwa madaktari hao, kwa kupata nyumba hizo za uhakika, karibu na kituo cha kazi.

Akizungumzia huduma katika hospitali hiyo alisema, ni kuwepo kwa kipimo cha kisayansi cha magonjwa ya ndani ya mwili na mishipa midogo midogo ‘MRI’, ambapo hapo awali, hakikiwepo.

Kwa upande wao wananchi wa wilaya ya Mkoani, walisema uwepo wa nyumba hizo kwa sasa, wanauhakika wa huduma za matibabu saa 24, jambo ambalo hapo kabla, walikuwa na dhiki nalo, hasa wakati wa usiku.

Mmoja kati ya wananchi hao Khadija Omar Mohamed, alisema hana budi kumshukuru Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi kwa uamuzi wake wa kuzijenga nyumba hizo.



Nae Nassir Abdullkadir, alisema kwa sasa hawana wasi wasi, kwanza kuwepo kwa madaktari kuishi karibu na hospitali, pamoja na kuimrika kwa huduma za matibabu.

Rahima Mohamed Haji, alisema anachosubiri kwa sasa ni kufika siku ya uchaguzi mkuu, kwa ajili ya kumshukuru Dk. Mwinyi kwa kumpigia kura ya ndio.

Wakati huo huo wananchi wa shehia za Kiwani na Kendwa wilaya ya Mkoani, wamesema kukamilika kwa mradi wa ujenzi wa tanki la kuhifadhia maji safi lenye ujazo wa lita milioni 1, kumesaidia kupatikana kwa huduma hiyo, kwa uhakika

Asha Iddi Suwedi, alisema kwa sasa wanauhakika wa kuendesha maisha yake, baada ya ujenzi wa tenki hilo, kumalizika na kupatikana hata umeme unapozimika.

 


Kwa upande wake Afisa Mdhamini wizara ya Maji, Nishati na Madini Suleiman Hamad Omar, alisema tenki hilo ni moja kati ya yale matano, yaliojengwa kisiwani Pemba na Dk. Mwinyi.

Alisema, mradi wa ujenzi huo ambao ulishakamilika tokea mwaka 2022, ulikusudiwa kwa wananchi wa shehia za Kiwani na Kendwa, ingawa kwa sasa, umeongeza shehia nyingine.



Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi aliweka jiwe la msingi wa nyumba za madaktari Disemba 3, mwaka 2024, na sasa tayari zimeshamiwa kwa zaidi ya miaka miwili.

Aambapo kwenye Ilani ya CCM iliyomalizika ya mwaka 2020, ibara yake 183 (k) na ibara ndogo ya (ii) ilitamka kuijenga upya hospitali ya Abdulla Mzee Mkoani na uwekazaji wa vifaa vya kisasa vya tiba vya uchunguzi.

Ziara hiyo ya waandishi wa habari, ilitembelea bandari kavu ya Mkoani, nyumba za madaktari Mkoani, uwanja wa michezo Gombani, kiwanda cha mwani, bandari ya Wete na eneo huru la uwekezaji Micheweni.

           Mwisho

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

Vikausha damu vya mjamzito hivi hapa, umo mchele, udongo, mkaa, chaki Uwezekano wa kuzaliwa watoto wenye udumavu, utapiamlo ni mkubwa

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ ‘’KILA ninapobeba mimba nimezoea kula mchele kwa wingi naweza kusamehe pilau au biriani,’’ ndio maneno ya mwanzao ya Bahati Mohamed Ali (sio jina lake halisi). Nilimfuma akiwa barazani kwake, mjini Ole wilaya ya Chake chake, pembeni yake akiwa na kibakuli cha mwazi, kwa umbali utaona amejaza chakula aina ya pepe, kumbe ni mchele wa Mbeya. Hujichotea kidogo kidogo na kuushindilia mdomoni mwake, huku akiendela kupiga storia na wenzake, bila ya kujali kuwa ujauzito alionayo na mchele huo hauna mwisho mwema. Kawaida yake akiwa mjamzito, kila anapoamka asubuhi anaroweka mchele upatao robo kilo hivi…na baada ya kumaliza kupika, yeye huchukua mchele wake kutafuna (kula). Wakati mwenza wake na watoto wao, wanakula chakula cha mchana, Bahati yeye hukaa pembeni na kibakuli chake cha mchele akiendelea kubahatisha afya yake. ‘’Mimba nyengine hupenda sana kutafuna mchele wa Mbea na nyengine hupenda mchele wa mapembe, kwa kweli huwa nina hamu (kileo), kwan...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...