Skip to main content

KUTISHIWA TALAKA KUNAVYOKATISHA NDOTO ZA WANAWAKE WANAOHITAJI UZAZI WA MPANGO

 



IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@

UZAZI wa mpango ni suala lenye kuleta utata kwa baadhi ya wanajamii ambalo huchukuliwa kwa sura tofauti.

Kwani kuna baadhi yao huamini kwamba, uzazi wa mpango ni kufunga kizazi moja kwa moja, jambo ambalo sio sahihi, kwa sababu ni sawa tu na kusema... ‘kumuachisha mtoto’.

Na kuachishwa mtoto ni kumpa nafasi mama aliejifungua kupumzika kwa ajili ya kuimarisha afya yake na mtoto, hivyo ni sawa na uzazi wa mpango.

Jamii ifahamu kwamba kutumia uzazi wa mpango ni muhimu sana katika kuimarisha afya za akinamama na watoto, kwani dini ya kiislamu imehimiza mtoto kunyonyeshwa miaka miwili.

Qur-an tukufu katika Suratul-Baqara aya ya 233 imeeleza kuwa, ‘Wazazi wa kike wanyonyeshe watoto wao miaka miwili kwa mwenye kutaka kutimiza kunyonyesha…’

Hiyo inaonesha wazi kwamba, kuachisha mtoto kwa miaka miwili ni muhimu sana kwa akinamama kutokana na faida inayopatikana ndani yake.

Lakini kuna baadhi ya akinababa huipa kisogo aya hiyo na kuamua kuwatishia talaka wake zao wanaohitaji uzazi wa mpango, jambo ambalo sio jema.

‘’Wanachukulia ile nafasi waliyonayo, kwa vile wamepewa mamlaka makubwa kwa wake zao, wanayatumia vibaya kwa kuwawekea vikwazo,’’ anasema Salha Hassan Ali Mkaazi wa Mzambarauni Wete.

Anaeleza, na hiyo ni kwa sababu hawajali yale maumivu wanayopitia wajawazito mpaka kujifungua kwao, ndio maana wamekuwa wanyanyasa wanawake.

Amina Khamis Hamad mkaazi wa Tumbe anaeleza, mwanaume anaejitambua na aliesoma dini yake vizuri basi hawezi kumkataza mke wake kutumia uzazi wa mpango, kwani anajua umuhimu wake katika makuzi bora ya mtoto na mke wake.

Fatma Kombo Khamis (sio jina lake halisi) mkaazi Gombani Chake anaeleza, mume wake wa mwanzo aliwahi kusema kuwa, mke wake yeyote ambae atatumia uzazi wa mpango basi ndio talaka yake.

‘’Mimi hakunitamkia lakini alisema mbele yangu kuwa, nimeshamwambia mwenzako kuwa mke wangu yeyote atakaetumia uzazi wa mpango ndio talaka yake,’’ anasimulia fatma.  

Saumu Said Mkiji mkaazi wa Pujini anasema, wanaume wengi hawataki wake zao watumie uzazi wa mpango na huwawekea kikwazo cha kuwatishia talaka, hivyo hubakia kudhoofika kiafya ili tu alinde ndoa yake.

Anasema, hakuna jambo wanaloliogopa wanawake kama kutishiwa talaka na ndio maana hata ikiwa ananyonyesha mtoto kwa miezi mitatu tu basi anachagua kustahamili huku akiumia lakini sio kuachwa.

‘’Afya ya mama na mtoto hudhoofika kwa sababu walio wengi hawana huduma nzuri kwenye familia na pia hawapati muda wa kuwashughulikia watoto wao,’’ anaeleza.



Mwananchi Massoud Juma Abdalla mkaazi wa shehia ya Shungi anasema, wengine wanahofia kukimbia kwa uzazi kwa wale wenye uzazi mdogo na ndio maana, waume zao hawataki kupanga kizazi.

‘’Wanaume wengine huwa wakali sana mpaka kufikia kuwatundikia wake zao talaka, hii sio sawa kwa sababu maumivu anayoyajua ni mwanamke,’’ anasema.

Mzume Juma Faki mkaazi wa Shanake Micheweni alikiri kukataa kutumia uzazi wa mpango yeye na mke wake kwani wanaamini kwamba watoto wengi ndio watakaowaleteamanufaa ya baadae.

‘’Sio mimi tu na hata mke wangu hatutaki tutumie uzazi wa mpango kwa sababu, tukipata watoto wengi jambo nusu yake watakuwa na imani ya kutulea tutakapokuwa watu wazima, ‘wahenga walisema…mapofu mengi mzigo’.

Khamis Makame Khamis wa Shanake Micheweni anasema, wanaume wa shehia yao hupanga uzazi kwa kuoa mke mwengine, kwani inasaidia yule wa kwanza kupumzika.

‘’Labda mwanamke awe mgonjwa lakini ikiwa ni mzima hatukubali uzazi wa mpango, lakini tunajitahidi kuwatafutia samaki kwa wingi, hivyo afya zao zinaimarika,’’ anaelezea.

Mama mmoja ambae hakutaka jina lake litajwe mkaazi Sizini anahadithia, kuna dada mmoja mkaazi wa Micheweni mwenye watoto kumi alijiunga na uzazi wa mpango bila kumpa mumewe taarifa.

Anasema, baada ya kurudi mumewe alimwambia, jambo ambalo lilimkasirisha sana na kupelekea kumshambulia kwa maneno machafu mpaka kumwambia kuwa hamtaki tena ndio maana aliamua kujiunga na uzazi wa mpango.

‘’Lakini huyo alijiunga na uzazi wa mpango kwa sababu mume wake huyo hampi huduma na huondoka kwenda nje ya Pemba kwa biashara zaidi ya miezi mitatu, hivyo aliona ni bora ajiunge kuliko kudhalilika na watoto,’’ anasimulia mama huyo.

Anaeleza kuwa, akinababa wengi hawataki wake zao wajiunge na uzazi wa mpango huku wakiwachia majukumu wake zao na wao kwenda na shughuli zao, jambo ambalo linawadhalilisha sana wanawake na watoto.

Mratibu wa Afya ya Uzazi Pemba Dk. Rehema Abdalla Abeid anasema, suala la uzazi wa mpango kwa akinababa bado ni changamoto, kwani mwanamke hata uwape ushauri basi mpaka amwambie mumewe apate ruhusa.

‘’Sasa wanawake wengine wanaojiamini kutumia, ndipo pale hutishiwa talaka, kutengwa na hata sisi watoa huduma hutishiwa maisha,’’ anasema.

Kwa sababu wanafuatilia mpaka wanamjua daktari aliemshauri mke wake, hivyo hujenga nae uhasama kwani wanakuwa sio waelewa.

Daktari huyo anaeleza kuwa, ndio maana wanataka wanaume washiriki kliniki na wake zao kwa sababu vifo vya mama na watoto vimekuwa vingi na moja wapo ya sababu ni uzazi wa papo kwa papo.

Mratibu wa Ofisi ya Mufti Pemba sheikh Said Ahmad Mohamed anasema, ikiwa mke hana sababu za kisheria basi mume ana haki ya kumkataza, ingawa sio vizuri kumtishia talaka kwani talaka sio jambo la kuchezea.

‘’Hii inaleta shida sana na kupelekea kesi kama hizo za kutundika talaka kujaa, kwa sababu mwanamke ikiwa hakutaki tena na umeshamuwekea kikwazo cha talaka, atakwenda kujiunga tu,’’ alisema.

Anaeleza kuwa, mwanamke anatakiwa kutii amri halali za mume wake na asipotii itakuwa amemuasi, jambo ambalo ni dhambi kubwa.

‘’Lakini ikiwa ana tatizo la kiafya na akaambiwa na daktari kwamba anatakiwa kupanga uzazi, basi mwanamme hana budi kukubaliana na hayo, lakini ikiwa atamkataza itakua amefanya ukatili kwa mke wake,’’ anafafanua.

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui katika hotuba yake ya mwaka wa fedha 2021/2022 ameeleza kuwa, watumiaji wa njia za kisasa za uzazi wa mpango wamepungua kutoka kinamama 63,261 kipindi cha Julai 2020 hadi Machi 2021 na kufikia kinamama 61,379 kipindi kama hicho kwa mwaka 2021/2022.

Kwa mujibu wa chapisho la Huduma kwa Mtoto Zanzibar la Januari 28, 2021 linaeleza kuwa, kiwango cha matumizi ya njia ya kisasa ya uzazi wa mpango kwa wanawake wenye umri wa miaka 15-24 ni kwa asilimia 2 kisiwani Pemba, ambapo kinatofautiana kati ya asilimia 1 hadi 12 kwa Unguja.

Katika ukurasa wa Jumuiya ya Wauguzi Zanzibar uliochapishwa Agosti 2019, umefafanua kuwa, licha ya elimu inayotolewa na sera mbali mbali zilizowekwa na Serikali ingawa matumizi ya mbinu za kisasa za uzazi wa mpango visiwani Zanbzibar yapo chini ikilinganishwa na Tanzania bara.

Ambapo Tanazania bara yaliongezeka karibu mara tatu kati ya mwaka 1996 hadi 2015 huku visiwani Zanzibar yakiongezeka kwa kiasi kidogo kutoka asilima 8 hadi 14.

                                      MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da...

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’...

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 m...

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa uf...

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kuta...